Hivi ni nani anawadanganya watanzania kuwa lockdown haifanyi kazi? Hata kama tumeigomea, tuache kupotoshana!

Hivi ni nani anawadanganya watanzania kuwa lockdown haifanyi kazi? Hata kama tumeigomea, tuache kupotoshana!

Hivi mnavyofananisha Ohio na Mikoa Masikini ya Tanzania huwa mnafikilia kwa kutumia Nini?
Tanzania hii kwa Mfano Dar es salaam, zaidi ya 50% Wakazi wake ni wale wanaotoka asubuhi kubaingiza jioni arudi na chochote kwa Familia, ukimfungia kwa week 3 asitoke nje atakula nini na Watoto?

Tuache Ubinafsi, mimi siipendi CCM, kuna baadhi ya mambo sikubaliani na Mh. Rais ila katika hili nam support 1,000%

Hatutaki Lockdown, but stay safe, Vaa PPE na Mwisho wa siku lazima maisha yaende!
Kiujumla, unapokubali ku"-stay safe", tayari umekwishajiwekea 'lockdown' kiaina. 'Measures' zoote za ku'stay'safe' zinahimizwa kufuatwa katika lockdown' ya aina zote.
 
Unadhani kwa nini Rwanda inagawa Chakula kwa Raia wake kipindi hiki cha Lockdown?
Haya unasema kugawa chakula Rwanda, na hapo hapo unaona Dar hawawezi kugawa chakula huku sisi wenyewe tukijigamba kulisha mataifa mengine.
Kwa hiyo ni bora zaidi ku'risk' maisha ya watu wetu kuliko kuyaokoa kwa kuwagawia chakula ambacho tunao uwezo nacho?
 
Kuna mifano pia ya nchi ambazo hazijafanya ,,lockdown” na ziko vizuri na kufanikiwa zaidi klk zile zilizofanya, mfano Taiwan ingawaje ipo karibu kabisa na China na ni moja kati ya nchi za kwanza kabisa kushambuliwa lkn haikufanya ,,lockdown” na sasa hivi Taiwan ni success story kwenye kupambana na virusi vya corona, hata Sweden haikufanya lockdown na bado wametoka vizuri klk nchi zilizofanya lockdown kama Italia au Uingereza, isitoshe swala hapa siyo kwamba lockdown inasaidia au la, bali swala ni kwamba nchi nyingi hata zilizoendelea haziwezi kumudu lockdown, na watu wengi zaidi watakufa kutokana na madhara ya lockdown kuliko corona, wengi wamepoteza kazi, wamepoteza Health insurance, hata Afrika kwetu wanaokufa na njaa ni wengi kuliko wa corona, hiyo ndiyo argument, kwamba lockdown inaumiza zaidi kuliko kuponya, ...
Hivi mbona watu waongo sana 😂😂😂 Sweden wanafanya vizuri wakati wenzako wanataabika huko na ndiyo wanaongoza kwa vifo kwa Nchi za Scandinavia, Italy walifanya baada ya mambo kuchacha same as UK alitaka kujaribu mbinu ya ndugu yako ikalipuka walivyokuja kupata akili ikawa too late. Vipi Brazil mbona hamuitaji na walijigamba kuwa Corona mafua tu sasa hivi chamoto wanakipata. Tuombe Mungu atuepushie hichi kikombe ila tusitake kujaribu kupotosha watu kwa mfano ya uongo na kijinga
 
Kiujumla, unapokubali ku"-stay safe", tayari umekwishajiwekea 'lockdown' kiaina. 'Measures' zoote za ku'stay'safe' zinahimizwa kufuatwa katika lockdown' ya aina zote.
Unaweza kwenda kwenye shughuri zako za kila siku bila kuwa Under Lockdown na Uka stay safe.....
 
Hilo swali la kufananisha ulijibu wewe kwa maana ndiye unayelilia lockdown kama USA, mimi nimekupa tu mifano kwa maana wewe umekuja na mifano ya Ohio, USA kuhalalisha lockdown kwetu, isitoshe lockdown inahitaji nidhamu zaidi ili ifanikiwe kuliko kutokuwa nayo, ...
Wewe si ndiye umetolea mifano ya Sweden na Taiwan? Kwa taarifa yako, hata kule wanakoanza kufungua sasahivi, bado wanajali kuhusu social distancing! Hata wakifungua, wanahakikisha kuwa namba ya watu wanaoingia ni idadi ambayo inaruhusu social distancing, yani kunakuwa hakuna msongamano. Hayo ni mambo yanayohitaji uongozi na mikakati.
 
Unaweza kwenda kwenye shughuri zako za kila siku bila kuwa Under Lockdown na Uka stay safe.....
Ndipo hapa naona wengi wanataka kupotosha wananchi kwasababu za kisiasa! Kwasababu sasahivi naona ni kama “hakuna corona”, na watu hawachukui hatua. Kumuiga Trump kwa kuacha kuvaa barakoa nayo ni makosa makubwa kabisa.
 
