Hoja dhidi ya Hoja: Maswali Sahihi Huleta Majibu Sahihi: Tatizo la Kudhania Kutoonekana kwa Magufuli

Hoja dhidi ya Hoja: Maswali Sahihi Huleta Majibu Sahihi: Tatizo la Kudhania Kutoonekana kwa Magufuli

Sioni tatizo kuuliza wapi Rais alipo, hakuna shida yoyote hapo, tatizo la serikali ni kukaa kimya muda mrefu hali hiyo ndio huzalisha maswali mengi zaidi kutokana na nadharia tofauti ambazo watu huzifikiria, kama wangesema mapema Rais anaumwa hizi kelele zisingekuwepo, kwasababu mtu kuumwa sio jambo la ajabu.
Hata wangesema anaumwa bado hao watu wangetaka kujua anaumwa nini na pia wakijibiwa anachoumwa tofauti na corona pia kelele zingekuwepo.
 
Cha kushangaza ni kwamba wanaoulizia Rais aliko ni walewale waliotuambia yuko nairobi hospital, ni walewale waliotuambia yuko kati ya sehemu mbili🙄 india au china 🤔🤔

Yohane johnthebaptist hawa watu tuwaiteje!?
I like your thinking.

Sina shaka wafaa kuwa mshauri elekezi.
 
Chadema imepoteana sana, nikiikumbuka ile chadema ya kina kitila, slaa na Zito kabwe awa wa sasa hivi wanaonekana kama vitoto vinavyojifunza bange.

Wameshatolewa kwenye Corona wapo kwenye kummiss Rais.
 
Mkuu, utajibiwa kuwa Waziri Mkuu alishalijibu swali la Rais alipo na jibu lake ni "Anachapa Kazi."

Sasa lililobaki ni kuvuta subira tu, pengine hadi mwisho wa Kwaresma, maanake wengine walisema jamaa kajifungia kwa sababu hiyo.

Baada ya hapo, kama bado atakuwa hajulikani alipo, basi huenda kila mtu ataruhusiwa kusema lolote aonalo linafaa kuhusu alipojificha rais.
Yesu alipata shida sana pale shetani alipompeleka pale mlimani na kuanza na mambo yake.

Kumbuka ilikuwa ni siku 40.

Lakini Yesu aliweza alishinda majaribu.
 
Chadema imepoteana sana, nikiikumbuka ile chadema ya kina kitila, slaa na Zito kabwe awa wa sasa hivi wanaonekana kama vitoto vinavyojifunza bange.

Wameshatolewa kwenye Corona wapo kwenye kummiss Rais.
That's another shot on target.

Nasikia WHO nao wahangaika kutafuta habari.
 
Cha kushangaza ni kwamba wanaoulizia Rais aliko ni walewale waliotuambia yuko nairobi hospital, ni walewale waliotuambia yuko kati ya sehemu mbili🙄 india au china 🤔🤔

Yohane johnthebaptist hawa watu tuwaiteje!?
Ungesikiliza star tv wananchi jumamosi,ungesikia wananchi walivyotoa maoni yao walipopewa fursa ya kupiga simu!
Watanzania wengi wanahoji Rais wao yuko wapi!Huo ndio ukweli,pita hata kwenye vijiwe vya kahawa utasikia haya!
 
MASWALI YASIYO SAHIHI HULETA MAJIBU YASIYOSAHIHI: TATIZO LA KUDHANIA

Na. M. M. Mwanakijiji

Katika hoja yangu ya wiki iliyopita nilijikuta nami nimechokosa udhanifu (assumptions) katika kujenga hoja hiyo na hivyo kuingia kwenye mtego wa maswali yasiyo sahihi. Mtu anapouliza kitu anafanya hivyo kwa sababu anataka kujua au kujulishwa jambo fulani. Hata hivyo, wakati mwingine watu wanauliza maswali ambayo yanaangukia makundi mbalimbali.

Maswali ya Jela: Maswali haya ni maarufu kuwa ni maswali ya jela kwa sababu yanauliza kitu ambacho kiko wazi. Yanaitwa ya “jela” kwa sababu ukiona mtu yuko jela kafungwa ni kwa sababu kafungwa. Sasa ukimuona mtu kaingia na magwanda ya wafungwa halafu unamuuliza “na wewe uko jela”? anaweza kujibu kuwa ameenda kutalii! Maswali ya “jela” ni maswali ya vitu vilivyo wazi. Unakutana na mtu halafu unamuambia “mbona huoenakani bwana”? ni kichekesho.

