Hivi Serikali hii mna tatizo gani kutolipa wastaafu mafao yao? Hii ni laana mtaua wazee wa watu kwa mawazo

Hivi Serikali hii mna tatizo gani kutolipa wastaafu mafao yao? Hii ni laana mtaua wazee wa watu kwa mawazo

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Haiwezekani mtu mwaka unaisha anafuatilia pesa yake na amekwisha staafu anazungushwa tu hakuna majibu ya kueleweka. Hivi huyu mzee mnata aingie mtaani aishi vipi wakati mshahara hana na pesa anazodai ni zake?

Hii siyo kujitafutia laana na chuki ni kitu gani? Mnadhani kiwango cha chuki nchini mwetu kiko juu, mnadhani kwa hali hii watu watalipendaje taifa?

Wazee hawa kila wakienda kwenye ofisi za mifuko yao ya hifadhi ya jamii wanaambiwa shida haipo kwao, tatizo Hazina ndio hawatoi pesa. Hivi Hazina hizi pesa ni za kwenu? Mtu process zote za kupatiwa pesa zake zimeshakamilika, mnachochelewesha ni kitu gani? Huu ubabe hata kwenye mali za watu utawasaidia kitu gani hasa?

Wabunge wanamaliza miaka yao 5 kabla hata ya kuanza uchaguzi mpya tayari wameshalipwa pesa zao, huu upendeleo ni wa hovyo kabisa na ni madhambi makubwa. Mungu ataendelea kuwalaani wote wanaohusika na kuwasumbua wazee hawa.
 
Mkuu kuwa mpole. Jiandae kisaikolojia kwamba hilo swala haliwezi kupungua miaka 3, unless otherwise una connection.

Ajira shida yake ndio hio,,, miaka yote unaishi ofisini mchana kutwa,, usiku unarudi kulala nyumbani halafu ukistaafu wanakuzingua hela yako wakati ndio muda wa kuishi nyumbani.

Faki politiksi
 
Mimi nadhani uendeshwaji wa mifuko ya hifadhi ya jaamii unahitaji kuboreshwa.na serikali isichukue feda na kupeleka kwingine.mfano mwaka 2022 kutakuwa na sensa,utasikia viongozi wetu wakisema tutafanya sensa kwa fedha za ndani,kumbe Wana chukua kwenye mifuko ya hifadhi.unadhani hapo wastaafu wetu watalipwa kwa wakati?
 
Mkuu kuwa mpole,,, Jiandae kisaikolojia kwamba hilo swala haliwezi kupungua miaka 3,,, unless otherwise una connection...

Ajira shida yake ndio hio,,, miaka yote unaishi ofisini mchana kutwa,, usiku unarudi kulala nyumbani....halafu ukistaafu wanakuzingua hela yako wakati ndio muda wa kuishi nyumbani.

Faki politiksi
Kuna haja gani kuchelewesha mtu kupata mafao ambayo ni pesa zake?
 
Mimi nadhani uendeshwaji wa mifuko ya hifadhi ya jaamii unahitaji kuboreshwa.na serikali isichukue feda na kupeleka kwingine.mfano mwaka 2022 kutakuwa na sensa,utasikia viongozi wetu wakisema tutafanya sensa kwa fedha za ndani,kumbe Wana chukua kwenye mifuko ya hifadhi.unadhani hapo wastaafu wetu watalipwa kwa wakati?
Wanatenda madhambi makubwa sana hawa tu. Ndio maana hatua kujengeana chuki na unakuta watu wanaombeana mabaya
 
Kuna haja gani kuchelewesha mtu kupata mafao ambayo ni pesa zake?

Mkuu mbona bank unapanga foleni japokuwa ni hela zako,,, na ukifika muda wa kufunga hupewi hela, japo pia ni zako..

Tz mafao imekuwa kama chanzo cha mapato kwa serikali na miradi mingi wanayofanyia zile hela kuna wakati huwa hailipi kama walivotarajia so wanavokusumbua ni kwamba wana buy time ili circulation ya pesa iwe ina balance(in&out).

Ukiacha hayo ni UNYANYASAJI NA KUKOSA MIPANGO KWA SERIKALI.. Na uFalla wa baadhi ya tuliowapa mamlaka.
 
Halafu kuna jamaa ana kichwa kama anachungulia kwenye kona anatuambia eti "inji" hii ni dona kantre!What a hopeless fella!Wawalipe wazee wetu.Maccm yanaendaga kukopa kwenye mifuko ya pensheni
wanapigia kampeni na kununua kofia!To hell with CCM regime!
 
Yaani we mwaka tu unaanza kulialia!!
We ulitaka iwe miaka ngapi?
Juzi wakti Jiwe anazungumza na Mapolisi alipokea malalamiko ya MAPOLISI WALOSTAAFU MIAKA 3,2 NA 1 ILIYOPITA NA BADO HAWAJAPA MAFAO YAO!!!
Hivi unajua kwamba kulingana na sheria ya PENSHENI, Mzee akistaafu mwezi huu wa March,2021 basi mwezi April ,2021 aanze kupata mshahara wake wa Pensheni na marupurupu yake yote.
Kawaida miexi 6 kabla ya kustaafu mtumishi, mchakato wa kuandaa stahili zake unatakiwa kuanza mara moja Ili siku ya kuondoka mtu anakabidhiwa mzigo na mwezi unaofuata anaanza kula Pensheni yake.

Tatizo lililopo kwa sasa ni kwamba Utawala huu wa CCM ya Jiwe hauthamini Watumishi wake kiasi kwamba Fedha yote ya mifuko ya Jamii au Akiba uzeeni PSSSF na NSSSF imekopwa kupelekwa kwene miradi mikubwa!!!K.m. SGR, STIEGLERS, KUNUNUA BOMBADIER, KUJENGEA UNIVERSITIES kama UDOM n.k....!!!

Halafu utasikia Jiwe anatamba kwa mbwembwe ati SERIKALI HII NI TAJIRI SANA INAWEZA KUWA DONA KANTRI....kumbe Fedha ya Wastaafu....!!!
Ni aibu kubwa sana kwa nchi hii kuwa na Utawala wa hovyo kama huu!!!
 
Hii issue ni nyeti sana mkuu.Mimi kiukweli hua inanipa shida na ukakasi kuiongelea.Halafu the bad thing is,serikali imekiri ilikopa somewhere around 2.8tri.kwenye mifuko ya jamii,imelipa 1.2 trillion na zimebaki 1.6 trillion.Halafu wanasema wanajua wanadaiwa kiasi hicho, ila wanahakiki madeni.Ni ajabu,una hakiki nini sasa,umekopa rudisha.....!Mimi najua nadaiwa 100,000/= na Mr.X,halafu eti nahakiki!Nahakiki nini sasa?Ridiculous.Mbaya zaidi,nasema with laxity, huku wazee wa watu wakiendelea kuteseka,na wengine hata wanakufa!No, we have serious moral problems kama jamii.Yaani upendo umepoa kabisa.

Na hawa watumishi wanaotesa wazee wa watuu,hivi wamesahau kwamba na wao ipo siku watastaafu?Ajabu sana.
 
Wale waumoja wa jumuhia ilio vunjwaa sijui iliishia wap! inchii hii ?!!
 
Back
Top Bottom