Hizi tozo kubwa kwenye uingizaji magari zinalenga nini hasa?

Hizi tozo kubwa kwenye uingizaji magari zinalenga nini hasa?

Kwa hiyo gari ikiwa mpya ndio inakuwa na kodi zaidi??.
Ndio maana huwa nasema katika Taasisi za Serikali ambazo ni hovyo ni hiyo TRA.
Hao jamaa wanafata MSRP ya gari husika kisha wanakuja na 90% ya charge kama kodi.

Kitu kinachofanya gari ya 2024 na ile ya 2022 kupishana kodi ni mfano gari la 2024 linauzwa $38,000 Japan unakuta la mwaka wa chini bei inapungua kidogo labda ni $34,000 wanakupigia 70%-90% ya hio hela unayotakiwa kulipa Japan ndo wanai term kama kodi.

Hii iko kinyume na tafsiri yao kana kwamba gari inavyozidi kuwa mpya ndio kodi inazidi kuwa ndogo. Its irrelevant na mfumo kabisa.
 
Kwa kifupi, serikali kupitia mamlaka yake ya TRA kitengo cha kodi za magari used wanazingua. Inabidi watengeneze formula upya.

Kwasababu, moja: theoretically, gari la zamani linatakiwa liwe na kodi kubwa kuliko gari jipya. Ila angalia CX5 hizi tatu, moja ya 2024, then 2023 na 2022. Ya 2024 ina ushuru mkubwa zaidi ya mil 10 kutoka 2022.

View attachment 3015297View attachment 3015298View attachment 3015300

Na pili, wajue haya magari sasa sio anasa ni chombo cha usafiri, na kinatusaidia katika mishe mbalimbali. Haina haja gari unalipia vitu kibao kuanzia kodi, unakuja kulipia kwenye mafuta kodi, bima nao wanakodi yao serikali, etc. Wangepunguza gharama za kuagiza.


Tatu, kuna magari wangeyawekea exemption mfano yenye cc chini ya 1000 au ya umeme au gesi etc. Ata kama sio 100% free basi kodi iwe ndooogo sana.
Hoja yako ya kwanza ningepanda kukuelewesha, hizo Gari zote tatu, hakuna hata moja iliyotozwa Kodi ya uchakavu, Gari ya 2024 imekupa Kodi kubwa sababu, bei yake ya kununua ni kubwa kuliko ya 2023 na 2022. Rate ya kuchaji iko flat Kwa zote so automatically chenye bei kubwa na Kodi yake ndivyo hivyo itakuwa kubwa kuliko chenye bei ndogo, mfano 1gari umenunua Shingi 1000, 2gari Shingi 600 na 3gari shingi 400 then zote ukachaji 20% so automatically 1gari itakuwa na Kodi kubwa.

Kuhusu hoja zingine Nami nakusapoti upo sawa kabisa kiufupi Kodi ya magari ingepigwa flat iwe 30% badala ya 75%
 
Serikali ingeanzisha viwanda v
Sababu
1. Kuongeza mapato ya serikali
2. Kupunguza msongamano wa magari
3. Kupunguza uchafuzi wa hewa kwa sababu magari mengi yametumika miaka hadi 20
4. Kuchochea utengenezaji wa magari hapa hapa nchni
5. Kupunguza matumizi ya mafuta
6. Kulinda viwanda vya ndani (local manufacturer eg Nyumbu)
ya kuzalisha magari ya kawaida na kuondokana na ujinga wa kujazana makodi.
 
Serikali ingeanzisha viwanda v

ya kuzalisha magari ya kawaida na kuondokana na ujinga wa kujazana makodi.
Pointi ya kwanza ndio muhimu zaidi, hizo zingine ni za kujibia swali
Hizi kodi zitaendelea kuongezeka kwa sababu ya deni la taifa
 
Ukimudu kununua gari maana akee una mahelaa ya kuchangiaaa serikali yako pendwaa iwezee kununua vieteeeee.
 
Sema Tanzania tu mkuu Zambia au Malawi kodi ya gari ni ndogo sana nililipia gari ya mteja Zambia kodi sawa na Tsh 6m gari ya 2018 GD 6 hilux double cabin wakati hiyo gari Tanzania kodi yake itaenda zaidi ya 30m...
Fortuner ya 2018 hapa kodi ni Tsh 33m..bei ya kununulia gari ingine..
boss hivi inawezekana nikanunua ndinga ili nikwepe kodi kubwa niipeleke Lusaka nikalipe kodi kidogo halafu isajiliwe huko number plate ya Zambia halafu nije nayo bongo mazima tupishane mitaani usajili wa zambia.

