Hivi Uchagani watu wanafundishwa nini kuhusu Pesa?

Hivi Uchagani watu wanafundishwa nini kuhusu Pesa?

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
5,175
Reaction score
16,488
Jamani kwa wale ambao mmewahi kuishi uchagani, watu wa huko wanafundishwa nini kuhusu pesa?

Watu karibia wote wanaotoka uchagani ni wafuatiliaji wazuri sana wa pesa.

Jamii zote zinapenda pesa, ila hii jamii ya watu wa kaskazini ni kama vile ina kitu cha ziada kwenye kupenda pesa.

Hii inatokana na nini wakati pesa haitengenezwi uchagani?
 
Ule mlima sio wa bure tu kwa watu wanao uzunguka!
IMG_0431.jpg
 
Mi ni wa huko lakini amna chochote tunafundishwa.

Ni jamii yetu tu kina babu zetu waliwahi mjini tu, hichi kitu jamii nyingine hawaelewi wachagga hatufundishwi pesa.

Sema tu tuliwahi na bado tunawahi mjini ndiyo hicho tu, mbona wakinga sasa hivi wanawahi mjini na jamii nyingine kama waha, wakuria, wanyakysa, wamakonde, wamaasai, na wasukuma.

hizi jamii nilizo zitaja hapo juu nao pia wanawahi mjini miaka hii japo kuwa walikuta wachagga na wahindi washawahi mjini ni hicho tu kiongozi.

Na kuwahi mjini siyo bongo tu watu wako marekani toka miaka ya 90's mi nina uncle zangu miaka hiyo wapo wanaishi marekani.

Ninafahamu wazee walio wahi kariakoo enzi hizo una ambiwa wana ardhi pale na kijibanda cha mangi, leo hii wana ghorofa ile ardhi imepanda thamani.

Amna cha zaidi kwa wachagga useme kabila nyingine hawawezi kuwa kama wao, japo tu kabila nyingi zimeridhika na maisha mi naona hivo.

kabila hizo mmoja akipata utasikia kaja baba, mama, shangazi, mjomba, mtoto wa baba mkubwa, mawifi, mashemeji, n.k yaani wote wanaenda kwa mji mmoja wa mtu mwenye familia moja wanakula na kulala hapo kisa eti wamesikia anafanya benki.😅😅 hii kitu inafanya mtu ashindwe kujikwamua kiuchumi yaani mtu mshahara laki7 au laki 5 mnamgandaa hivyo hawezi tobo.

kwa wachagga wengi huu utaratibu amna.

yaani wewe ni mgeni ukija kwetu utabidi uulizwe ratiba yako ikoje upo kwetu mpaka lini na kama tuna 3 bedroom tutakuambia hatuna nafasi hivyo utalala huku unatafuta guest japo wakuu mi roho hiyo sina😅😅ila wengi wa wakwetu ninao wafahamu.
 
Hatuna mafunzo yoyote kuhusu pesa ila ni vile thamani ya kila kitu inapatikana kwa pesa.
Hakuna furaha yoyote, amani yoyote, fahari yoyote, haki yoyote katika umaskini.

Na hakuna namna yoyote ya kuondokana na umaskini bila pesa, kwa muktadha huo msimiati wa pesha kule kwetu unazingatiwa sana popote pale utakapo kuwa.
 
wanafundishwa kwamba kidogo kidogo hujaza kibaba,... unaanza mtaji wa kushona viatu (nguvu zako mwenyewe), unaongezeka unapata mtaji wa kuuza karanga, nao unaongezeka unafungua genge ...... baada ya miaka kadhaa una miliki duka la mangi ... anakopesha na kutengeneza conekekishenii na watu .... mtaji unaongezeka
 
Mkuu ukikuliya malez ya wazaz wa kichaga...kuna muda unaweza zani sio wazaz/ ndugu zako...yan ni malez fulan hivi ya kibabe...unaweza ukaona kabisaa wazee hawa cash ipo...lakin mpaka ikufikie umetoa jasho...hawadekez kabisa na misimamo yao ni mikali...lakin ukaja ukakuwa utawashukuru sana...kumbe walikuwa wanakuandaa mbeleni
 
Kuna rafiki yangu mchagga nilimaliza nae chuo mwezi unaofuata akanicheki kwenye simu tukutane sehemu flani jijini dar kufika jamaa ana duka kubwa sana lenye thamani ya kama 20M kumuuliza vp umeweza kufungua duka mapema hivi ananiambia hapa Mama na Baba na Yeye ndio wamejichanga wameona asiozee nyumbani.
 
Kuna rafiki yangu mchagga nilimaliza nae chuo mwezi unaofuata akanicheki kwenye simu tukutane sehemu flani jijini dar kufika jamaa ana duka kubwa sana lenye thamani ya kama 20M kumuuliza vp umeweza kufungua duka mapema hivi ananiambia hapa Mama na Baba na Yeye ndio wamejichanga wameona asiozee nyumbani.
Kwa hilo wachaga nawasifu sana, huwa wana ile spirit ya kubebana sana katika fursa za kimaendeleo na uchumi.
 
Mkuu ukikuliya malez ya wazaz wa kichaga...kuna muda unaweza zani sio wazaz/ ndugu zako...yan ni malez fulan hivi ya kibabe...unaweza ukaona kabisaa wazee hawa cash ipo...lakin mpaka ikufikie umetoa jasho...hawadekez kabisa na misimamo yao ni mikali...lakin ukaja ukakuwa utawashukuru sana...kumbe walikuwa wanakuandaa mbeleni
Umenikumbusha zile enzi soda mpka sherehe
 
wanafundishwa kwamba kidogo kidogo hujaza kibaba,... unaanza mtaji wa kushona viatu (nguvu zako mwenyewe), unaongezeka unapata mtaji wa kuuza karanga, nao unaongezeka unafungua genge ...... baada ya miaka kadhaa una miliki duka la mangi ... anakopesha na kutengeneza conekekishenii na watu .... mtaji unaongezeka
Halafu hili nimeliona, mchagga atakuwa shoe shiner leo ila baada ya muda humkuti hapo tofauti na kabila zingine

Unaweza kumuona mtu mshonaji wa nguo, toka upo primary hadi unamaliza chuo lakini bado yupo mtaa uleule na cherehani ileile

Pia kuna siku nilipanda daladala na dereva mchagga, wakawa wanapiga story na makonda na watu wengine kuhusu faida ya bodaboda. , yule dereva hesabu zake ni kufanya saving ya buku tano per day na anajua hesabu hadi ya miaka miwili na biashara gani atafanyia hicho kiwango cha pesa 😩

Naona kama wana discipline na akili ya kutafuta, kuweka akiba na kukuza kipato chochote walichonacho. Wengi mtihani wetu upo hapa
 
Kuna uzi mmoja upo humu..cjui anaitwa Anunaki kisa cha yy na baba yake...yaan yule mzee ana tabia za kichaga kabisa
 
Sana nimeliona kwa rafiki zangu tuliosoma wote uchagani wazazi&ndugu wanabebana sana miaka miwili mtu kashatoboa.
Waswahili kazi ni kuvimbiana tu 😂😂😂 mtu anaona raha akitoboa awaoshee ndugu zake kuwa ana hela na kubadili magari. Nyie muwe mnalia lia njaa tu.

Hata kama ana connection hawezi kukupa shavu, yupo radhi asaidie watu baki sio ndugu.
 
Back
Top Bottom