Hivi unajua unaweza kutumia akili kidogo tu ukapata pesa nyingi?

Mtoa mada, nikupe pongezi kwa mada yako nzuri inaelimisha na kufungua watu ubongo, wafikirie nje ya box, ila kusema suala la kutumia akili ndogo napinga kabisa, ukitaka jambo lifanikiwe inahitaji akili kubwa, kufanya kazi kwa bidii + commitment

Biashara bila mkakati utaishia kufeli. Na wengi wanaishia kufeli kwa kukurupuka, kama mdau hapo juu ana chance kubwa sana ya kufeli (80%) (compactor) hajui chochote kuhusiana na biashara hiyo, hamna hajafanya market research, hajawai kuifanya ila kwa kuwa umemtajia 50,000/= kwa siku kachanganyikiwa. Sawa kabisa na wale wa kilimo cha matikiti

Ushauri wangu kwa wadau, hamna biashara inayohitaji akili ndogo, biashara zipo na zinaonekana tafuta ambayo una passion nayo, think big start small(kuwa na dira unataka kuifikisha wapi biashara yako) ikikua multiply it,(fungua matawi) ila ni akili kubwa, juhudi, utayari na huduma nzuri zitakufikisha unapopataka ila haya ya mtoa mada mwenye biashara 10 zinazofanya vizuri kwa kutumia akili ndogo mkikurupuka yatawaingiza chaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
13 mega pixel,
Indeed mdau nimeona tu post yako na najua kabisa una experience sana ya biashara. Kama watu hawatachukua kitu chochote katika post yako, kitu kimoja tu angalao basi wazingatie ni ulivyosema kuhusu passion.

Watu nimeona wanapenda kupewa idea za biashara. Na ndio tz yetu unakuta watu wanaiga kila mtu. Creativity na innovation ni ndogo sana. Kila mtu anafanya duka wakati kuna fursa nyingine nzuri tu sana.

Idea ya biashara nzuri kama ulivyosema ni ile ambayo mtu unaguswa sana nayo (you are passionate about it). Na pia ni muhimu na inasaidia mtu kuwa na ujuzi nayo angalao kwa kiasi fulani. Lakini passion huwa inasaidia hata mtu kujifunza hicho kitu kwa moyo sana na akapata ujuzi wa kufanikiwa vizuri kabisa. Vilevile passion itasaidia mambo yakiwa magumu. Sababu mtu ana-enjoy hicho kitu kwa moyoni, hata mambo yakiwa magumu bado anamudu kuendelea kupambana tofauti na kitu ambacho ni kama mzigo.

Mara nyingi watu walioajiriwa wanapenda field zao na ndio maana wamezichagua, na mtu anaweza kuanzia hapo. Kama mtu ni accountant, anaweza anzisha huduma binafsi ya mambo ya accountancy au hata akasaidia mambo ya hesaby za kifedha pamoja na mambo ya ushuru (taxes) kwa biashara ndogo ndogo kwa kuanzia. Kama mtu ni mwalimu, anaweza anzisha ufundishaji wa tuition hata nyumbani kwake kwanza. Kama ni computer expert, kuna njia nyingi ya kuanza kutoa huduma binafsi.

Point nyingine kubwa umesema ni kuhusu kuanza na kidogo huku mtu akiwa na lengo kubwa (Start small, but think big. Hata ngazi mtu unapanda kuanzia chini. Mtu anafanya kitu kwa moyo huku akibuni na kujifunza njia za kukuza kampuni ikawa kubwa sana baadaye. Mhasibu akawa na kampuni kubwa ya accounting and finance, mwalimu baadaye akawa na shule binafsi, computer expert pia hivyo hivyo.

Asante sana kwa mchango wako mjasiriamali mwenzangu.
 
DocJayGroup,
TANGAZA BIASHARA: Biashara ni kuitangaza (Marketing). Bila marketing, hakuna kitu. Kama mhasibu unaanzisha huduma ya kusaidia biashara ndogo ndogo mambo ya hesabu za fedha, mambo ya TRA nk, ni lazima ukatangaze huduma hiyo. Wafanya biashara wakufahamu. Kama ni mwalimu wa tuition. Hivyo hivyo. Unatangazia wazazi, wanafunzi nk.

MATOKEO: Lakini pia lazima matokeo (results) za huduma yako ziwe nzuri. Wanafunzi wasaidike. Tuition unayotoa ilete mabadiliko chanya. Hakika watakuja na kuja na kuja. Kama ni huduma ya uhasibu poa hivyo hivyo. Mtu unasaidia biashara ndogo zinaepuka matatizo ya TRA nk. Unawaonyesha hata namna ya kufanya mahesabu wao wenyewe nk.

Marketing italeta wateja, lakini Matokeo mazuri ndio yatakayofanya wateja walete wateja wengine na biashara ikue.
 
