Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Ni suala la kupima tu, kwanini siku hizi ambapo haki sawa inapiganiwa sana, ndoa nyingi zinavurugika na watu wanaachana sana kuliko zamani ambapo wanawake hawakuwa na elimu, kumiliki mali na wanaume walikuwa wanaoa wake wengi lakini kuachika ilikuwa ni nadra sana.

Jibu ni moja tu, hakuna nyumba inayoweza kuendeshwa na viongozi wawili na ikafanikiwa, labda mmoja awe msaidizi.
Kiongozi lazima awe na majukumu mengi kuliko msaidizi na ayatimize kikamilifu sasa inapotokea kiongozi hatimizi majukumu yake anamwachia msaidizi huyo kiongozi ana sifa tena ya kuwa kiongozi?

Halafu unapotolea mifano ya babu zetu na bibi zetu usiangalie upande wa ndoa kudumu tu jiulize bibi zetu walikuwa wanafurahia hayo maisha? Yaani kwenu nyie wanaume ili mradi ndoa imedumu na nyie mnafurahia maisha basi haina shida hata kama wanawake huku wanaugulia maumivu? That's selfishness at it's best.
 
Mimi nimemaanisha kwamba wanawake wanaostahili kusaidiwa kazi za nyumbani na waume zao ni wale ambao wanatafuta pesa na pesa zao zinachangia katika maendeleo ya familia na haziishii kwenye matumizi yao binafsi tofauti na hapo basi mke hastahili kusaidiwa majukumu yake na mume wake
Tufafanulie mpenzi, maana mwanamke anaetoa elfu moja yake akanunua fungu la kitunguu huyo pia anachangia huduma.....
 
Edelyn kazi gani hizo za nyumbani mnazofanya siku hizi!? Asilimia 70 za nyumba zetu za mjini zina wadada wa kazi.. kama mwanamke anafanya kazi ni wajibu wake pia kuitunza familia, hapa hakuna ubishi.. na mara nyingi wanaume hutangulia kufariki kabla ya wake zao hasa huku africa sasa mama hapo utaendeshaje familia kama uliweka akilini kwamba hiyo ilikua kazi ya mwanamme!?
Kwanza, hiyo ya wanaume kufa mapema siyo sababu.

Pili, wanaume wangapi mnalalamika kuwa wake zenu wamewaachia kazi zote wadada wa kazi na hatimaye mnaamua kutembea na hao wadada wa kazi?
 
Hiyo hali imehatarisha sana ndoa za Watu hadi kufikia hatua Wanaume tunaogopa sana Ke wenye kazi zao, elimu 7bu hujawa na viburi na hata hawajali Waume zaidi ya kuangalia mahitaji yao wenyewe.

So kwanini walilie kufanya kazi ilihali hiyo kazi yenyewe hazina tija yoyote ktk ndoa zaidi ya kuwapumbaza kutwaa nzima kushinda kwenye mitandao, kujipodoa na kununulia viwalo vyao tu [emoji848]
Wanafanya hivyo kwa sababu ya mgawanyo wa majukumu kumbuka mwanamke ambaye anafanya kazi zote za nyumbani peke yake wakati mumewe yupo na hamsaidii, ni ngumu kwa huyo mwanamke kutumia pesa zake kwenye maendeleo ya kifamilia
 
Kwanza, hiyo ya wanaume kufa mapema siyo sababu.

Pili, wanaume wangapi mnalalamika kuwa wake zenu wamewaachia kazi zote wadada wa kazi na hatimaye mnaamua kutembea na hao wadada wa kazi?
Mwanaume kutembea na dada wa kazi ni utashi wake yeye mwenyewe tu kama atakavyoamua kuchepuka na mwanamke mwingine yeyote yule..

Nataka nijue hayo majukumu unayoyazungumzia ni yapi haswa.. itapendeza ukiyataja..
 
Mmmmmmhmn hapa sasa utakuwa unalenga kuachieve nini zaidi yaani?! Kama ni kuelemewa na kazi tafuta msaidizi mzee atalipia mshahara wake.

