Hivi vitu wanavyovalishwa Watoto Wachanga wa Kiafrika mikononi, viunoni na miguuni mbona navitafuta kwa wa Kizungu sivioni?

Hivi vitu wanavyovalishwa Watoto Wachanga wa Kiafrika mikononi, viunoni na miguuni mbona navitafuta kwa wa Kizungu sivioni?

Kama unaishi ushuani kama Masaki, Oysterbay au Upanga huna haja ya kumfunga vidude hivyo mtoto! Wachawi hawakanyagi maeneo kama yale 😂 ila kama upo uswahilini jiandae na zongo tu! Waafrika ni washirikina sana tena wanaweza kukulogea mtoto bila sababu ya msingi kabisa. Binafsi mie nimezaliwa Aga Khan na utoto ulinikutia Upanga kwetu wote hatujawahi kuvalishwa hayo mataka taka mpaka tumekuwa watu wazima ila huku uswahilini nilipo sasa kwa ushirikina uliopo siwezi shangaa mtu akimvalisha mwanae hivyo vitambaa.
Machawi yako hadi mabungeni kiongozi!. Ukitaka kujua, angalia misafara ya kuelekea B'gmoyo uchaguzi ukikaribia. Sema haya machawi ya huko hayaachi watoto uchi, na watoto wanakuwa magetini.
Tena siku hizi, kuna maboresho yamefanyika. Hao masangoma hawafuatwi badala yake wanachukuliwa na kuletwa site wakiwa wamevalishwa shuti na briefcases zilizojaa hayo madudu. Wakifika location wanapewa chumba, shughuli inaanza, wakimaliza wanavaa suti na kurudishwa kama walivyo bebwa.
Utajua tu kwamba hawa ni wale wale kwa namna suti mpya inavyokaa mwilini na utembeaji.
Ogopa mkuu!. Shetani si wa kumkadiria
 
Machawi yako hadi mabungeni kiongozi!. Ukitaka kujua, angalia misafara ya kuelekea B'gmoyo uchaguzi ukikaribia. Sema haya machawi ya huko hayaachi watoto uchi, na watoto wanakuwa magetini.
Tena siku hizi, kuna maboresho yamefanyika. Hao masangoma hawafuatwi badala yake wanachukuliwa na kuletwa site wakiwa wamevalishwa shuti na briefcases zilizojaa hayo madudu. Wakifika location wanapewa chumba, shughuli inaanza, wakimaliza wanavaa suti na kurudishwa kama walivyo bebwa.
Utajua tu kwamba hawa ni wale wale kwa namna suti mpya inavyokaa mwilini na utembeaji.
Ogopa mkuu!. Shetani si wa kumkadiria
Dah hatari sana mkuu ila Africa na ushirikina ni kama chupi na tako 😂😂😂
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
Kwani akivas vinamdhuru? Kama havimdhuru haina shida.Mbona wakubwa wanavaa macheni,vidani ,mabangili yanafaida gani?
 
Kaangalie shape za wadada wengi wa kizungu alafu urudi uku kwa waafrika, ukimaliza njoo toa ushuhuda[emoji3][emoji3]
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
Hao watoto wakipelekwa clinic kwa hospitali za dar manesi huwa wanavikatilia mbali ila manesi wa bush bado waoga kugeuka chura maji aka yanga
 
Wanaovalisha hayo madude mostly ni wa dini ile ya mtume
Ni nadra kukutana wa muingereza kamvalisha mtoto hayo madude

Mimi naona kinyaa nkiyaona hata mtoto najikuta namuogopa
Wanaovalishana hayo madude mostly ni wa vijijini town wanakuwa wamevamia tu, ilipotokea dini ya mtume kwenyewe mbona hawavai?
 
Binafsi naona hizo kamba wanazovalishwa watoto ni kama kinga kwao dhidi ya uchawi au ushirikina, pia kila mtu ametoka kwenye tamaduni na mila tofauti kwa iyo nawashangaa nyie mnao kuwa na mawazo tofauti yakusema kuwa eti nikikutana na mtoto kavalishwa ayo madude wala simbebi kwani uliombwa msaada wa kumbeba au? Kila mtu aamini anachoamini isipokuwa asivunje sheria ya nchi.
 
Kwani akivas vinamdhuru? Kama havimdhuru haina shida.Mbona wakubwa wanavaa macheni,vidani ,mabangili yanafaida gani?
Mkuu wengi naona wana mawazo negative bora wewe umeelewa watu wanatokea kwenye jamii tofauti sana ndio maana mtu ufanya vyovyote vile kwa kulinda uhai wake sasa nashangaa watu wanajifanya hawaelewi.
 
Wanaovalisha hayo madude mostly ni wa dini ile ya mtume
Ni nadra kukutana wa muingereza kamvalisha mtoto hayo madude

Mimi naona kinyaa nkiyaona hata mtoto najikuta namuogopa
Hahaha eti muingereza jamani watu mna code mnajuaaga kukaa kea password kweli wakija povu hutapata asee
 
Ni Karogwa na siyo Kalogwa Mkuu sawa?
Mhh, mkuu... mbona ni kuloga. Kiswahili sahihi ni kipi? Sikusoma kurogwa mbona.

Anyways, sijawahi kielewa hiko kidude. Kuna sista angu mmoja anajifanyaga mlokole kweli ila nilimkuta kakifunga kwa mwanae eti atangamaza akiwa sijui analialia ama akiona kitu kibaya. Na akanihakikishia hakina tatizo. Mimi nikamjibu honestly kuona ktk kitu cheusi kwangu ni kama hirizi tu. Akanambia si kweli kwamba eti ni mavi ya tembo sijui. Wooii.. uchaggani sionagi hivi vidude though. Sikitaki
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
...Mkuu Gentamycine, mbona ulikuwa unatenda jambo jema tu la kumuelimisha mama kuwa alichokuwa amekifanya kwa mtoto wake ni 'Uppuzi'...lakini hapo hapo alipokuchimbia mkwara wa kukuambia atakugeuza chura ukaogopa 'Upuuzi' wake na kuingia Mitini, Mkuu? Uliuamini 'Upuuzi' wake??? [emoji846][emoji846]
 
Back
Top Bottom