Hizi hotuba za kisiasa za Rais Magufuli zitatuponza. Tuchague mambo ya kusema hadharani

Hizi hotuba za kisiasa za Rais Magufuli zitatuponza. Tuchague mambo ya kusema hadharani

Magufuli ni Raisi wa aina yake, siyo mtu wa kumumunya maneno kuogopa mabeberu watamfikiriaje. Kwa Africa hadi sasa sijaona Rais mwenye uthubutu Kama huo, maraisi wengi wa Africa ni wanafiki wanaojipendekeza kwa mabeberu wakiogopa kusitishiwa misaada...
Hapa unazungumzia watu wengi kukubaliana na msimamo wa Magufuli au usahihi wa msimamo wa Magufuli? Maana hata viongozi waliofanya mambo maovu kwa binadamu wengine pia waliungwa na watu wengi na historia imetunza kumbukumbu hizo. Mfano mrahisi kabisa, Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini aliungwa mkono na wengi katika kuwabagua weusi.

Kama msimamo wa Magufuli ni sahihi, taja ni watu wa nchi gani, au kiongozi yoyote wa Afrika aliyesimama na kuunga mkono msimamo wake ili kuibeba hoja yako. Kitu kipekee alichopatia kwenye huu ugonjwa, ni kutokutuweka watanzania lockdown, hayo mengine anaongea mambo ya aibu tu, hasa ukizingatia yeye ni msomi wa sayansi kama ni kweli.
 
Sijaona kosa lolote la Rais Magufuli. Yeye ametoa angalizo kuhusu chanjo ya korona, na amewataka wozara ya afya kutokurupuka kuchukua chanjo bila utafiti. Sasa kosa lipo wapi?...
Hakuna mwenye tatizo akiwa na msimamo wake, ila hilo liwe kwenye vikao vya ndani, na sio kwenye majukwaa ya kisiasa. Akiongea kwenye jukwaa la kisiasa anaongea kama rais wa nchi, hivyo kutafsirika kama msimamo wa nchi, wakati tuko wananchi wengi sana tusiokuwa na imani naye na baadhi ya misimamo yake. Kutokutuweka lockdown yuko sawa, hayo mambo mengine ni bora akae kimya.
 
Labda Jamaa walimfanya kitu wakati alipopita ujerumani,maana chuki zake kwa mzungu hazina tofauti na chuki za Hitra kwa wayahudi,sema tu hana uwezo ila wazungu wangekoma
Ndiyo hulka ya hao viumbe wote duniani! Hitler aliwachukia Wayahudina Wakomunist, Musolini naye aliwachukia Wakomunisti, Idd Amini aliwachukia Wahindi na Wazungu, Saddam Hussein aliwachukia Washia, nk.

Na mzee wangu wa kaya naye bila shaka anapitia mule mule! Anawachukia sana matajiri, watumishi wa umma na mabeberu!!
 
Ni bora tusitumie chanjo kabisa Kama hatuna uhakika wa ubora na usalama kwa hizo chanjo walizotengeneza kwa sababu miili yetu Ina uwezo wa kutengeneza kinga yake yenyewe (Natural immunity).

Kutengeneza chanjo ya virus siyo kitu kirahisi Kama unavyofikili. Virus Wana tabia ya kubadilika badilika (mutate) ndani ya muda mfupi Sana. Kwa hiyo haingii akilini katika muda wa miezi kadhaa tayari kuwe na vaccine ya Covid-19.
Polio na ssurua ni wadudu gani mkuu na mara ya mwisho walibadirika lini kwa kumbukumbu zako? Mnajazana ujinga tu
 
Tunaweza tukasikilizwa au hapana, ukweli ni kwamba rais anatakiwa kusaidiwa jinsi ya kuchagua maneno ktk majukwaa ya kisiasa. Tunaona jinsi Rais anavyotumia jukwaa na kujisahau kwamba maneno ya rais hutafsiriwa na ofisi zote nchini na kuvuka mipaka...
Leo jiwe kaongea utopolo sawa chanjo hataki kwani akikaa kimya shida iko wapi?
 
Tuache siasa za CHADEMA na CCM. Hata ujitoe kichwa huyo ndo rais. Rais yupo Boss! Upende usipende huyo ndo rais anayesaini kwa niaba ya nchi: Hata Uganda. Amin ndo alikuwa rais.
Ni kweli kabisa Kama Idd Amini na hata Mobutu Seseseko, Charles tylor, Omar Al bashiri, walikuwa Marais na walikuwa wanatukuzwa Sana na watu Kama wewe wakati wa utawala wao
 
Hakuna mwenye tatizo akiwa na msimamo wake, ila hilo liwe kwenye vikao vya ndani, na sio kwenye majukwaa ya kisiasa. Akiongea kwenye jukwaa la kisiasa anaongea kama rais wa nchi, hivyo kutafsirika kama msimamo wa nchi, wakati tuko wananchi wengi sana tusiokuwa na imani naye na baadhi ya misimamo yake. Kutokutuweka lockdown yuko sawa, hayo mambo mengine ni bora akae kimya.
Wewe naona hujielewi, kwenye majanga makubwa Kama haya kunahitajika Leadership, kiongozi wa nchi anatakiwa atoe kauli thabiti bila kupepesa macho ili wananchi tujue tunaendaje. Kauli ya Rais ni kauli ya nchi upende usipende. Kwa hiyo wewe vumilia tu.
 
