Hivi Rais Magufuli alifanya maamuzi ya busara kwa kuwaita Wakuu wa Vyombo vya Usalama kuongelea COVID19, badala ya kuwaita Wataalamu wa Afya?

Wataalamu wa afya walikua katika majukumu


Izo tangawizi na limau ziwe nyingi
The-Monk
Unataka kuniambia kuwa hao wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama hawakuwa na majukumu mengine?

Ni watu wachache sana waliohitajika kwenye kikao hicho cha Rais, ambao ni waziri Mkuu na waziri wa Afya, kwa hiyo usitafute sababu za "ku-justify" maamuzi ya Jiwe
 
Mkuu
Ilo jibu nililiandika tu ili nifurahi

Kwa sababu jiwe kashafanya hatuna case mpya

Ongeza tangawizi na limau

Twafa
 
Maslahi ya umma ndio muhimu, yale ya wapigaji hayapaswi kukuumiza kichwa.

Ukimsikiliza kila mtu wasio na shukrani baadae watakuita dhaifu.
Hayo maslahi ya Umma ndiyo yapi hayo?

Unaweza ukaita hiyo ya kuwaita wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini kuwa ndiyo maslahi ya Umma??

Mimi naona kama angekuwa amewaita wataalamu wa Afya akawahutubia na baadaye akaruhusu maswali ya papo kwa hapo, hicho kikao ndiyo kingekuwa cha maslahi mapana ya Umma
 
Katika wageni waalikwa aliapishwa mmojawapo ambaye nu mtu wa afya, ujumbe wa afya unakwenda kufanyiwa kazi kupitia yeye.

Umuhimu wa ulinzi na usalama ni kitu muhimu sana ndio maana nchi yetu ipo salama.
 
Mimi kilichonistua na nikadhani kua jamaa wenda siyo mTanzania halisi ni hali ya kuona jambo aliloliita ya kupumbavu inafanyika yeye yupo kimya then anakuja kuibuka baadae ..sijui ingekua na madhara kwa wananchi angesemaje.
 
Amefanya busara kwa sababu hawa watamuelewa zaidi kuhusu tiba ya mvuke kuliko wataalamu wa afya.
 
Labda corona ingekua TZ peke yake ningeunga mkono haya uyasemayo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alikataza wagonjwa wapya wa corona kutangazwa
Ni utaratibu wa WHO ni lazima utaje kwa uwazi, idadi ya wanaoambukizwa, idadi ya wale waliopona na idadi ya waliokufa

Sasa yeye alitaka kufanya siri siri, kama alivyozoea kufanya mambo yake mengine??
 
Sababu za kuwa lilivyo sasa zipo za kisayansi mkuu, tatizo hakuna ukamilifu katika kila akifanyacho binadamu.
Mbona wenzetu wanafanikisha.Tusipoweka Sheria za kuwafunga viongozi yaani wakitoka madarakani ni jela maisha wataendelea kuchezea Kodi zetu na maendeleo tutayasikia kwenye radio
 
Mbona wenzetu wanafanikisha.Tusipoweka Sheria za kuwafunga viongozi yaani wakitoka madarakani ni jela maisha wataendelea kuchezea Kodi zetu na maendeleo tutayasikia kwenye radio
Sisi tunafanikisha tena sana tu, inategemea wewe binafsi mtazamo wako upo vipi.

Kama glass imejaa nusu kwenda juu au imepungua nusu kwenda chini, hilo ni suala la akili yako binafsi.
 
Tulishaandika hapa hidden facts in President magufuli's speech on 22th aprill 2020 - jamii forums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…