Lakini pia yapo maswali ya aina nyingine; maswali ya kuudhi. Maswali haya hayana lengo la kutaka kujua kitu bali yanataka katika jibu anayejibu akasirike. “We mbona mjinga sana!” hili si swali ni kero. Ni maswali yenye kuchokoza hasira.

Lakini pia yapo maswali ya aina nyingine; yenye lengo la kudadisi lakini yenye kutaka kuchokoza ufahamu wa kitu. Maswali ya mtu kutaka kujulishwa kitu. Hata hivyo, wakati mwingine maswali haya yanajikuta yanakosa majibu sahihi kwa sababu ndani ya swali lenyewe kuna jibu linalopendekezwa.

Mfano mzuri ni suala la “kutoonekana” kwa Rais Magufuli hadharani kwa wiki kadhaa sasa. Swali hili linaulizwa huku kukiwa na pendekezo – anaumwa. Kwamba, wanaotaka kujua aliko tayari wamedhania kuwa anaumwa na hivyo wanataka uthibitisho kuwa ‘haumwi’. Hapa ndipo na mimi nilipounga tela na kutaka serikali iseme kama Rais anaumwa basi waseme “anaumwa”. Ndani ya swali langu nami kulikuwa na kudhania; kuwa Rais anaumwa.

Ni kwa sababu hiyo jibu la Waziri Mkuu wiki iliyopita naamini lilijibu swali lisilo sahihi. Jibu lake lilisema kwa ujumla wake ni kuwa Rais yupo anaendelea na kazi zake ofisini na kuwa anaweza kuwasiliana na viongozi wenzake. Na kuwa si lazima Rais atoke toke nje kuonekana ili kuridhisha tu udadisi wa watu. Kwa maneno mengine, jibu la Waziri Mkuu ni kuwa linajibu swali lililokosewa la “Rais anaumwa ndio maana haonekani”? Lakini pia limejibu maswali ya kama aliondoka nchini kwenda Nairobi kutibiwa au kukimbizwa hadi India usiku wa manane (kama ilivyodaiwa miezi kadhaa nyuma kuwa alikimbizwa Afrika ya Kusini halafu Ujerumani)! Labda hili si swali sahihi.

Naamini swali lililotakiwa kuulizwa kwa usahihi wake ni “Kwanini Rais hajaonekana hadharani au hata kupiga simu radioni au kwenye TV kama ilivyo kawaida yake na badale yake tunaambiwa tu ameongea na watu”. Na kuwa kama Rais yuko ofisini kuna ugumu gani wa yeye kuonekana kwa TV (kukiwa na ushahidi wa muda wa sasa) kuwa rais yuko anaendelea na shughuli zake? Kwamba, kuna ugumu gani kwa yeye badala ya kutuma tu “salamu” angepiga simu kama ilivyokuwa kawaida yake. Si mara moja Rais amepiga simu kwenye mkutano wa hadhara au tamasha na kuzungumza na wapenzi na mashabiki wake. Kinachozuia yeye kufanya hivi ni nini?

Hapa ndipo tunaweza kuanza kupata majibu ya uhakika au yenye kutosheleza udadisi wa watu. Lakini pia maswali mengine ambayo hayajaulizwa na yanahusiana na hili ni:

Mbona hatujamuona Mama Janeth Magufuli kwa muda karibu na ule wa Rais? Naomba kupendekeza kuwa inawezekana kuwa swali hili ndilo kubwa zaidi kuliko lile la kutoonekana kwa Rais. Lakini pia, watu wangeuliza – baadaya baadhi ya watendaji wa karibu wa Rais akiwemo Katibu Mkuu kiongozi kufariki kwa kinachodaiwa ni COVID-19 serikali imechukua hatua gani kuhakikisha kuwa Rais Magufuli na kundi la wasaidizi wa karibu limepimwa na kuhakikisha kuwa hawamuexpose Rais kwenye kirusi hiki? Na japo tumesikia vifo vya baadhi ya watu wa karibu hasa wa ngazi za juu; je, kuna watendaji na watumishi wengine wa chini wa Ikulu ambao ama wameugua au wamefariki kwa changamoto ya kupumua inayoweza kuhusishwa na COVID-19?

Katika kujibu maswali haya ni vizuri kuangalia kwa uhakika bila kudhania; hata tunaposema “COVID-19” je tunajuaje ndio sababu ya vifo vya watu hao isipokuwa ni vifo vilivyotokea wakati kuna wimbi la maambukizi? Je, serikali inafanya utaratibu gani wa kupima watendaji wakuu wa serikali. Binafsi nikiangalia mikutano ya Waziri Mkuu na Makamu wa Rais najiuliza kama wao wenyewe wanaamini COVID haijagusa Ikulu na kama ni hivyo, basi ni vigumu kujua kama ugonjwa huu umegusa watu Ikulu. Nje ya hapo, yumkini kuna tatizo jingine kabisa – lisilohusiana na COVID-19 ambalo limegusa afya ya Rais.

