Hizi ndio Taasisi zenye mishahara minono Tanzania

Hizi ndio Taasisi zenye mishahara minono Tanzania

kuna taasis na wizara kibao watu wanapiga pesa na zingine zinatumia TGS hazivumi ila wana walioko huko maisha yao sio mchezo

Wizara ya ardhi ,Hazina, bodi ya nyama, bodi ya korosho, road fund, Tume ya pamoja ya fedha, TFRA,NFRA, DCEA, IMMIGRATION, TAWA ,NFRA ,WMA nk
Uhamiaji hii hii ambayo kuna jamaa angu katoka kuniomba nimuazime elfu 10 muda huu au unazungumzia uhamiaji ya nchi gani?
 
shida ya hizi posho na safari sio constant, anaweza akatokea boss kavurugwa anafuta zote au anawapa kidogo sana na hamna la kumfanya.....so kwa wadau ambao hamjapata kazi, mkipata kazi wekeni kwenye mindset yenu kwamba mshahara ndo haki yako, ivyo vingine lolote linaweza kutokea.
Absolutely

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Wewe amka.
Jwtz wanalipwa chenji tu sema mapolisi na askari Magereza kutwa kutwa kuwamezea mate jwtz.
Imagine kuna taasisi kima cha chini kabisa ni sh. 1.5m huyo hata diploma hana je, mshahara wa Eng. ?
JWTZ Private mwenye elimu ya form four anapokea 1.1M mshahara na marupurupu, Luteni mwenye elimu ya form six anapokea 2.3M mshahara na marupurupu, sasa kama hizo nazo ni chenji basi taasisi nyingi za serikali zinalipa chenji tu mkitaka mishahara na marupurupu nendeni private sector kwenye makampuni ya madini huko
 
JWTZ Private mwenye elimu ya form four anapokea 1.1M mshahara na marupurupu, Luteni mwenye elimu ya form six anapokea 2.3M mshahara na marupurupu, sasa kama hizo nazo ni chenji basi taasisi nyingi za serikali zinalipa chenji tu mkitaka mishahara na marupurupu nendeni private sector kwenye makampuni ya madini huko
Bado kuna kagape kakubwa. TPA mlinzi daraja la 3 yule entry level analipwa 1.3 na posho zake zikiwekwa pamoja ni zaidi ya mshahara.
TRA driver anakunja 1.5 huyo anayeanza kazi.
TPDC pesa anayolipwa Mhandisi daraja la pili unaweza kuwalipa maafisa wa ngazi ya chini wa TPDF 3.
 
JWTZ Private mwenye elimu ya form four anapokea 1.1M mshahara na marupurupu, Luteni mwenye elimu ya form six anapokea 2.3M mshahara na marupurupu, sasa kama hizo nazo ni chenji basi taasisi nyingi za serikali zinalipa chenji tu mkitaka mishahara na marupurupu nendeni private sector kwenye makampuni ya madini huko
Mkuu una uhakika na hizo salary za JWTZ? Mimi kuna jamaa yangu luteni alinikopa laki 1. Hivi ninavyoongea unaelekea mwezi wa tano story tupu.
Kama hiyo 2.3 ni mshahara wa luteni basi mimi kanizidi zaidi ya laki 9.
 
Mkuu una uhakika na hizo salary za JWTZ? Mimi kuna jamaa yangu luteni alinikopa laki 1. Hivi ninavyoongea unaelekea mwezi wa tano story tupu.
Kama hiyo 2.3 ni mshahara wa luteni basi mimi kanizidi zaidi ya laki 9.
Kakuzidi zaidi ya laki 9 bado anakudhuruma laki moja😁😁 nchi ngumu hii mkuu,ila yawezekana ikawa kweli labda jamaa ana mikopo hivyo kabaki na take home sisimizi
 
Bado kuna kagape kakubwa. TPA mlinzi daraja la 3 yule entry level analipwa 1.3 na posho zake zikiwekwa pamoja ni zaidi ya mshahara.
TRA driver anakunja 1.5 huyo anayeanza kazi.
TPDC pesa anayolipwa Mhandisi daraja la pili unaweza kuwalipa maafisa wa ngazi ya chini wa TPDF 3.
TPA mhandisi anakunja ngap?

TPDC Mhandisi anakuja ngapi?

Wote ni daraja la pili
 
Back
Top Bottom