iwe kama natumia gari nililokodi nchi nyingine, hii imekaaje? au bado TRA watanibamba kodi kuendesha gari ya nchi nyingine kwa matumizi yangu hapa town?
 
boss hivi inawezekana nikanunua ndinga ili nikwepe kodi kubwa niipeleke Lusaka nikalipe kodi kidogo halafu isajiliwe huko number plate ya Zambia halafu nije nayo bongo mazima tupishane mitaani usajili wa zambia.

iwe kama natumia gari nililokodi nchi nyingine, hii imekaaje? au bado TRA watanibamba kodi kuendesha gari ya nchi nyingine kwa matumizi yangu hapa town?
Watakusumbua mkuu ingawaje wapo watu wanafanya hivyo maana kule kodi ni kidogo inalipwa kwa GVM sio mwaka wala aina ya gari Hilux ya 2020 kodi ni Z kwatcha 60,000 sawa na Tsh 6,000,000..
 
Hii hapo chini ni gari Mazda CX5 ya 2014 ambayo unamlipa mjapan milioni 14 unusu.

Kikokotoo cha kodi ya tra kwenye gari hilo ni milioni 10 unusu. Ukijumlisha unapata kama milioni 25 hivi. Hapo bado haujaweka gharama za bandarini.

HAPA UKIANGALIA NI KAMA SISI NA HAO WATENGENEZAJI NI KAMA TUNAGAWANA PASU KWA PASU.

Sasa unajiuliza kwanini kunawekwa tozo kubwa kama hizi kwa vitu ambavyo hata hatuvitengenezi sisi? lengo ni nini hasa?

Huku sio kujikolonisha wenyewe kweli? kulikuwa na sababu au ulazima gani kuwa na tozo kubwa ivi wakati hatutengenezi hizo gari hapa? au tunataka kufidia nini kwa tozo kubwa namna hii? maswali ni mengi wakuu.View attachment 3013556View attachment 3013557
Ni wivu tu mkuu, hawataki tuwe kama wao
 
Watakusumbua mkuu ingawaje wapo watu wanafanya hivyo maana kule kodi ni kidogo inalipwa kwa GVM sio mwaka wala aina ya gari Hilux ya 2020 kodi ni Z kwatcha 60,000 sawa na Tsh 6,000,000..
yaanii kamavipi naanzisha kikampuni uchwara kule cha kukodisha magari ila lengo langu sio hiyo biashara,

lengo langu ni gari ntalonunua nijikodishie, so vibali vyote paperwork mimi kukodi hilo gari ntakuwanavyo usumbufu upi ntakaopata?
 
Hii hapo chini ni gari Mazda CX5 ya 2014 ambayo unamlipa mjapan milioni 14 unusu.

Kikokotoo cha kodi ya tra kwenye gari hilo ni milioni 10 unusu. Ukijumlisha unapata kama milioni 25 hivi. Hapo bado haujaweka gharama za bandarini.

HAPA UKIANGALIA NI KAMA SISI NA HAO WATENGENEZAJI NI KAMA TUNAGAWANA PASU KWA PASU.

Sasa unajiuliza kwanini kunawekwa tozo kubwa kama hizi kwa vitu ambavyo hata hatuvitengenezi sisi? lengo ni nini hasa?

Huku sio kujikolonisha wenyewe kweli? kulikuwa na sababu au ulazima gani kuwa na tozo kubwa ivi wakati hatutengenezi hizo gari hapa? au tunataka kufidia nini kwa tozo kubwa namna hii? maswali ni mengi wakuu.View attachment 3013556View attachment 3013557
Bado vipuli, bado mafuta labda yangekuwa yanatumia maji sawa
 
Wala hamna mwenye roho mbaya na nyinyi. Tatizo ni nchi kuwa na vyanzo vichache vya mapato. Wangekuwa wabunifu na kukawa na vyanzo vingi magari yasingekuwa kimbilio lao. Walipa kodi Tz ni wachache sana ndio maana wanashikilia vitu vile vile miaka nenda rudi wanaongeza kodi tu.
Na bora sasa hiyo kodi yenyewe ingekuwa inatumika vizuri...zaidi zaidi inaishia mifukoni mwa mafisadi na matumizi mengi tu mabovu ya serikali.
 
Hakuna mafomula fomula kama hii calcutor ya zakayo?
Yani kuna ma formula ya kupunguza bei mengi tu.

Mimi nimeenda kununua BMW yangu ya pili, nilikuwa natoka kuenxesha X3 naenda kununua X5, nikakuta kuna formula ya kwamba ukirudia kununua BMW unapewa discount ya $500 na dealer.

Yani mara nyingine unapigwa punguzo la bei kwa formula ambayo hata hukuijua.

Kwa sababu wanajua competition ni kubwa sana.
 
Back
Top Bottom