Ndugu iko hivi, kwanza lazima ujue hilo punguzo la asilimia moja, Linawahusu wale tu wenye vipato vya chini yaani utahusika hapo kama unapokea mshahara wa 270,000-520,000.
Sasa twende vizuri hilo kundi hapo juu walikuwa wanakatwa kodi asilimia 9 ya mshahara wanaopokea.
Jana mama samia kasema atawapunguzia asilimia moja, kwenye hiyo asilimia 9 ili ibaki asilimia 8.
Sasa tuchukulie mfano mtu aliekuwa analipwa mshahara wa 300,000 kabla mama hajawapunguzia hiyo asilimia moja
300,000×9%=27,000 huyu mtu alikuwa analipa elfu ishirini na Saba.
Baada ya punguzo la asilimia 1 ikabaki asilimia 8
300,000×8%=24000.
Sasa huyu mtu mwisho wa mwezi badala ya kukatwa 27,000 atakuwa akikatwa 24000 ..so 27000-24000=3000 atapata unafuu wa 3000 kwa mwezi ya kunywa maziwa