Lakini, kama Waziri Mkuu amesema Rais ni mzima, imara na anaendelea na shughuli zake za ofisini; tunaweza vipi kupinga? Na hili linajibu swali la Zitto juzi kuwa nani anaongoza nchi. Kama Rais ni mzima wa afya na anaendelea na shughuli zake basi utawala wa nchi haujakaimishwa kwa yeyote isipokuwa Rais mwenyewe. Makamu wa Rais anafanya shughuli zake zote kama Makamu wa Rais na hajachukua jukumu lolote kwani Rais hajashindwa kutimiza majukumu yake kwa sababu zilizoanishwa kikatiba. Kinachoitwa “ulinzi” wa Makamu wa Rais mbona hakuna kipya, ulinzi wa Mama Samia Suluhu Hassan umekuwa hivyo wakati wote isipokuwa mara nyingi watu hawafuatilii sana. Lakini pia kama Rais yuko Ikulu, Makamu anapotoka anaweza kuongezewa ulinzi. Nina uhakika kama kuna tatizo lolote la ombwe la uongozi Katiba yetu wala haina shida.

Kwa sasa tujaribu kuuliza maswali sahihi; ili tupate majibu sahihi. Vinginevyo sote tutakuwa tunaangukia huu mtego wa kudhania na matokeo yake kupewa majibu yenye kuridhisha tu udhanifu wetu. Maswali sahihi, huleta majibu sahihi. Hata kama ni majibu tusiyoyapenda au yasiyoridhisha.


Mkuu, PM alijibu alimwaga ugali, na mama Samia akaongezea nyama ya mbuzi pale Tanga, akasema "kuna wakti inabidi kukaguliwa" .

Sasa mwapewa dondoo mwataka nini zaidi?

Hivyo, tuvute subira tuvuke kwaresima.

Tusubiri Pasaka.
 
Tatizo la kukosea kuuliza maswali linatokana na kwamba watu hawakuwa wakishughulishwa na ukimya wa rais hadi pale ulipokuja uzushi wa kwamba Rais ni mgonjwa na yupo Kenya kwa matibabu,kwahiyo kinachoendelea sasa hivi ni watu kutaka kujiridhisha kuwa ni kweli anaumwa na ndio maana wengine wanaitaja hadi corona katika hili jambo.
 
Wapo ambao leo wakisikia sauti yake redioni, "hai" isiyo ya rekodiwa, watasema ni Baraka Magufuli. Dawa yao ni kigae cha msauzi tu. Usingizi mnono, hata inyeshe ya mawe!
Lazima unaishi kijijini.
 
Ulichoandika sijaona hoja hapa

Zaidi zaidi naona kama unataka kujikosoa nakuona ulikosea kwenye ile thread yako ya "ya rais kama anaumwa tuambiwe"

Umeingiwa na woga.

Swali linabakia lile lile "Rais yuko wapi"?

Kama ni mzima ajitokeze hadharani, kama anaumwa tuambiwe.
Hii comment ingefaa ipandishwe iwe ya kwanza kabisa...
 
Kapotea mbwa tu dau limetangazwa,ijekuwa rais
 
Ungesikiliza star tv wananchi jumamosi,ungesikia wananchi walivyotoa maoni yao walipopewa fursa ya kupiga simu!
Watanzania wengi wanahoji Rais wao yuko wapi!Huo ndio ukweli,pita hata kwenye vijiwe vya kahawa utasikia haya!

Uzushi wenu ndio unazua taharuki kwa wananchi ambao rais Magufuli ni kipenzi chao
Tangu PM na VP waongee mioyo yao imetulia
 
MASWALI YASIYO SAHIHI HULETA MAJIBU YASIYOSAHIHI: TATIZO LA KUDHANIA

Na. M. M. Mwanakijiji

Katika hoja yangu ya wiki iliyopita nilijikuta nami nimechokosa udhanifu (assumptions) katika kujenga hoja hiyo na hivyo kuingia kwenye mtego wa maswali yasiyo sahihi. Mtu anapouliza kitu anafanya hivyo kwa sababu anataka kujua au kujulishwa jambo fulani. Hata hivyo, wakati mwingine watu wanauliza maswali ambayo yanaangukia makundi mbalimbali.

