Hivi ongezeko la mshahara linalofanywa kisiasa kwa kupunguzwa kodi kwa asimilia 01 lina matokeo gani?

Hivi ongezeko la mshahara linalofanywa kisiasa kwa kupunguzwa kodi kwa asimilia 01 lina matokeo gani?

Hakuna faida yoyote kwa mfanyakaz coz basic inabaki vilevile na hakuna nchi kukua kiuchumi kama Samia ataogopa kutake risk kama mtangulizi wake.
So its change la macho as waswahili say!
 
Ndugu iko hivi, kwanza lazima ujue hilo punguzo la asilimia moja, Linawahusu wale tu wenye vipato vya chini yaani utahusika hapo kama unapokea mshahara wa 270,000-520,000.
Sasa twende vizuri hilo kundi hapo juu walikuwa wanakatwa kodi asilimia 9 ya mshahara wanaopokea.
Jana mama samia kasema atawapunguzia asilimia moja, kwenye hiyo asilimia 9 ili ibaki asilimia 8.

Sasa tuchukulie mfano mtu aliekuwa analipwa mshahara wa 300,000 kabla mama hajawapunguzia hiyo asilimia moja
300,000×9%=27,000 huyu mtu alikuwa analipa elfu ishirini na Saba.
Baada ya punguzo la asilimia 1 ikabaki asilimia 8
300,000×8%=24000.
Sasa huyu mtu mwisho wa mwezi badala ya kukatwa 27,000 atakuwa akikatwa 24000 ..so 27000-24000=3000 atapata unafuu wa 3000 kwa mwezi ya kunywa maziwa
Sidhani kama badiliko la shilingi 3,000/- linaweza kutangazwa kwa namna ile pale Mei Mosi - ninaona kupata jibu zuri ni kusubiri tu. Shilingi elfu 3 kama ni kweli itakuwa ni dharau kwa wafanyakazi wa Tanzania.
 
Back
Top Bottom