Hivi Wazee wetu wa kuanzia Miaka ya 70 hawa Mabinti wa 20's na 30's Mnaowaoa na Kuzaa nao huwa hampigiwi na hambambikiwi Watoto kweli?

@
GENTAMYCIME siku hizi dish limeyumba ai umekuwaje? Mzee wa miaka 70s anapeleka moto kama kawa! Mengi alizaa akiwa above 75! Kwanza wazee wanaooa dogodogo wana ukwasi wa kumuwekea ulinzi mke wake! Atachepukaje? GENTAMYCIME
 
Kapigiwa mzee Madiba, na maisha yanaendelea
 
Kijana,kuna muda ukifika mnatutenga baba zenu,hamtutembelei wala kutupigia simu.
Kazi yenu kubwa ni kuhakikisha mama zenu hawakaukiwi safari za kuja huko mnakoishi.

Sasa sisi baba zenu tunabaki wapweke kwa kukosa watu wakutuchangamsha km vile wajukuu (watoto wenu ambao wanatumia siku 365/1 kuwa masomoni.

Sasa tujaribu kusahihisha makosa tunaoa damu changa ili tupande begu upya huenda zikaota vizuri kuliko za mwanzo ambazo zimefifia (ninyi vijana wetu) lkn pia kupata nguvu kazi kwa ajili ya kuchotewa maji,kuchumiwa mboga kwani hata fedha japo kidoogo hamtumi mkisingizia ada za watoto.

Vijana wetu,mama zenu wakishakuwa na uhakika wa kuletewa matumizi kutoka kwenu watoto wetu hawataki hata tukumbushane stori zetu za kipindii kile tulivyokuwa tunawavizia njiani kuelekea visimani na kuchelewa kurudi nyumbani.

Sasa ukiongezea na ninyi kutusahau na kututupilia mbali sisi baba zenu basi tuaamua kuangukia kwa hivi vibinti ilimradi tu tuchangamshe afya ya akili wakati ninyi mkisubiri tufariki kwa unyong'onyevu na mawazo mfanye vikao vya kuchapisha picha zetu kwenye flana ili muwafurahishe wafanyakazi na wafanya biashara wenzenu kwamba mlikuwa mnatupenda.

Msituone pindi tukutanapo kwenye matukio yanayotukutanisha kuwa tumeinama muda mwingi7,huwa tunakumbuka mengi ya kipindi mkiwa wadogo huku tukijivunia uwepo wenu sasa matokeo yake ndiyo hayo yamekuwa kinyume na matarajio yetu.

Miezi 8 yooote mmeninyang'anya mke wangu bila hata taarifa,halafu tunapo oa mnachukia,mnakosea sana. Muwe mnawaleteeni mama zenu wadogo hawa hata vi 500 na flana za vyama vyenu angalau waendelee kuboresha afya za akili zetu huenda nanyi umri ukisogea tukingalipo akili zitawariudi.
 
Sidhani ni suala la umri bali afya ya mwili.Wapo wazee wenye miaka kuanzia 70 wapo fiti na wapo vijana wa miaka 30 tia maji tia maji.
Kuchapiwa kuna sababu nyingi zikiwepo za kiafya kama kisukari kwa kila umri,tamaa za pesa,na kutokuwa waaminifu kitabia.Soko la dawa za kuongeza nguvu za kiume lipo kwa rika zote ila vijana wa sasa wanaanza kupata matatizo hayo kwenye umri mdogo wa miaka 25 na kuendelea.
 
Hili jambo ni la Sayansi ya kibaiolojia hutakiwi kuandika kihisia.

Kwanza ungeweka umri wa mwisho mwanaume kuweza kutungisha mimba.

Jee mtu Wa miaka 70 hawezi kutungisha mimba??

Rest in Peace Mzee Reginald Mengi.
Baba yetu amefariki akiwa na umri wa miaka 80 alituachia mdogo wetu wa mwisho akiwa ananyonya na alikuwa copyright na Sisi ndugu zake kutoka mama wengine. Sasa usifikiri hizi changamoto ni kwa watu wote wazee wapo vizuri mno. Natamani niweke picha kama ushahidi lakini maadili yananizuia. Kuchapiwa hata vijana ndio mnachapiwa kuliko wazee. Aliyeamua kuolewa na mzee kaamua kuachana na tamaa ya ujana yupo na amekubaliana na mzee wake . Sasa Hao mnaowaita vijana mnakoma
 
Umeshawahi kunikuta najiliza Kwa moderator kwenye jukwaa la complain kama wewe zezeta?

Haya screenshot na hii huende ukalie Kwa Mods. Fanculo.
Huende ndiyo Kiswahili gani na cha wapi hiki? Nikikuambia Wewe ni Kubwa Jinga la JamiiForums nzima unakataa. Fanculo ni Watu Wawili Waliokuzaa na siyo Mimi.
 
@

GENTAMYCIME siku hizi dish limeyumba ai umekuwaje? Mzee wa miaka 70s anapeleka moto kama kawa! Mengi alizaa akiwa above 75! Kwanza wazee wanaooa dogodogo wana ukwasi wa kumuwekea ulinzi mke wake! Atachepukaje? GENTAMYCIME
Mimi siyo hilo Parody la GENTAMYCIME bali naitwa GENTAMYCINE sawa? Nachoka saaa kila Siku tu kutoa Ufafanuzi Kwenu kuhusu hilo Parody.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…