Africa ndio ingekuwa baa la mwanzo kupatiwa chanjo lakiti kutokana na kelele zetu za ubishi kukataa kufanywa chambo, mabeberu wameamua wapeane wao kwanza Africa baadae wakimaliza ubishi. Tunasema wanataka kutumaliza, sasa watatuacha ka covid kitumalize mpaka tushike adabu zetu.
 
Aisee hapo kwenye swala la chanjo amefanya mistake.
Kuna kauli za kuongea mezani mkiwa dinner nyumbani na kuna kauli za kuongea ukiwa podium.

Zingine unaongea ukiwa chumbani na mkeo, na kuna zingine unaongea na moyo wako pekee[emoji1666]
 
Hapa unazungumzia watu wengi kukubaliana na msimamo wa Magufuli au usahihi wa msimamo wa Magufuli? Maana hata viongozi waliofanya mambo maovu kwa binadamu wengine pia waliungwa na watu wengi na historia imetunza kumbukumbu hizo. Mfano mrahisi kabisa, Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini aliungwa mkono na wengi katika kuwabagua weusi.

Kama msimamo wa Magufuli ni sahihi, taja ni watu wa nchi gani, au kiongozi yoyote wa Afrika aliyesimama na kuunga mkono msimamo wake ili kuibeba hoja yako. Kitu kipekee alichopatia kwenye huu ugonjwa, ni kutokutuweka watanzania lockdown, hayo mengine anaongea mambo ya aibu tu, hasa ukizingatia yeye ni msomi wa sayansi kama ni kweli.
Wewe mbona hujielewi? Nimetoa fact ya kwa Nini vaccine ya covid inatia mashaka lakini naona hiyo hujaiona.
Unauliza viongozi wa Afrika kuunga mkono kaulli ya Magufuli? Nani ana ubavu wa kuwachallenge mabeberu zaidi ya Magufuli, viongozi wengi wa Afrika ni wanafiki.

Mimi nimepitia comments za waafrika kwenye mitandao ya kijamii, wengi wameunga mkono kauli ya JPM.
 
Sijaona kosa lolote la Rais Magufuli. Yeye ametoa angalizo kuhusu chanjo ya korona, na amewataka wozara ya afya kutokurupuka kuchukua chanjo bila utafiti. Sasa kosa lipo wapi?

Kwenye dunia ya leo unatakiwa 'ku doubt' kila kitu... Hatuwezi kuchukua kila kitu eti sababu wazungu wa juu wamesema. Kwanza ni maoni yake na msiokubaliana na nyie toeni yenu, si ndio demokrasia?

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
Kuna tofauti kati ya kutoa angalizo na ku dismiss chanjo.

Magufuli ame dismiss chanjo, si ya Corona tu, chanjo zote.

Ujinga ni kwamba Tanzania haitengenezi hata toothpick.

Kama watu wanataka kuwaua huko, hata kwenye mitumba tu wanaweza.

Hawahitaji chanjo.
 
Wewe naona hujielewi, kwenye majanga makubwa Kama haya kunahitajika Leadership, kiongozi wa nchi anatakiwa atoe kauli thabiti bila kupepesa macho ili wananchi tujue tunaendaje. Kauli ya Rais ni kauli ya nchi upende usipende. Kwa hiyo wewe vumilia tu.

Sina tatizo na kauli ya rais kuwa ndio kauli ya nchi, ninachosema ni kuwa usahihi wa hiyo kauli ya rais ni wa kiwango gani. Usidhani kila mtu anashikiwa akili na rais kama ww. Alichopatia ni kutokuweka watu lockdown tu, lakini sio zaidi ya hapo.
 
Wewe mbona hujielewi? Nimetoa fact ya kwa Nini vaccine ya covid inatia mashaka lakini naona hiyo hujaiona.
Unauliza viongozi wa Afrika kuunga mkono kaulli ya Magufuli? Nani ana ubavu wa kuwachallenge mabeberu zaidi ya Magufuli, viongozi wengi wa Afrika ni wanafiki.

Mimi nimepitia comments za waafrika kwenye mitandao ya kijamii, wengi wameunga mkono kauli ya JPM.

Nimekuambia kuungwa mkono haimaanishi kuwa ni msimamo sahihi. Kwani hao wazungu wako kwenye mashindano na viongozi wa Afrika mpaka viongozi wa Afrika waonyeshe kuwachallenge? Cha msingi una challenge nini, sasa kama kiongozi anasema kuna raia wake wamekimbilia nje ya nchi kwenda kuchanjwa kisha wamerudi kuambukiza wananchi wengine, hiyo ni challenge au ni aibu kwa kauli kama hiyo kutolewa na kiongozi?
 
Sina utaalamu wowote kuhusu mambo ya afya, lakini tangu nikiwa mtoto wa Miaka 10, Mwanafunzi wa darasa la 4, nilifundishwa na Mwalimu wangu wa Sayansi Kimu kuwa Ugonjwa wa Malaria huambukizwa na Vimelea(Parasites) aina ya Plasmodium wanaoenezwa na Mbu jike aina ya Anopheles..

Miaka mingi baadaye Daktari wa Madaktari, one John Magufuli ameitangazia dunia na amenitangazia mimi huku akionesha kujiamini kwamba Malaria, kama ilivyo Korona, ni moja ya Magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya Virusi (aina gani, hajafafanua).

Sasa nimeachwa kichwa kinazizima 💤💤

Sasa Wataalam mko Wapi? Some factchecking please!
 
Back
Top Bottom