Hizi radi leo kazini kwangu kuna kazi

Hizi radi leo kazini kwangu kuna kazi

Hahaa..🤣🤣 mmenikumbusha miaka ya nyuma kidogo kuna taasisi moja nilikua nimeajiriwa. Bosi wetu alikua mwanamke ni mkali kama pilipili! Kichekesho kilitokea siku imenyesha mvua na radi aisee yule mama ni muoga wa radi sijawahi kuonaa! Kitendo cha radi kupiga kufumba na kufumbua tulimkuta mama yupo chini ya meza, mikono kaziba masikio, macho kafumba na ukunga kama kuna msiba vile... Watu wote tuliokuwa ofisini (na wateja kibao) tulibaki kucheka kuanzia siku hiyo tukawa hatumuogopi tena 😀

Anyway, mimi binafsi huwa sipendi kelele za aina yoyote so mara nyingi mvua zikianza huwa navaa "earplugs" nalala zangu.
Screenshot_20250201-190457_Chrome.jpg
 
Hakuna kitu nakiogopa (nina hofu nacho) duniani kushinda radi.
Radi zinapopiga huwa nakosa amani kabisa.

Tena zikigonga zile kubwa zaidi wakati nipo homu huwa nafunga milango na madirisha naingia chumbani nachukuwa shuka zito najifunika.

Kivumbi huwa pale zinapo piga wakati nipo kazini, kazi yangu ni uvuvi vuta picha tunakwenda baharini mbaaali kutoka nchi kavu.
huko hakuna kibanda wala mti ni maji tu. na inasemwa radi hushuka katika vitu virefu, mule baharini vitu virefu huwa ni sisi wavuvi na chombo/boti zetu.
Dah inahofisha sana.
Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom