Hivi wanachofanya Panya Road hakiwahusu Taasisi za Haki za Binadamu? Wapo kimya kama kila kitu kiko poa

Hivi wanachofanya Panya Road hakiwahusu Taasisi za Haki za Binadamu? Wapo kimya kama kila kitu kiko poa

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Kwa sasa Dar es Salaam ni kama imeanza kutikisika, haijafikia kiwango hicho lakini kiuhalisia kuna mambo hayako sawa hasa yanayohusu ulinzi.

Hawa vijana wa Panya Road sijui niseme wanachekewa au mamlaka hazijapata jibu hasa la kudili nao, wenyewe mamlaka za ulinzi zinajua zinachokifanya.

Juzi hapa wametutangazia wamewakamata zaidi ya 100, kesho yake wanafanya tukio Kawe na kuua mtu, je kilichokuwa kinafanywa na mamlaka ni siasa au kweli waliwakamata.

Na wale wengine wanaokamatwa siku za nyuma wanazotutangazia ni kweli wanahukumiwa au ndio inakuwa zuga ili ionekane mambo yameenda?

Anyway, hoja yangu ya msingi pia leo ni kuhusu hizi taasisi zinazojiita zinatetea haki za binadamu, mbona sizioni zikipiga kelele wala kusema lolote!

Ajabu sana huu, hizo haki za binadamu wao wanaziona kwenye masuala ya Sheria pekee? Watu hasa wa ngazi za chini wanavyoteswa na Panya Road kwao siyo haki?

Najua hawawezi kuingia mitaani wao kupambana na Panya Road lakini kama wanaamini sauti zao huwa zinasaidia kwenye suala la malaka kuamka na kuzingatia haki za binadamu kuhusu jambo fulani, mbona sasa hivi hawaamki na kusema kitu?

Au Panya Road kuua, kupora na kujeruhi watu siyo haki za binadamu?
 
Suala la Panya Road ni mavi yanayopakwa kwenye sare ya jeshi la polisi ama vyombo vya usalama na wao wamekubali harufu ya kinyesi hicho iliendelee kunuka miilini mwao.

Hivi kwa ufahamu wa kawaida unaanza vipi kuamini kuwa Jeshi la polisi limeshindwa kuthibiti matukio ya hawa wanaoitwa Panya Road!

Tulipoamua kuichagua siasa kuongoza usalama wetu hapa ndipo tuliua kabisa mizizi ya furaha kwa raia wa Tanzania.

Hili suala sitalaumu jeshi la polisi bali vyombo vyote vya ulinzi, haiwezekani kikundi cha watu wenye visu na mapanga kinashamiri nchini na wanakichekea tu kama vile ni kikundi cha ngoma za jadi, leo hii hicho kikundi kikipata uwezo wa kuwa na silaha za moto maisha ya watanzania huko yatakuwaje?

Waziri mwenye dhamana umeamua kukubali hili! IGP umekubali kabisa kuwa jeshi lako ni dhaifu kwa hawa vijana! Kama mmekubali basi wekeni wazi kuliko kukaa wananchi wakakaa kutegemea jeshi la polisi ambalo halina meno kwenye matukio ya uhalifu.

Iko wapi furaha ya Mtanzania kwenye nchi yake? Kila sehemu anayogusa inamtoa machozi hata kwenye hili la usalama wake na mali zake nalo mmeshindwa?
 
Tunapenda sana kugombelezewa. Hatutaki shida. Haki zetu azipiganie fulani kwa niaba yeti. Si nadra kuchungulia madirishani jirani anapokuwa akilizwa na Panya road hawa hawa:

Dar: Panya road wavamia nyumba 24, wanne wajeruhiwa

Tatizo letu si ujinga?

IMG_20220914_180443_804.jpg
 
Suala la Panya Road ni mavi yanayopakwa kwenye sare ya jeshi la polisi ama vyombo vya usalama na wao wamekubali harufu ya kinyesi hicho iliendelee kunuka miilini mwao.

Hivi kwa ufahamu wa kawaida unaanza vipi kuamini kuwa Jeshi la polisi limeshindwa kuthibiti matukio ya hawa wanaoitwa Panya Road!

Tulipoamua kuichagua siasa kuongoza usalama wetu hapa ndipo tuliua kabisa mizizi ya furaha kwa raia wa Tanzania.

