Hizi hapa bifu zaidi ya 60 zilizowahi kutikisa hapa nchini zinazohusisha wanamuziki, watayarishaji wa muziki, media nk

Hizi hapa bifu zaidi ya 60 zilizowahi kutikisa hapa nchini zinazohusisha wanamuziki, watayarishaji wa muziki, media nk

Solo alimind kwa kuwa kwa namna Top 5 ilivyowekwa, ilikuwa lazima tu ashinde Afande Sele. Yaani top 5 iliwaacha Prof. J na Solo Thang nje, hapo ndio ikaonekana ushindi ni wa kupangwa mezani.

Shindano linahusu Vina halafu Solo Thang anatupwa nje!!
Namkubali sana Msafiri Kondo kusema kweli. Ila sikuona mbaya Afande kushinda
 
Namkubali sana Msafiri Kondo kusema kweli. Ila sikuona mbaya Afande kushinda
Afande hakuwa na uzito kulinganisha na marapa wote wa kipindi kile Japo kweli nyimbo yake ya Darubini ilikiwa kali ila shida ilianza walipowatoa baadhi ya wasanii na kutangaza Watu wao
 
Man-X alidai aliitaka beat, akamcheki Bwana Misosi, Misosi akampa beat kwa CD
wimbo ulivyotoka uka-hit sana kuliko ule wa Misosi, ndipo beef lilipoanzia, Misosi akakomaa chinichini mpaka redioni usipigwe
Prof J alisuluhisha
misosi nitoke vipi imelia kuliko hiyo ya man x nimechezea bahati.Nitoke vipi ni kali mno kuliko ya huyo mtoto wa keko.
 
Aliwapoteza Sana hata kwenye mtazamo solo aliangamiza Sana... Ile intro tu Hakuna S bila O, L bila O mwingine aitwae Thang bila Solo shupavu awajibike ka mwanaapolo....
Living Legend
Vidato sita nilivyopitia,
Ndivyo vinavyonisaidia,
Mbunifu ukizingatia,
Hata wakinibania,
Ni kipaji tu,
Ni mtazamo tu,
Msikasirike washikaji hayo ni mawazo tu.
 
Hahaha mzee hapo kuna scandel mbili Hapo [emoji28][emoji28] na una kumbukumbu sana umanifanya nimekumbuka mbali sana...Ngoja niziweke sawa hizo scandel ili uzielewe vizuri...Hiyo ilikuwa 2001 mpka 2002..

Ishu ilianzia Kwa Mtoto wa dandu (Cool James) kweli ila ilikoishia Ni Kwa Jaymo

Ishu ilikuwa Hivi kipindi cool james (Mtoto wa dandu) ndo ametoka sweeden na vihela hela kibao wakishua tena akaja akaanza kufanya mziki na nyimbo zake pale kwa Master J..

Nakumbuka kipindi hicho Mwanamke aliyekuwa moto kweli kweli ndo alikuwa Sinta, Sasa jamaa kuona hivyo akamwita sinta mwanza kwenye kufnya naye Shooting ya nyimbo yake inaitwa mapenzi kama sijakosea sana alitka awe kama video vixen,

unamkumbuka rafiki yake na Sinta kipindi hicho walikuwa wanaigiza naye alikuwa anaitwa Nina (Mdada fulan alikuwa ana macho fulan hivi) Ndo walienda naye sasa shida ikaja Nina alipobanwa sana na Nature aliporudi Bongo baada ya scandel kuzagaa mwenye magazeti ya udaku ya shigongo ikabidi aropoke tu Mzigo wake umeliwa na Dandu [emoji28][emoji28]

kipindi hicho wanashoot Nature alikuwa south na scandel ya JMo ilikuwa bado iko chini chini bado haijawaza hadharani sana..na haikuwa confirmed

na ndo maana kwenye ile nyimbo ya inaniuma sana
kuna kipande anasema

"Wengine ni Rafiki zangu nikiwataja huwezi kuamini"

ningekuwa na Muda ningekuandikia Hadi mistari yote Inavyochana watu humo nikakuchambulia vizuri..

Sasa nature ikamuumiza ndo akaingia Studio
katoka na Nyimbo Ya INANIUMA SANA..

sasa Hapa na pale wakarudiana ndo akatoa ile nyimbo kama unaifahamu ya Aah wapi (Sijui kama itawezekana,Mtu niliyempenda sana,Tukaja tukafarakana kwa sababu wanachonga sana)

sasa Kilichomuuma Sana mpaka akatoa nyimbo Mbili Double za Sitaki Demu na remix yake...
ni baada ya kuthibitisha kwamba Sinta anachukuliwa na Jaymo [emoji28][emoji28]

hapa ndo aliamua kuacha kabisa na hii ndo scandel na zingine zilizifuata ndo zilomfanya mpaka sinta akaondoka nchini maaana watu kadhaa walipiga Saini pale ..ahaah

ukisikia vizuri nyimbo ya Sitaki Demu verse ya kwanza jamaa anamalizia amasema " haya Sasa nimeghairi nenda kwa huyo Jaymo"
Nadhani aliposema "haya sasa nimeghairi nenda kwa huyo Jay Mo " alikuwa analazimisha vina tu
 
P Funk alimpa beat Jose chamillion bila ridhaa ya J wa Mitulinga
Hii haikua shida. Shida ni kuwa P Funk alilipwa na Chameleone pamoja na kampuni ya movie ambao walitumia wimbo wa Bomboclat na akazipiga hela zote bila kumtaarifu wala kumgawia Prof. Jay. Ilikua kitu kama $ 50,000 hivi mwaka 2016
 
Back
Top Bottom