Maswali ya Jela: Maswali haya ni maarufu kuwa ni maswali ya jela kwa sababu yanauliza kitu ambacho kiko wazi. Yanaitwa ya “jela” kwa sababu ukiona mtu yuko jela kafungwa ni kwa sababu kafungwa. Sasa ukimuona mtu kaingia na magwanda ya wafungwa halafu unamuuliza “na wewe uko jela”? anaweza kujibu kuwa ameenda kutalii! Maswali ya “jela” ni maswali ya vitu vilivyo wazi. Unakutana na mtu halafu unamuambia “mbona huoenakani bwana”? ni kichekesho.

Lakini pia yapo maswali ya aina nyingine; maswali ya kuudhi. Maswali haya hayana lengo la kutaka kujua kitu bali yanataka katika jibu anayejibu akasirike. “We mbona mjinga sana!” hili si swali ni kero. Ni maswali yenye kuchokoza hasira.

Lakini pia yapo maswali ya aina nyingine; yenye lengo la kudadisi lakini yenye kutaka kuchokoza ufahamu wa kitu. Maswali ya mtu kutaka kujulishwa kitu. Hata hivyo, wakati mwingine maswali haya yanajikuta yanakosa majibu sahihi kwa sababu ndani ya swali lenyewe kuna jibu linalopendekezwa.

Mfano mzuri ni suala la “kutoonekana” kwa Rais Magufuli hadharani kwa wiki kadhaa sasa. Swali hili linaulizwa huku kukiwa na pendekezo – anaumwa. Kwamba, wanaotaka kujua aliko tayari wamedhania kuwa anaumwa na hivyo wanataka uthibitisho kuwa ‘haumwi’. Hapa ndipo na mimi nilipounga tela na kutaka serikali iseme kama Rais anaumwa basi waseme “anaumwa”. Ndani ya swali langu nami kulikuwa na kudhania; kuwa Rais anaumwa.

Ni kwa sababu hiyo jibu la Waziri Mkuu wiki iliyopita naamini lilijibu swali lisilo sahihi. Jibu lake lilisema kwa ujumla wake ni kuwa Rais yupo anaendelea na kazi zake ofisini na kuwa anaweza kuwasiliana na viongozi wenzake. Na kuwa si lazima Rais atoke toke nje kuonekana ili kuridhisha tu udadisi wa watu. Kwa maneno mengine, jibu la Waziri Mkuu ni kuwa linajibu swali lililokosewa la “Rais anaumwa ndio maana haonekani”? Lakini pia limejibu maswali ya kama aliondoka nchini kwenda Nairobi kutibiwa au kukimbizwa hadi India usiku wa manane (kama ilivyodaiwa miezi kadhaa nyuma kuwa alikimbizwa Afrika ya Kusini halafu Ujerumani)! Labda hili si swali sahihi.

Naamini swali lililotakiwa kuulizwa kwa usahihi wake ni “Kwanini Rais hajaonekana hadharani au hata kupiga simu radioni au kwenye TV kama ilivyo kawaida yake na badale yake tunaambiwa tu ameongea na watu”. Na kuwa kama Rais yuko ofisini kuna ugumu gani wa yeye kuonekana kwa TV (kukiwa na ushahidi wa muda wa sasa) kuwa rais yuko anaendelea na shughuli zake? Kwamba, kuna ugumu gani kwa yeye badala ya kutuma tu “salamu” angepiga simu kama ilivyokuwa kawaida yake. Si mara moja Rais amepiga simu kwenye mkutano wa hadhara au tamasha na kuzungumza na wapenzi na mashabiki wake. Kinachozuia yeye kufanya hivi ni nini?

Hapa ndipo tunaweza kuanza kupata majibu ya uhakika au yenye kutosheleza udadisi wa watu. Lakini pia maswali mengine ambayo hayajaulizwa na yanahusiana na hili ni:

Mbona hatujamuona Mama Janeth Magufuli kwa muda karibu na ule wa Rais? Naomba kupendekeza kuwa inawezekana kuwa swali hili ndilo kubwa zaidi kuliko lile la kutoonekana kwa Rais. Lakini pia, watu wangeuliza – baadaya baadhi ya watendaji wa karibu wa Rais akiwemo Katibu Mkuu kiongozi kufariki kwa kinachodaiwa ni COVID-19 serikali imechukua hatua gani kuhakikisha kuwa Rais Magufuli na kundi la wasaidizi wa karibu limepimwa na kuhakikisha kuwa hawamuexpose Rais kwenye kirusi hiki? Na japo tumesikia vifo vya baadhi ya watu wa karibu hasa wa ngazi za juu; je, kuna watendaji na watumishi wengine wa chini wa Ikulu ambao ama wameugua au wamefariki kwa changamoto ya kupumua inayoweza kuhusishwa na COVID-19?