Haya unasema kugawa chakula Rwanda, na hapo hapo unaona Dar hawawezi kugawa chakula huku sisi wenyewe tukijigamba kulisha mataifa mengine.
Kwa hiyo ni bora zaidi ku'risk' maisha ya watu wetu kuliko kuyaokoa kwa kuwagawia chakula ambacho tunao uwezo nacho?
Mkuu nashukuru kwa nondo za ukweli. Wape makavu! Saafi sanaa!
 
Haya unasema kugawa chakula Rwanda, na hapo hapo unaona Dar hawawezi kugawa chakula huku sisi wenyewe tukijigamba kulisha mataifa mengine.
Kwa hiyo ni bora zaidi ku'risk' maisha ya watu wetu kuliko kuyaokoa kwa kuwagawia chakula ambacho tunao uwezo nacho?
Nchi hii haina Uwezo huo wa kuwagawia Raia chakula..... Hilo moja.

Pili.
Huwa kuna baadhi ya Maeneo huwa na njaa na Serikali hupeleka chakula cha msaada, I hope unajua Kile kinachotokea!
 
Tanzania raha ,tunaongozwa na kiongozi mwenye akili na uwezo mkubwa sanaa..... thanks God

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Hivi mbona watu waongo sana 😂😂😂 Sweden wanafanya vizuri wakati wenzako wanataabika huko na ndiyo wanaongoza kwa vifo kwa Nchi za Scandinavia, Italy walifanya baada ya mambo kuchacha same as UK alitaka kujaribu mbinu ya ndugu yako ikalipuka walivyokuja kupata akili ikawa too late. Vipi Brazil mbona hamuitaji na walijigamba kuwa Corona mafua tu sasa hivi chamoto wanakipata. Tuombe Mungu atuepushie hichi kikombe ila tusitake kujaribu kupotosha watu kwa mfano ya uongo na kijinga

Hakuna nchi ambayo haitaabiki na corona Ulaya, lkn waliofanya lockdown hawako vizuri zaidi kuliko waliofanya ndicho nilichomaanisha, na kama una ushahidi kwamba Sweden imeathirika zaidi na corona kuliko nchi nyingine za Ulaya, karibu uweke hapa, ...
 
Eritrea hawajapiga lockdown na wamemaliza ugonjwa .. lockdown sio tiba ya corona ni njia ya kupunguza maambukizi kama ilivyo kuosha mikono kwa sabuni na maji


It is never too late to begin. Start now
 
Wewe si ndiye umetolea mifano ya Sweden na Taiwan? Kwa taarifa yako, hata kule wanakoanza kufungua sasahivi, bado wanajali kuhusu social distancing! Hata wakifungua, wanahakikisha kuwa namba ya watu wanaoingia ni idadi ambayo inaruhusu social distancing, yani kunakuwa hakuna msongamano. Hayo ni mambo yanayohitaji uongozi na mikakati.


Nimetoa hiyo mifano baada ya kusoma ulichoandika na wewe kutumia mifano ya Ohio, USA kutaka kuhalalisha lockdown TZ, ...
 
Naona kumekuwepo na hali ya upotoshaji nchini kuwa hatua za lockdown hazina manufaa! Hili naona kama ni upotoshaji ambao unasababishwa na ukweli kwamba viongozi wengi wameingiza siasa kwenye vita dhidi ya corona na matokeo yake ndo haya ya upotoshaji pamoja na mambo mengine.

Mifano iko mingi, lakini kuna mfano nilioamuwa kuutumia kujenga hoja yangu. Mfano huu ni wa gavana wa Ohio kule marekani anayeitwa Mike Dewine! Huyu alichukuwa hatua zote kabla ya Trump! Pamoja na kwamba Trump anaogopeka na viongozi wengi ndani ya republican mfano maseneta na magavana, huwa wana wasiwasi kupingana naye kwasababu ya umaarufu alio nao ndani ya chama cha Tembo ama Republicans!

Sasa huyu alichukuwa hatua za lockdown toka mwanzo kabisa wakati Trump akiwa analeta utani na gonjwa hilo! Matokeo yake, jimbo lake linafanya vizuri sana na yeye amekuwa maarufu siyo tu kule Ohio, bali marekani nzima! Alikuwa na guts za kufanya maamuzi sahihi ya kulinda raia wake kuliko rais wa nchi!

