Yaani huwa nikiangalia pantoni au meli na boat ilivyo kwenye maji wakati inaelea nikivuta picha mule mvunguni najua kuna kitu kinafanya iende yaani engine au motor lakini mule chini nashindwa kujua hayo mapanga au propeler inafanyaje kazi kwenye maji bila engine kuzima.
Wakati engine ikiingia maji kama tunavyoambia anaungua na je kwa kuwa inatumia mafuta lazima itoe moshi sasa huo moshi hua unatokea wapi maana mle kwenye maji kuna viumbe hai. Je, huo moshi nao hauwadhuru?
Ngoja nitowe mfano wa Ferry ama Meli ya kubeba abiria.
Meli ya abiria ina metal plete kwa chini kabisa ambayo ndiyo inalalia maji, na baada ya hiyo metal plate juu yake kama urefu wa futi mbili+ huwekwa metal plate nyingine ambayo hujengwa kitu kama chumba kilicho ungana kutoka plate ya chini na yajuu upande wa mbele.
Hicho chumba huchomelewa mujarab kabisa na kisha kufanyinwa X-Ray ili kuhakikisha kwamba kimechomwa sawia na hewa haipenyi.
Hicho chumba ndicho hufanya kazi kama boya na kukifanya chombo kisizame majini.
Meli inatumia Engine kama machine zingine za aina yeyote, ingawa engine za meli huwa na Horsepower kubwa kuliko machine nyingi za ardhini.
Kawaida engine ya meli haikai ndani ya maji, bali fungwa ndani ya meli na haiguswi na maji kabisa. Hivyo basi Exhaust ya meli nyingi huwekwa juu kabisa ya meli ili kuepuka moshi usilete madhara kwa abiria ama mizigo iliyo bebwa na meli.
Sasa, technical mechanism inayo ifanya meli itembee ni:-
Engine huzungusha shaft ambazo zimeunganishwa kwa kutumia couplings ili ku protect vibrations from one to another component. Hivyo basi shaft imeunganishwa na Propeller ama mapanga boi ambazo zinakuwa ndani ya maji kwa upande wa nyuma kwenye mataki ya meli, na pangaboi hizo zinapo zunguka ndipo hufanya meli husogea.
Sasa.....
Kawaida ya meli nyingi pembeni ya panga boi huwekwa metal plate nene ambazo tunaziita flaps, hizi flaps ndizo husaidia kuongoza uelekeo wa chombo kwa maana ya kwamba unapo igeuzia upande flani basi flap huzuwia maji na kusababisha meli kupunguza mwendo upande flani. Na hapo ndipo ziwezi la kukata kona hufanyika.
Agggghhhhhh.....
Nimechoka kuandika mkuu, ngoja niwahi nikagonge kimoja kwanza...