Hivi wapo wanaofanikiwa kupata wenza makini (serious) mitandaoni?

Hivi wapo wanaofanikiwa kupata wenza makini (serious) mitandaoni?

Teknolojia imerahisisha Sana maisha, hivi karibuni kumetokea website na Apps mbalimbali za kupata marafiki wachumba na hata kuoana kabisa. Wengi wa walioko mtandaoni wapo kwa ajili ya maslahi, wengi wao ni matapeli, unaweza Kuta mwanaume kaweka picha ya Binti mzuri kweli kweli jilengeshe uone sasa, hata Kama ni wa kike unakuta Kuna vigezo vinavyokukwamisha kama unataka kumuoa mfano mwenye mtoto.

Kuna [emoji2765] site nyingi kv JF, Telegram, na nyinginezo play store. Waliofanikiwa na kutofanikiwa kupatana kupitia mtandao tupeni uzoefu humu.

Karibuni.
 
Kama unavyoona mtaani wengi ni wadangaji,watu safi wachache, basi huko mtandoni hali ni hiyo hiyo, wema wachache, wadangaji wengi.
 
wengi wa hao wachumba ni wajasiria-uchi,
Wanajitangaza wazi yaani ukiingia Instagram na Telegram ni mitandao ya ovyo kabisa unakuta mtu kaanzisha group la wauza malaya JF Pekee ndio mtandao safe
 
Kwa siku za karibuni kwenye mitandao mbali mbali kumeshamiri maombi ya kuhitaji Wenza...natamani kujua kama kuna utafiti umefanyika kujua mafanikio ya mfumo huu.

Maombi haya yamekuwa yakiambatishwa na vigezo lukuki huku vingi ya hivyo ni ngumu hata kupatikana kwa Mtu mmoja.

Pia kinachochanganya zaidi ni pale unapokuta eti hata binti wa mika 21, 22, mpaka 25 kukuta nae anatafuta Mchumba au Mwenza wa kuishi nae mtandaoni.

Sikatai kwamba wapo wanaofanikisha matakwa yao lakini pia wapo wengi wanaokwama kutokana na kutoka kabisa kwenye uhalisia na kubaki tu kama Wacheza kamari.

Kwa vyoyote ni ngumu kwa Mtu kumkubali Mtu kwa kusoma tu maelezo yake mtandaoni...sidhani kama yeye kwa kuandika tu anahitaji Mwenza Mcha Mungu basi Msomaji ajiridhishe kuwa Muombaji ni Mcha Mungu.

Nadhani kunahitajika namna nyingine zaidi ya kutafuta Wenza zaidi ya hii ya mitandaoni, yaani hata kama itaanzaia mtandaoni basi kwa kipindi maalumu Waombaji na Wahitaji wakae chini ya uangalizi wa Wajuzi wa mambo kabla hata ya kukutana.

Na baada ya hicho kipindi wote watakuwa na nafasi ya kupitia matokeo (results) ya aina ya Waombaji na Wahitaji wao...bila shaka kwa njia hii itakuwa ni rahisi zaidi kwa Mtu kuchagua Mtu mwenye kuendana nae badala ya Mtu kulazimika kwenda kwa asiyemju kabisa.
Ushauri mzuri na wenye busara, kutangaza hadharani hili suala inahitaji umakini wa hali juu. Na wale walio siriazi wanaweza wakachukulia tofauti na mhitaji.
 
Unaweza pata 😅😅😅

Nina watu wa4 nawajua wameolewa wanaishi safi tu na wote walikutana na wenza wao mtandaoni tena sio mtandaoni tuu ila ni kule kwenye dating sites
 
Back
Top Bottom