Hiyo Dar yenu inapigwa bao siku si nyingi

Hiyo Dar yenu inapigwa bao siku si nyingi

Dar ni jiji la kibiashara la Tz ...huwezi linganisha na hao wengine
 
Mikoani now kupo hot
Screenshot_20250221-071925.png
 
Wakuu ni hivi kutokana Hali ilivyo sasa naona kuna kila sababu ambayo itaitoa Dar kama namba moja katika swala Zima la uchumi. Sababu ni hizi.

1. Kuhamishwa Kwa ikulu na ofisi za Serikali. Hii imepunguza idadi kubwa ya watu ambao wangelazimika kusafiri na kuwepo mjini Dar. Hivyo imepunguza wananuzi wa mahitaji na huduma mji Dar es Salaam.

2. Ujenzi wa SGR ya Dar Hadi Dodoma hii itapelekea kuhamishwa kwa viwanda vingi kwani vikiwepo Dodoma kutakuwa na urahisi wa usafirishaji wa mizigo na magarifi kutoka mikoa mingine. Pia viwanda vingi vitapenda kuwa karibu na ofisi za Serikali.

3. Ujenzi wa miundo mbinu Bora Kwa mikoa mingine Kwa kipindi kifupi kilichopita tumeshuhudia ujenzi wa miundo yenye tija Kwa mikoa mingine Mfano mpango wa upanuzi wa bandari ya Mtwara na ya Mbambabay pia ujenzi wa reli ya Mbambabay Hadi Mtwara. Kwa hiyo baadhi ya mizigo itapungua bandari ya Dar pia baadhi ya viwanda vitajengwa huko Mtwara.

4. Ukuaji wa science na technology Kwa Sasa rasilimali nyingi ambazo zilikua hazivuniki lakini Kwa Sasa Kwa mashine za kisasa za bei nafuu. Zimefanya hata wazawa na wageni wakizitumia kuvuna rasilimali zilipo mkoani Mfano Iringa kumekuwepo na viwanda vingi vya playwood ambavyo Kwa Sasa vingi vinamatawi Njombe hivi vimeifanya Dar kupunyuliwa mkiani Kwa uchumi na Iringa na uwepo wa solar na bodaboda n.k umefanya watu waweze kulima hata sehemu za mbali.

5.Ukuwaji wa center nyingine za kibiashara kama vile Mwanza, Makambako na Dodoma kutapunguza umaarufu wa Dar.

Karibu Kwa mjadala
Dar Es Salaam litabaki kuwa kuwa Jiji kubwa katika nyanja zote Kwa miaka mingi ijayo katika nchi hii
 
Waziri wa viwanda na biashara Selemani Jafo ametembelea na kukagua viwanda viwili vya Magari na mafuta Mjini makambako na kuwahakikishia usalama wa mitaji yao ambayo itaongeza uchumi wa taifa.

Viwanda vilivyo tembelewa ni pamoja na Kiwanda cha Mafuta ya Parachichi cha AVO AFRICA ambacho tayari ujenzi wake umekamilika pamoja na kiwanda cha Utengenezaji wa Magari ambacho ujenzi wake umeanza rasmi na kinatarajia kutumia chuma cha Liganga na Mchuchuma kitakachoanza kuchimbwa wilayani Ludewa mapema mwaka huu.

Waziri Jafo amesema, kukamilika kwa viwanda hivyo viwili kutatoa fursa ya Ajira, Mapato kwa serikali pamoja na kupunguza ombwe la uagizaji wa bidhaa kutoka nnje ya nchi, yakiwemo mafuta.

Wakazi wa Mkoa wa Njombe na mikoa jirani wanasema, Uwekezaji uliofanyika unatoa fursa si tu ya kukuza sifa ya Mkoa bali uchumi, ajira na maendeleo ya Taifa katika sekta ya viwanda.

Ikumbukwe kwamba viwanda hivyo vyote viwili vinatarajia kutumia malighafi zinazopatikana mkoani Njombe yaani Chuma cha Liganga pamoja na Parachichi ili kuongeza mnyororo wa thamani katika malighafi hizo.

#StarTvUpdates
1740165846515.jpg
1740165854621.jpg
 
Makambako steel industrial park ni mwendelezo wa kuufanya mji mkubwa wa viwanda na biashara nyanda za juu kusini
1740365210798.jpg
1740365457135.jpg
1740365299200.jpg
1740365249668.jpg
1740365241477.jpg
 
Wakuu ni hivi kutokana Hali ilivyo sasa naona kuna kila sababu ambayo itaitoa Dar kama namba moja katika swala Zima la uchumi. Sababu ni hizi.

1. Kuhamishwa Kwa ikulu na ofisi za Serikali. Hii imepunguza idadi kubwa ya watu ambao wangelazimika kusafiri na kuwepo mjini Dar. Hivyo imepunguza wananuzi wa mahitaji na huduma mji Dar es Salaam.

2. Ujenzi wa SGR ya Dar Hadi Dodoma hii itapelekea kuhamishwa kwa viwanda vingi kwani vikiwepo Dodoma kutakuwa na urahisi wa usafirishaji wa mizigo na magarifi kutoka mikoa mingine. Pia viwanda vingi vitapenda kuwa karibu na ofisi za Serikali.

3. Ujenzi wa miundo mbinu Bora Kwa mikoa mingine Kwa kipindi kifupi kilichopita tumeshuhudia ujenzi wa miundo yenye tija Kwa mikoa mingine Mfano mpango wa upanuzi wa bandari ya Mtwara na ya Mbambabay pia ujenzi wa reli ya Mbambabay Hadi Mtwara. Kwa hiyo baadhi ya mizigo itapungua bandari ya Dar pia baadhi ya viwanda vitajengwa huko Mtwara.

4. Ukuaji wa science na technology Kwa Sasa rasilimali nyingi ambazo zilikua hazivuniki lakini Kwa Sasa Kwa mashine za kisasa za bei nafuu. Zimefanya hata wazawa na wageni wakizitumia kuvuna rasilimali zilipo mkoani Mfano Iringa kumekuwepo na viwanda vingi vya playwood ambavyo Kwa Sasa vingi vinamatawi Njombe hivi vimeifanya Dar kupunyuliwa mkiani Kwa uchumi na Iringa na uwepo wa solar na bodaboda n.k umefanya watu waweze kulima hata sehemu za mbali.

5.Ukuwaji wa center nyingine za kibiashara kama vile Mwanza, Makambako na Dodoma kutapunguza umaarufu wa Dar.

Karibu Kwa mjadala
JPM angekuwepo mpaka leo kule Dsm watu wangekuwa wameshapungua sanaaa.
 
Back
Top Bottom