Jimbo lake lina maambukizi machache na vifo vichache sana, na wameshaanza kufungua taratibu taratibu. Pia jimboni kwake alifanya mkakati siyo wa total lockdown, hiyo ni baadhi tu ya sehemu. Wale wanaojitetea kuwa lockdown ni mbaya, wanawaongopea wananchi kwa manufaa yao binafsi, most likely uchaguzi. Ni bora waseme lockdown siyo njia muafaka kwasababu ya mfumo wetu wa uchumi ulivyo na maisha ya wananchi wake, lakini haina maana kuwa partial lockdowns hazifai. Na lockdowns kwenye maeneo korofi.



Bila kupoteza muda, naweka hiki kipande hapo chini chenye kusapoti ninachokisema, pia link kama ukitaka kusoma habari yote na kujiridhisha wewe mwenyewe kuwa nisemayo ni kweli.

Mike Dewine gavana wa Ohio, alipata umaarufu hata kumzidi Trump ambaye naye akaanzisha utaratibu wa kuongea na waandishi kila siku, jambo ambalo Dewine alikuwa akilifanya jimboni kwake kila siku saa sita mchana, na wakati huo wana Ohio wanakuwa kwenye luninga zao wakimsikiliza. Ndiyo wakaanzisha usemi wa it’s “12’oclock somewhere...wine with mr Dewine”, ambapo wanapata wine wakimsikiliza Dewine. Wala hawa kuwa na habari na Trump!


A Republican, he took early and bold actions to lock down his state, even as the head of his party, President Trump, dismissed the threat of the pandemic.



Ohio’s G.O.P. Governor Splits From Trump, and Rises in Popularity

Kwahiyo ndugu watanzania wenzangu, kabla ya kufanya upotoshaji, jiridhishe kwa kautafiti kidogo tu ili uweze kuwa huru kifikra! Ikifkia mahali unamkabidhi mtu mwingine afikirie kwa niaba yako, ujuwe kuna shida kubwa sana! Kusema lockdown haisaidii, ni sawa pia na kusema “to hell with social distancing”. Huwezi kuwaambia watu wafuate masharti kwa ugonjwa ambao siyo hatari kabisa kwa jinsi unavyochuliwa kutokana na hatua za viongozi wetu.

Siyo sahihi kusema lockdown haisaidii kwasababu zenu za kisiasa! Kwanza ingekuwa ni kwetu, huyo Dewine angekiona cha mtemakuni! Lakini kwasababu ya kiasi cha demokrasia na mfumo wao wa uongozi, Dewine aliweza kuchukuwa maamuzi muhimu kwenye jimbo lake kinyume na rais wa nchi! Na ameonekana kwamba alikuwa sahihi na kiongozi shupavu! Nyota yake inang’ara! Trump hawezi tena kusema kuwa lockdown haisaidii! Na Tanzania siyo sahihi kusema hivyo, semeni tu hamkuchagua lockdowns kwasababu mtakufa njaa.

Mag3 Nguruvi3 JokaKuu Kalamu1 imhotep Detective J
Lockdown, begins with you

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaweza kwenda kwenye shughuri zako za kila siku bila kuwa Under Lockdown na Uka stay safe.....
Ndiyo, inawezekana..., hakuna anayelikataa hilo.
Upotoshaji ni hapo mnaposisitiza kuwa maana ya lockdown ni kusitisha shughuli zote. Hii siyo kweli

Na ni mhimu kujua maana ya kuweka 'lockdown' ni nini. Sisi tunakataa tu bila hata ya kuelewa 'lockdown' inakusudia kufanya nini.

Sio swala la kuzuia tu watu wasitoke nje, au wasifanye shughuli zozote wakiwa wanafuata maelekezo yote ya kuzuia maambukizi.

Sisi tunahimiza watu waende makanisani, huku tukifunga shule zote. Hapo huone 'contradiction' yoyote na kuonyesha kwamba tunaamua tu kufanya yanayotupendeza bila hata ya kuweka fikra nyuma yake?
 
Nimetoa hiyo mifano baada ya kusoma ulichoandika na wewe kutumia mifano ya Ohio, USA kutaka kuhalalisha lockdown TZ, ...
Hata kama hawajatangaziwa lockdown, wanamudu social distancing na mikusanyiko hakuna! Msiwapotoshe watanzania kwa tamaa za madaraka!
 
Nchi hii haina Uwezo huo wa kuwagawia Raia chakula..... Hilo moja.

Pili.
Huwa kuna baadhi ya Maeneo huwa na njaa na Serikali hupeleka chakula cha msaada, I hope unajua Kile kinachotokea!
Hapana.
Hilo moja, sikubaliani nalo, na wala hata huelezi inakuwaje Rwanda wagawe lakini sisi tushindwe na Dar peke yake. Tena sio kila raia aliyeko Dar atahitaji kugawiwa chakula.

Hilo la pili; sijui "kile kinatokea" baadhi ya maeneo wanapogawiwa chakula wakati yanapokumbwa na njaa. Ukieleza naweza nikaelewa, na kukubali/kukataa ikibidi.
 
Back
Top Bottom