Mwenye ndoa ni mwanamume, mwanamke umeletwa ndani kumsaidia mume baadhi ya maeneo. Ni ukweli ambao wanawake wa siku hizi umeukiuka, mkijifanya much know. Mumeo akivutiwa na vya nje maana yake kuna mambo ndani hayajakaa sawa, imekupasa kujitazama na kurekebisha hapo, sio kuleta ushindani. Ndivyo ilivyokuwa tokea awali, pale wanawake walipotambua nafasi ya mwanamume kwenye ndoa.
Umewahi kusikia msemo mwanamke moumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe? Basi ni kwa ujuaji wa kijinga, kujifanya kupambana na mumeme ndani ya ndoa. Asikudanganye mtu, ndoa ya kweli haina haki sawa, anayetoa mahari ndio mwenye ndoa yake.