Shukrani sana mkuu kwa kushare nasi ideas ambazo kwa macho ya kawaida hauwezi kabisa kuziona .
 
Shukrani mkuu vp Biashara ya kununua air compreser kwa ajili ya kujaza upepo hivi ukimuachia mtu si anakuibia tu pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
Biashara ambazo huwezi kujua kama hela imeingia au haijaingia,makabidhiano ni kwa makubaliano maalum,mfano bodaboda akipewa dereva hesabu kwa siku ni 8000 kila siku,hii 8000 kila siku ni "lazima"


afanye kazi asifanye boss haimuhusu,anataka 8000 yake iwe pale pale. na pia Kwenye hii Air compreser nayo hesabu ni kama boda boda,daladala,nk


kwanza kabla ya kumpa/kumuajiri mtu kaa kazini boss wewe mwenyewe kwa mwezi 1,hii ni ili kujua ofisi kwa siku inaingiza sh ngapi,ukikaa mwezi kisha kila siku ofisi inaingiza 15,000 kwenda mbele (tayari umeshajua income ya ofisi yako)


ndipo unaleta mtu sasa unamwambia kuwa nakupa ofisi hiii nataka kila siku unipe 10,000 unamwambia 10,000 lakini unajua kabisa anapata zaidi ya 10,000 lakini unamwambia vile ili nayeye apate chochote kitu,kwahiyo kwenye hii 10,000 hamna maelezo ya biashara mbaya au nzuri

hela ya ofisi 10,000 inahitajika,kama hawezi mweke pembeni Hafai huyo,ataekubali mpe kazi.
 
CONTROLA,
Ila pia asisahau huyo mtu atakayemweka awe ni mwaminifu sana kwa asilimia zote. Binafsi naamini watu wasio na uaminifu mkubwa, hawastahili kabisa kusimamia biashara.
 
DocJayGroup
Kwanza nitoe pongezi kwa kuweza kuchangamsha mada hii ,maana biashara yoyote bila kuingia lazima tujaribu ku analyse risk mbalimbali zinazoweza tokea. Watanzania wengi tunapenda kufanya investment kwa ajili ya generate pesa na pia wengi wetu tunapenda kufanya biashara ambazo sisi hatutojishughulisha nazo na ndio mwanzo wa matatizo.

Mleta mada kaleta mada nzuri na yenye kumjenga kila mmoja hivyo basi yafaa kila mmoja wetu ajaribu kuangalia risk mbali mbali zinazoweza tokea kabla ya kufanya kitu. Yaweza tokea mtu sasa ameenda chonga vibanda bila kujua wateja wake akiamini baada ya kumaliza kuchonga ata anza kupokea hesabu kwa siku.

Hakuna biashara rahisi kila biashara inachangamoto zake ..take risk kuwa na nidhamu mafanikio utayaona
 
Nimeipenda hii, na jenereta lipo hapa home alinakazi, kama kunaaliye interest tunaweza kushirikiana. Kwa aliye dar
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yani niweke mill 4 huku nikitegemea kupata elfu 80 kwa mwezi hiv unaijua nguvu ya mill 4 wewe hilo sio wazo la biashara
 
Mii nilishafanya hii biashara ya kukodisha vitu tangu mwaka 2001-2003.
Karibu na pale mbezi Sasa kimejengwa kituo Cha mabasi. Niliweka mashine za kupiga matofali, vibao vya matofali, manailoni ya kufunika matofali ikija mvua.
Pia nilikuwa na welding machine 4 niliziweka hapa Sinza kwa Remmy Sasa Pana ukumbi unaitwa majestic hall. Nilikuwa nawakodisha mafundi uchomeleaji.
Nikawa na guta 2 zilikuwa zinapaki manzese.
Ic matumizi ya hivi vitu daah. Mtu akichukua kitu chako anavyokitumia yaani anakikomesha.
Hazingatii uwezo wa kitendea kazi. Mashine ndogo ya welding anataka aweke Moto mpaka mwisho ili skate chuma wakati Ile niya kuungia chuma na sio kukatia.

Baadae nilianza kukodisha screen kwaajili ya kombe la dunia Kama mtakumbuka mwaka 2002 world cup ilifanyika Japan na Korea. Jamaa walikodi mwezi mzima, lkn ilibidi wavunje mkataba kwa sababu hawakuwa na wateja maana mechi zilikuwa zinachezwa alfajili.

Ninachotaka kusema hapa unatakiwa kuwa makini Sana na kifaa chako. Matumizi ya wanaokodi huwa Ni mkomoeni. Vinginevyo kifaa chako kitachakaa kabla ya kukulipa..
Unaweza kukuta chombo kimewekwa upside down. Kipo kwenye vumbi, yaani unaweza kulia.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…