Ila sio tu kutaka kupima kama mwanaume ukiamua kumpelekesha atapelekesheka huku ni kumkosea adabu mumeo na utomvu wa nidhamu.

Mwanaume unatakiwa utazame kwa jicho la provider na protector na si vinginevyo. Atakusaidia pale inapobidi, labda ni mgonjwa, mjaumzito, umejifungua mtoto na dharula zingine ila sio kwa lengo la kupimana nae ubavu wakati akitokea nyoka hapo chumbani unarukia mgongoni kwake.... Wakija majambazi unataka yeye atoke akawavimbie, mimi kama unakuja na hizo itikadi nawalipa watu siku watuvamie halafu nione reaction yako, utakavyoweza pambana nao
...... Kama haujaingia uvungu wa kitanda....
Hahahaha hapana mkuu tunaposema mtusaidie siyo kwamba tunakuwa tunawaambia ila tunataka mjiongeze wenyewe yaani mchukulie hayo ni kama majukumu yenu na msione kama vile kuyafanya ni dharau

Halafu kuhusu kitafuta mfanyakazi kwani wanaume wangapi wanatembea na hao wafanyakazi kwa kisingizio cha kuwa wake zao wamejisahau na majukumu yote wamewaachia wafanyakazi?
 
Izo ni sifa za wanaume wa dar,

Huku mikoani wanaume tunalima mashamba, tunapasua mbao, tunafanya kazi ngumungumu ambazo mwanamke hawezigusa!

Ndomaana uku heshima bado ipo
Oohh basi hapo sawa
 
Ni suala la kupima tu, kwanini siku hizi ambapo haki sawa inapiganiwa sana, ndoa nyingi zinavurugika na watu wanaachana sana kuliko zamani ambapo wanawake hawakuwa na elimu, kumiliki mali na wanaume walikuwa wanaoa wake wengi lakini kuachika ilikuwa ni nadra sana.

Jibu ni moja tu, hakuna nyumba inayoweza kuendeshwa na viongozi wawili na ikafanikiwa, labda mmoja awe msaidizi.
Hahaaa..."Mafahali wawili......."
 
But at the same time you want us to take care of you especially in the financial matters. hapa ndo nliposhindwaga kuwaelewa ni 50/50 gani mnayoitaka!
Tunataka mtuhudumie kiuchumi kwa sababu ya huo huo mgawanyo wa majukumu
 
Hahahaha hapana mkuu tunaposema mtusaidie siyo kwamba tunakuwa tunawaambia ila tunataka mjiongeze wenyewe yaani mchukulie hayo ni kama majukumu yenu na msione kama vile kuyafanya ni dharau

Halafu kuhusu kitafuta mfanyakazi kwani wanaume wangapi wanatembea na hao wafanyakazi kwa kisingizio cha kuwa wake zao wamejisahau na majukumu yote wamewaachia wafanyakazi?
Thats a valid point.... Hao wanatembea na mabosi wanafanya hivyo kama sehemu ya income kwao....
 
Unajua mimi sidhani kama kuna wanaume waliokamilika wanatafuta wanawake kwaajiri ya kutafuta nao pesa. Bali wanaume waliokamili wanataka wanawake wenye uelewa na hali ya maisha aidha awe na kipato ama la.

Sio mwanamke unafika nyumbani tu hata haujashusha pumzi anakupokea na list ya bili za utility za nyumba, sijui hakuna mafuta, hakuna mchele, umeme unaisha, frji imeharibika, tunadaiwa pesa ya maji na takataka, mtoto anadaiwa ada,nahitaji pesa ya salooni, sijui vitu gani.

