Kura ni siri haijalishi CCM wana wanachama wangapi wanafuatwa na nani,wote hao ni wapiga kura na mara hii nakuhakikishia wafuasi hao wanafanya maamuzi magumu mbele ya sanduku la kupigia kura,wanaweka na kulinda uwanachama wao, ila kura mwaka huu wanaipeleka upinzani,kura ni siri hapa wenye viti na meza wa CCM wanalijua hilo,na wao kwa umoja wao maamuzi magumu wanajua vipi wanayapitisha,wanamwacha bashilu na polepole kupiga gitaa kumpigia mbuzi.
Nakuambia haludishi mtu kadi ya CCM ila badiliko la kuikataa CCM ni pale anapotumbukiza kura yake akijua ndani ya moyo wake mabadiliko ni lazima na mabadiliko hayo si ya hadharani ni siri bila ya kuharibu mlo wake,Wewe ulisikia wapi mtu kukamatwa kwa kuipigia CCM kura ya hapana ?Wapi ? Mwenyekiti wapi ulisikia?
Ulichokiona ni wale walioikataa CCM hadharani wakiandamwa hadi wanaamua kurudi eti nyumbani,mwaka huu wanaccm wanaikataa CCM kwenye sanduku la kura sio hadharani tena. Wala usiogope utajulikana hata ukijulikana CCM itakuwa umeshaiondoa sumu yake.