Katika kujibu maswali haya ni vizuri kuangalia kwa uhakika bila kudhania; hata tunaposema “COVID-19” je tunajuaje ndio sababu ya vifo vya watu hao isipokuwa ni vifo vilivyotokea wakati kuna wimbi la maambukizi? Je, serikali inafanya utaratibu gani wa kupima watendaji wakuu wa serikali. Binafsi nikiangalia mikutano ya Waziri Mkuu na Makamu wa Rais najiuliza kama wao wenyewe wanaamini COVID haijagusa Ikulu na kama ni hivyo, basi ni vigumu kujua kama ugonjwa huu umegusa watu Ikulu. Nje ya hapo, yumkini kuna tatizo jingine kabisa – lisilohusiana na COVID-19 ambalo limegusa afya ya Rais.

Lakini, kama Waziri Mkuu amesema Rais ni mzima, imara na anaendelea na shughuli zake za ofisini; tunaweza vipi kupinga? Na hili linajibu swali la Zitto juzi kuwa nani anaongoza nchi. Kama Rais ni mzima wa afya na anaendelea na shughuli zake basi utawala wa nchi haujakaimishwa kwa yeyote isipokuwa Rais mwenyewe. Makamu wa Rais anafanya shughuli zake zote kama Makamu wa Rais na hajachukua jukumu lolote kwani Rais hajashindwa kutimiza majukumu yake kwa sababu zilizoanishwa kikatiba. Kinachoitwa “ulinzi” wa Makamu wa Rais mbona hakuna kipya, ulinzi wa Mama Samia Suluhu Hassan umekuwa hivyo wakati wote isipokuwa mara nyingi watu hawafuatilii sana. Lakini pia kama Rais yuko Ikulu, Makamu anapotoka anaweza kuongezewa ulinzi. Nina uhakika kama kuna tatizo lolote la ombwe la uongozi Katiba yetu wala haina shida.

Kwa sasa tujaribu kuuliza maswali sahihi; ili tupate majibu sahihi. Vinginevyo sote tutakuwa tunaangukia huu mtego wa kudhania na matokeo yake kupewa majibu yenye kuridhisha tu udhanifu wetu. Maswali sahihi, huleta majibu sahihi. Hata kama ni majibu tusiyoyapenda au yasiyoridhisha.
Naona unajaribu kama kukubaliana na upuuzi uliosemwa na na PM na VP na kujilaumu kwa ile thread yako ya kuulizia alipo.meko..

Anyway jambo lililowazi na najua hauwezi kukiri hapa, ni kwamba sasa umeona madhara ya kuongozwa na kichaa kwa jinsi alivyoligharimu Taifa..

Pole.
 
Mimi naomba nikujibu swali lako la tatu,nyie mnadhania kwamba Raisi anaumwa,labda nikweli ni mgonjwa...Kama MNA uhakika anaumwa Basi Raisi hayupo na nchi inajiendesha yenyewe...Na sisi wanachi hatuoni shaka mana hakijakwama kitu!!!
Wala hata mimi sijazania kuwa Rais wetu anaumwa.
Naomba usirudie tena kunilisha maneno, nina mke na watoto na pisi moja matata sana wote wananitegemea mimi.
 
MASWALI
1. Rais yuko wapi?
2. Huko alipo afya yake ikoje?
3. Kwasasa nani ndiyo anaendesha nchi?
Answers;
1. Rais yupo Ikulu ya Tanzania kama alivyosema Mh. Makamu wa Raisi na Waziri Mkuu
2. Kwasababu anachapaka kazi zake ofisini/ikulu basi ni mzima wa afya hii na kwa mujibu wa Mh. Makamu wa Rais na waziri Mkuu
3. Kama rais yuko ikulu anafanya kazi kama kawaida yake, ni mzima wa afya; kama tulivyojuzwa na viongozi wetu, yeye Mh. Rais ndiye anayeendesha nchi ndiyo maana hakuna jambo lolote la nchi ambalo tumejulishwa limekwama

Unayo maswali mengine?🤔
 
Nawaza tu wale walinzi wa rais yule mwanjeshi na yule mlinzi wake mweuzi lzm watakuwa nattarifa za jpm iwe isiwe wao wanajuw kinachoendelea .. nao pia tuwaombee jmn kutoka na mgonjwa gafla Mara Kenya Mara India bila hata kujiandaa vxr ni kaz saan watakuwa wanapiga mihayo tu ktk chemba za ospitali za apoolo
 
Back
Top Bottom