Hivi tukiacha ushabiki ni lazima Diamond aangushe wasanii wengine ili aendelee kutamba?

WCB mengi yamejaa mapunga na mauza mikoba.

Huwa yanabishana kumtetea Domo mpaka midomo into jasho.
 
Abdul ana tofauti gani na Darlin?

Au kutokung'aa kwa Abdul tatizo ni Ally lakini kutokung'aa kwa Darlin tatizo ni Darlin[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Darlene hana kipaji, hilo liko wazi pale yupo yupo tu anabebwa.
Abdul Kiba ni talented hata ukisikiliza anavyoimba lakini tatizo nadhani ni promo au mipango mibovu ya management, kwa kipaji chake angekuwa na Diamond angeshafika levels za akina Harmo, Vanny, Mbosso au Lavalava.
Kwa sasa anazidiwa hata na Ibra na Mac Voice, yeye akiitisha show na Mac Voice akaitisha show ya Mac Voice itajaza zaidi ya show ya Abdul Kiba.
 
Kwa akili yako kama mtu mzima Diamond anawezaje mshusha msanii anaefanya kazi zake mbali na yy, na n kwann ameshindwa mshusha Alli kiba kama ameweza kwa hao wengine....? Hv unaamini wasanii wote walioshindwa kimziki wameshushwa na Diamond...?
Wa Kibakuli huyu
 
Wewe ambaye huna roho ya kukunja umewainua watu wangapi kwenye jamii yako ?
 
Max Voice ndio namsikia kwako, anaimba nin?
 
Hv ukiwa na duka kariakoo mnafanya biashara inayofanana na unauza sana mpk wenzako wanalalamika, hv ili wauzaji wengine wasilalamike inakubidi siku mojamoja usiwe unafungua ili wenzako nao wauze? Au inakubidi wenzako wawe wanawahi kufungua then wewe uchelewe mpk mchana ili na wao wauze ili kuepuka kelele? Mziki ni biashara kama biashara nyingine pambana umpite mwenzako wateja wanunue kwako. Kelele hazisaidii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…