Hili suala sitalaumu jeshi la polisi bali vyombo vyote vya ulinzi, haiwezekani kikundi cha watu wenye visu na mapanga kinashamiri nchini na wanakichekea tu kama vile ni kikundi cha ngoma za jadi, leo hii hicho kikundi kikipata uwezo wa kuwa na silaha za moto maisha ya watanzania huko yatakuwaje?

Waziri mwenye dhamana umeamua kukubali hili! IGP umekubali kabisa kuwa jeshi lako ni dhaifu kwa hawa vijana! Kama mmekubali basi wekeni wazi kuliko kukaa wananchi wakakaa kutegemea jeshi la polisi ambalo halina meno kwenye matukio ya uhalifu.

Iko wapi furaha ya Mtanzania kwenye nchi yake? Kila sehemu anayogusa inamtoa machozi hata kwenye hili la usalama wake na mali zake nalo mmeshindwa?
Police wapo bize na kambi ya upinzani
 
kwa hio Polisi wameshindwa kabisa kudhibiti panya ?
 
Suala la Panya Road ni mavi yanayopakwa kwenye sare ya jeshi la polisi ama vyombo vya usalama na wao wamekubali harufu ya kinyesi hicho iliendelee kunuka miilini mwao.

Hivi kwa ufahamu wa kawaida unaanza vipi kuamini kuwa Jeshi la polisi limeshindwa kuthibiti matukio ya hawa wanaoitwa Panya Road!

Tulipoamua kuichagua siasa kuongoza usalama wetu hapa ndipo tuliua kabisa mizizi ya furaha kwa raia wa Tanzania.

Hili suala sitalaumu jeshi la polisi bali vyombo vyote vya ulinzi, haiwezekani kikundi cha watu wenye visu na mapanga kinashamiri nchini na wanakichekea tu kama vile ni kikundi cha ngoma za jadi, leo hii hicho kikundi kikipata uwezo wa kuwa na silaha za moto maisha ya watanzania huko yatakuwaje?

Waziri mwenye dhamana umeamua kukubali hili! IGP umekubali kabisa kuwa jeshi lako ni dhaifu kwa hawa vijana! Kama mmekubali basi wekeni wazi kuliko kukaa wananchi wakakaa kutegemea jeshi la polisi ambalo halina meno kwenye matukio ya uhalifu.

Iko wapi furaha ya Mtanzania kwenye nchi yake? Kila sehemu anayogusa inamtoa machozi hata kwenye hili la usalama wake na mali zake nalo mmeshindwa?
Binafsi shida naona inaanzia TISS, maana kuna mambo huku chini yanaendelea hata raia anaweza akawa anajua lakini dhamana ya usalama wa taifa hawajui,issue zinazoendelea kwenye sehemu za mikusanyikoa kama k'koo, Mbagala mwisho, Tandika, Stendi ya Magufuli na stendi ya mbezi mwisho kama ni kweli ni aibu kwa taifa kiujumla kama ni kweli, vibaka na wapiga debe wa maeneo nasikia wamepewa hesabu ya siku kuwakilisha sehemu, raia wa kawaida ukiibiwa maeneo hayo utazungushwa tu mchezo wote unajuliakna.
 
Watu wa haki za binadamu kwa Tanzania hujikita maeneo yale tu ambayo wafadhili wa nje wanawapa pesa. Usishangae wao kunyamzazia panya Road
 
Haki za binadamu utasikia pale Polisi watakapo ua panya road
 
Tusijikite tu kwenye Haki za Kisiasa
Nilikuwa naangalia, najiuliza utetezi wa Haki. Kwa muda mrefu tulikuwa tumejielekeza kwenye kutetea Haki, lakini hata nyie wanamitandao mmejielekeza zaidi kwenye Haki za kisiasa kuliko haki nyingine.

Nilikuwa nasema, kuna tatizo kubwa la ubakaji, si Zanzibar tu hata huku, vya kike na vya kiume. Lakini sauti hazijaja juu sana kama ambavyo mnasema kuhusu haki za kisiasa.

Kuna watu wanakatwa mapanga na Panya Road, sijui kama metetea haki zao zaidi ya kusema Polisi wafanye kazi yao. Lakini je, mmejipangaje kuongea na vijana, kuwaelewesha haki na wajibu wao kama vijana?

Lakini pia kuna watu wengi wanakufa kwenye ajali, je mnafanya nini? Nimewasikia Mtandao wa Usalama barabarani lakini sauti haijaja juu kama ilivyopaswa kuwa.
 
Back
Top Bottom