Uchaguzi 2020 Hoja binafsi: Jaji Kaijage apongezwe kwa busara zake zilizombeba Tundu Lissu, busara zaidi itumike kuepuka sintofahamu za makusudi kwenye Uchaguzi

Uchaguzi 2020 Hoja binafsi: Jaji Kaijage apongezwe kwa busara zake zilizombeba Tundu Lissu, busara zaidi itumike kuepuka sintofahamu za makusudi kwenye Uchaguzi

Dam55

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2015
Posts
5,641
Reaction score
11,958
Jaji Kaijage na team yake ya Tume ya uchaguzi kama si busara zao za kukubali kufanya uhakiki wa wadhamini wa mgombea urais Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA Mhe. Tundu Lissu jambo ambalo kikanuni lilipaswa kufanyika kwenye ofisi za majimbo za Tume ya Uchaguzi basi ni dhahiri Lissu alitakiwa kutopitishwa na Tume.

Ajabu ni kwamba Mhe Tundu Lissu hakufanya hivyo iwezekana hakujua ama alijua Ila tu ni kiburi na kutaka kuonyesha umwamba mbele ya Tume ya Uchaguzi. Kikawaida hapa alitakiwa kukatwa moja kwa moja kwasababu tayari ameshavunja kanuni lakini busara za Tume zimembeba.

Mwanasheria makini msomi na mjuaji kama Tundu Lissu unawezaje kuvunja kanuni muhimu kama hii? Je hapo angakuta baadhi ya wadhamini ni hewa ingekuwaje ?

Hii inatoa picha kuwa kuna tatizo kubwa sana kwa hawa wagombea wa CHADEMA kwenye utaratibu wa ujazaji wa fomu za Ubunge na udiwani. Hawa wagombea wa ccm wanao pita bila kupigwa si kwamba ni mchezo mchafu wa CCM bali ni uzembe unao fanywa na wagombea wenyewe wa CHADEMA.

Kama imewezekana kwa Rais mtarajiwa kufanya kosa la kiufundi kama hili kwa wabunge je haitakuwaje?

Kama Lissu angekatwa na Tume asingekuwepo wa kulaumiwa makosa ni yake mwenyewe.
Kisha CHADEMA bila aibu wanakuja kusema hivi

Screenshot_20200826-011839.png

Kibaya zaidi mhe Tundu Lissu bila kujali busara zilizotumiwa na Tume bado ametoa lawama nyingi kuwa kwanini amekalishwa masaa mengi kwenye uhakika wakati mhe Rais Magufuli alitumia muda mchache Kama ilivyopangwa.
 
Jaji Kaijage Ni Jaji hasa alichokifanya Chadema hawaamini macho Yao kapangua mipango ya Chadema kisayansi kamati kuu
Chadema walikuwa ndumila kuwili walikuwa hawamtaki Lisu awe mgombea uraisi walimtaka Nyalandu na hawakutaka arudi

Kinafiki wakampitisha ili kukiondoa lawama apigiwe kura baraza kuu wakiamini Nyalandu kafanya kampeni ya kutosha atamshinda lakini baraza kuu likapiga kura za kinafiki pia kumpitisha wakijua kuwa Tume ya uchaguzi watamwengua tu ndio maana kukawepo kelele za kinafiki za akina Mbowe kutishia tume kuwa isimwengue Lisu wakitaka na sababu kumbe lengo lilikuwa kuiambia tume mwengueni huyo Lisu kwa sababu hizi!!! Chadema viongozi wa juu wakishaingia makubaliano ya Siri na ACT wazalendo kuwa Lisu akienguliwa wamuunge mkono Membe ambaye kwao ni mtu mwenye pesa ambaye angesaidia Chadema kifedha na kulipa chama influence Zanzibar sababu ya kuwa na Maaalim Seif

Tumaini la mwisho lililokuwa limesalia kwa Chadema kuhusu kukatwa jina lilibaki kwa NEC

Jaji Kaijage kapeleka kilio kwa CHADEMA kwa kuwapa my wasiyemtaka kakwepa zigo walilomtupia ili wajikoshe kuwa ni msajili ndio kamkakata sio wao Chadema

Kifupi Lisu wasiyemtaka huyo kaja kazi kwao
Nini kitakachoendelea Baada ya Lisu kuteuliwa ? Ni kuwa atapata supposed ndogo Sana ya kifedha na ki kampeni toka kwa Viongozi wa chadema kwa kisingizio kuwa na wao wako kwenye kampeni kwenye majimbo Yao hivyo apambane na hali yake yeye Kama yeye binafsi .Hivyo aniandae kwa kazi nzito ya kuji ratibia mwenyewe mikutano yake na hapo ndipo.penye kazi kubwa kunahitajika timu.kubwa mno ya watu wengi vifaa vingi na gharama kubwa Sio utani

Namuona Lisu Kama mgombea binafsi asiye na support ya chama ndani ya Chadema ambaye kila kitu atajitegemea mwenyewe kwenye kampeni sababu chama pia hakina hela na Viongozi wengine wanapigania majimbo.yao

Jaji Kaijage katibua mipango yote ya ACT wazalendo na Chadema kwa mpigo kwa kumpitisha Lisu
 
Weka basi na hizo kanuni ili wasomaji tujue kama Lisu kushinda na njaa jana ni makosa yake?
 
Nita mpongeza akifuta matokeo ya kipumbavu yaliyo wapa wabunge wa Ccm ushindi. Na pia anatakiwa akemee polisi kuwaingilia tume kwenye kazi zao. Mfano Tunduma, Morogoro, Mtama etc. Hayo mashauri polisi waliyo wakamata nayo watuhumiwa yange weza kusubiri. Ila uchaguzi hausubiri. Tuna taka haki..
 
Back
Top Bottom