Uchaguzi 2020 Hoja fikirishi: CHADEMA kwanini mnadai Uhuru wa Vyombo vya Habari huku mkivinyima haki, kufukuza na kuvidhalilisha!?


Ndio TBC hawana haki hio.
 
Kaka ule ndio weledi wao.

..hebu fikiria kama ungekuwa unaangalia mechi ya mpira halafu kituo cha TV wanafanya michezo ile.

..aliyetoa maelezo kwamba studio wawe wanakatiza-katiza ndio hana akili hata kidogo.

..I hope watakuwa wamejifunza.
 
bora hata wamefukuzwa maana walikuwa wanataka kulisha propaganda za ccm kwa wafuwasi wa chadema, huku wakijifanya wanaonyesha mkutano wa chadema.
 
..hebu fikiria kama ungekuwa unaangalia mechi ya mpira halafu kituo cha TV wanafanya michezo ile.

..aliyetoa maelezo kwamba studio wawe wanakatiza-katiza ndio hana akili hata kidogo.

..I hope watakuwa wamejifunza.
Sasa swali la msingi je hicho ndio kinawanyima haki ya kutangaza?
 


Chadema hatupendi unafiki. Nashangaa aliwapa 15min...mie ningetoa dk3!
 
Unaonesha mpira live, mchezaji anakaribia kufunga goli wewe unakata matangazo unaanza kuchambua chenga aliyopiga mchezaji. Baada ya goli unarudisha matangazo na hutoonesha jinsi goli lilivoingia. Huku ndo kurusha mpira kwa uhuru? Na je unaweza kuendelea kuangalia huo mpira kupitia hiyo Tv? Tuheshimiane na tusionane majuha. Watuache tujichambulie wenyewe. Tuna utashi wa kujua chema na kibaya.
 
..waruhusiwe kurekodi mikutano ijayo ya CDM.

..lakini kile walichokuwa wakifanya kilikuwa KERO na MAUDHI kwa watazamaji.

..kiliwachafua TBC kuliko hata CDM.
Mbona hujibu swali mkuu? Tunachokizungumza hapa ni uhalali wa wao kufukuzwa na haki yao Kama chombo cha habari. Je walichofanyiwa TBC si uvunjivu wa Uhuru wa vyombo vya habari.?

Kama ingekuwa ni kero kwa watazamaji ni jukumu la hao watazamaji kuhama kituo na si Chadema kuwafukuza kwasababu tunaweza sema ule ndio weledi wao wa habari na weledi wao hauwanyimi haki ya wao kurusha matangazo kwasababu bado Kuna watanzania wenye haki ya kupata habari wanaopenda kutazama tbc hivyo hivyo hata kama weledi wao ni mdogo.
 
Ni bora wamefukuzwa kwa sababu wameonyesha upendeleo wa dhahiri kabisa. Wengine huwa wanaongea mambo ya hovyo kabisa na kuwadhalilisha watu barabarani hawakuzimiwa wala kutoa sauti yalisikika yote bila kujali.
 
Mkuu acha kutetea upumbavu. Hata kama wewe ni ccm tumia hata akili kidogo ili uone aibu unachokitetea. TBC walikuwa wanakera mno. Ningekuwa nina uwezo ningefukuza wafanyakazi wote.
 

..sifahamu kama KISHERIA cdm walikuwa na haki ya kuwafukuza tbc au la.

..sifahamu ktk suala hili, haki za cdm, na haki za tbc, zinaanzia wapi na kuishia wapi.

..ningefurahi kama tbc wangeenda MAHAKAMANI ili kilichotokea kipate majibu ya KISHERIA.
 
Wewe jamaa mahaba yako kwa ccm yanakufanya kuwa taahira. Mbona bwana yule huwa hadi anatukana kabisa, kuita wateule wake wapumbavu lakini huwa hawazimi sauti wala kufanya walichofanya leo? Acha kutetea ujinga.
 
I was home watching.... Bora wamefukuzwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…