Na haya mambo yote anakwambia bila kujali unatafutaje pesa au kipato chako kipoje. Ila mwanamke mwenye busara atajitahidi kusoma nyakati na kujua mume wake kwa kipato kidogo alichonacho ni mambo gani ambayo anatakiwa kumsaidia kuyamudu. Anaweza hata kufanya biashara ndogo ndogo. Mwisho wa siku hata kipato cha mume wako kama utaongea nae vizuri anawezq hata kukupatia elfu hamsini ama laki kila mwezi uweke na kuhifadhi kwajiri ya dharula.....

Ni swala mtoto wa kike kufahamu obligation zako tu haitakusumbua hata kidogo kuwa mwanamke kwa mwanaume wako.
Sawa mkuu
 
Hao wachache ndiyo wanaokula mema ya wake sasa.

Kuna limama flani hivi Mumewe alikopa 8,00,000/= kalifungulia Mkewe mradi wa TIGO PESA, M-PESA & AIRTEL MONEY.

baada ya miezi 6 hv, Jamaa aliuguliwa Mama Mzazi(Mama Mkwe kwa Mke) akaenda kumwomba Mkewe 50,000/= ili amtibie Mgonjwa na ndipo ndoa ilipovunjikia hapo hapo baada ya Mkewe kumjibu Mume pumba eti "Hata nami wazazi wangu wana shida kibao lkn siwasaidii hivyo basi sina hela ya kukupa" ilihali pesa ipo kibandani.

Me alienda home kujipamba aliporudi kibandani alibomoa kibanda na kichapo juu kuchukua pesa, kesi ilisuluhishwa na Wazazi wote wa pande 2 lkn Jamaa alitwanga talaka papo hapo.

Ke ni Mama wa nyumbani na Me ni Mtafutaji kwa jinsi Mungu alivyotuumba kiuhalisia kabisa.
Sawa ila inapotokea mwanamke naye ni mtafutaji inakuwaje?
 
Kiongozi lazima awe na majukumu mengi kuliko msaidizi na ayatimize kikamilifu sasa inapotokea kiongozi hatimizi majukumu yake anamwachia msaidizi huyo kiongozi ana sifa tena ya kuwa kiongozi?

Halafu unapotolea mifano ya babu zetu na bibi zetu usiangalie upande wa ndoa kudumu tu jiulize bibi zetu walikuwa wanafurahia hayo maisha? Yaani kwenu nyie wanaume ili mradi ndoa imedumu na nyie mnafurahia maisha basi haina shida hata kama wanawake huku wanaugulia maumivu? That's selfishness at it's best.
Suala la mtu kuoa mtua aliyemzidi kipato au elimu na akaendeshwa huo ni uzembe wake na inabidi asubirie huruma au utashi wa mwanamke au atulie awe chini, ingawa kwangu mimi hata mwanamke awe na hela kivipi lazima nimdhibiti na lazima atulie.

Na kuhusu hilo la ndoa, ni kwamba ili ndoa idumu lazima kila mtu atimize majukumu yake, mke kujishusha kwa mume wake hata kama kosa ni la mume ( nafikiri hili lipo kwenye organization zote nchi; raisi , chuo; mkuu wa chuo, bunge; spika). Hivyo mwanamke akitimiza jukumu la kujishusha, ndipo mume atajieleza vizuri.
 
Ndio as long as anafanya majukumu yake ya nyumban na ananieshimu kama mume sio alete propaganda zake za usawa kisa na yeye ana earn


Halafu nilichogundua wanawake nyie ni selfish kwahyo mkuu Siku mume akikwama kwa sababu imezoeleka sisi ndo watoaji kama hana huwez msaidia?
Inategemea, kama na wewe mkeo siku akiumwa au akiwa na mimba kubwa huwa unamsaidia kufanya kazi za ndani basi na yeye siku ukiyumba kiuchumi atakusaidia tu ila tofauti na hapo usimlaumu na inaonyesha wewe hata mkeo akiumwa au akiwa na mimba kubwa hauwezi kumsaidia chochote bado utataka kazi zote afanye mwenyewe
 
Ndo maana kuna ma house girl halafu huwa nawashangaa wengi wenu tunawawekea wasaidiz wandani kabisa mnalalamika eti majukumuu
Inategemea, kama na wewe mkeo siku akiumwa au akiwa na mimba kubwa huwa unamsaidia kufanya kazi za ndani basi na yeye siku ukiyumba kiuchumi atakusaidia tu ila tofauti na hapo usimlaumu na inaonyesha wewe hata mkeo akiumwa au akiwa na mimba kubwa hauwezi kumsaidia chochote bado utataka kazi zote afanye mwenyewe
 
Utakapoingia maeneo ya kazi utajifunza kitu my dear. Wanawake wachache sana huwa kweli wamafikia hata 75% ya utendaji wa majukumu ya kazi bila msaada huko maofisini.

Pili, wanawake wanavyanzo vingi sana vya kupata pesa sababu wanadhamana ya miili yao katika utafutaji wa pesa. Ndo maaan hata hizi interviews siku hizi ni changamoto sana kwa mtoto wa kiume kupita.

Mwanamke anaweza pata msaada wa kifedha toka kwa baba, mama, kaka, dada, mjomba, bosi, marafiki, workmates na kadhalika ila trust me mwanaume nje ya kipato chake vyanzo vya kupata pesa ni vichache sana...... Na yeye hutoa zaidi.

Kwa kusema hivyo nataka kukujuza kuwa wanaume wanatafuta kwa jasho sana na kwasasa hali ni ngumu inazidi kuwabana wao zaidi kuliko wanawake.

Sasa huyu mtu ambaye anatakiwa kukaa chini kubuni vyanzo vipya vya mapato daily unataka tena akae na kuwaza vyombo havijaoshwa, sijafua nguo, usafi wa nyumba, sijakuna nazi, sijapika.

Aaaaaaah hebu kuwa serious kidogo..... Nadhani upo kinadharia zaidi.

Kimsingi wanaume wanaoa lengo kuu likiwa ni kupata usaidizi wa 100% wa majukumu ya kazi za ndani na mtu wa kumliwaza. Hiyo ya kutafuta pesa ni kiherehere chenu tu maana sidhani mwanaume anae jitambua atakaa kukushurutisha utafute kazi eti ulipie bili zote za nyumba ili hali yeye analala na kuamka na kukunja nne akitizama egoli kwenye tv. Hapo utakuwa umetunga uhalisia na si ukweli wa maisha halisi.....

So kama vipi naomba tuzungumze mambo practical katika jamii yetu na si maigizo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]wewe naona umeamua kunichekesha uko sahihi nimekuelewa ila nakuhakikishia mkuu kuna ndoa wanaume hawatimizi majukumu yao kabisa yote wamewaachia wake zao na hao hao wanaume nao wanataka heshima ndani kutoka kwa wake zao na jamii nzima mimi nina mifano ya ndoa hizo
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]wewe naona umeamua kunichekesha uko sahihi nimekuelewa ila nakuhakikishia mkuu kuna ndoa wanaume hawatimizi majukumu yao kabisa yote wamewaachia wake zao na hao hao wanaume nao wanataka heshima ndani kutoka kwa wake zao na jamii nzima mimi nina mifano ya ndoa hizo
Tatizo mnaexaggerate utadhani hizo ndoa hata 50 zinafika.... Tukitoa vijijini ambapo wanaume kwa asilimia kubwa ni walevi na hivyo ni unfit kudeal na familia.
 
Kuhusu maandiko mwanaume kaumbwa kutawala , mwanamke kma msaidizi t
Pia ukisem ufuate maandiko bas vitu vingi tumeenda kinyume na maandiko
Ndiyo mliambiwa mtutawale ila pia mliambiwa mtakula kwa jasho lenu sasa siku hizi kuna wanaume hawali kwa majasho yao wanakula kwa majasho ya wake zao halafu bado wanataka kuwatawala wake zao kwahiyo mnachagua maandiko ya kuyafuata (yanayowafaidisha) na maandiko ya kuyaacha (yanayowabana) si ndiyo?
 
Back
Top Bottom