Hoja ya Nape Kuhusu Uchunguzi wa Akaunti ya Deni la Taifa

Hoja ya Nape Kuhusu Uchunguzi wa Akaunti ya Deni la Taifa

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Hoja ya Mhe. Nape (MB) Bungeni kuhusu kukaguliwa akaunti ya deni la taifa sina shida na hoja na anazo haki zote kwa mujibu wa Katiba, sheria na kanuni za Bunge, isipokuwa nachelea kuamini kwamba uzito wa hoja hii unaweza kutambuka wigo wa mhimili wa Bunge na kuleta shida kwenye mhimili wa serikali (japo Bunge linaisimamia serikali). Shida iko hivi:-

1. Uelewa wangu unanishawishi kwamba hoja inaweza kuwa kizungumkuti kwa VP.

2. Anayeshikilia nafasi ya VP kwa sasa ndiye alikuwa jikoni wakati wa awamu ya 5 hivyo kwenye awamu ya 6 yeye ni Institutional Memory wa yaliyotokea kwenye awamu ya 5 kwa awamu ya 6.

3. Je, kwenye uchunguzi huo wa akaunti hiyo ya deni la taifa kwa awamu ya 5 siyo kwamba utamuhitaji VP akae pembeni kupisha uchunguzi huru huo? Je, Tz tunao utamaduni huo?

4. Chama cha mtoa hoja kinawezakuwa salama kweli kama ukaguzi huo ukifanyika na kuthibitika kwamba utaratibu haukufuatwa. Ikumbukwe kwa chama cha mtoa hoja mchakato wa uchaguzi mkuu unaofuata huwa unaanza pale serikali inapomaliza kuundwa; ya uchaguzi mkuu unaokuwa umemalizika, kwa maana ya kwamba hata muda huu hoja inapotolewa tayari chama kiko kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu unaofuata.

5. Kama uchunguzi wa Bunge ukigundua madudu kwenye akaunti ya deni la taifa kwa wakati wa awamu ya 5 je, siyo kwamba hoja ya mtoa hoja inawaweka pabaya Ma-CAG wa awamu za 5 na 6?

6. Je, kama awamu ya 6 ikimaliza muda wake, nani anajuwa kama awamu ya 7 nayo itakuja na watoa hoja wa aina hii kwenye hoja hii ya akaunti ya deni la taifa? Taifa litakuwa linajenga utamaduni gani wa kutafutana mchawi kila awamu?

7. Je, mahusiano mazuri yaliyoko baina ya wakuu wa mihimili ya Bunge na Serikali yanawekwa rehani endapo taarifa ya ukaguzi/uchunguzi itathibitisha mashaka ya mtoa hoja?

NB.
Juzi nilisoma gazeti moja kwamba deni la taifa limefika Tzs.64 tr hoja ya mtoa hoja ilitaja Tzs.9 tr kama ndiko deni la taifa lilifika. Sasa kwa hesabu ndogo tu zisizo za kitaalam, kama awamu ya 5 ilifikisha deni la taifa Tzs.9 tr ina maana kwa mujibu wa gazeti hilo na hoja ya mtoa hoja kuna ongezeko la Tzs.55 tr za awamu ya 6 ambayo pia mtoa hoja ni kiongozi wa awamu hii kwa nafasi yake ya Ubunge kama alivyokuwa pia kwa awamu ya 5 anayotaka ichunguzwe. Aidha, kati ya Tzs.9 tr za awamu ya 5 na Tzs. 55 tr za awamu ya 6 (kufanya jumla ya Tzs.64 tr awamu gani imekopa zaidi? Japokuwa hoja ya mtoa hoja imejikita katika kutilia mashaka juu ya uwazi na matumizi ya awamu ya 5 kwenye akaunti hiyo ya deni la taifa na siyo nani kakopa zaidi).

Lakini pia hoja hiyo ya mtoa hoja inatambuka zaidi na kuwateta wataalam wa mipango kwasababu kama awamu ya 6 imekopa basi ni kwa ajili ya kumalizia miradi mikubwa ya maendeleo ya awamu ya 5 maana miradi mipya ya awamu ya 6 haijawa mingi kiasi cha kukopa Tzs.55 tr ndani ya miezi 7 wakati awamu ya 5 ilifikisha deni la taifa kwenye Tzs.9 tr kwa miaka mi-5. Sasa hapa wataalam wa mipango ndiyo wamekosea au kiongozi wa mhimili wa serikali ambayo mtoa hoja ndiyo alikuwa kinara wa kuiweka madarakani?

Nadhani tupime kina kabla hatujavua nguo kuvuka mto.
 
Mbona unamuongelea makamu wa rais wa sasa kwa nafasi yake ya wakati huo kama waziri wa fedha tu.
Na umekwepa kuongelea popote kuhusu aliyekuwa bosi wake makamu wa rais wa wakati ambaye sasa ni rais wa JMT?

Je, unadhani kuna wizi kweli ulitokea au unawasikiliza hao wasaka tonge kina Nape ambao wanatafuta upenyo wa mamlaka kuwaona.

Je, bunge nalo liombe taarifa ya kamati ya uhakiki wa mali za CCM iliyosimamiwa na Bashiru isomwe hadharani tuone kama kuna wasafi kati ya hao wapiga kelele?

Nape ana madudu kibao na sio msafi linapokuja suala la mali za CCM hasa chanel ten na ule mtambo wa uchapishaji.
 
Nape anafikiri anamchafua Jiwe alifanya miradi mikubwa zaidi kuliko waliomtangulia,anasahau
Kuwa rais wa Sasa ndiyo alikuwa msaidizi wake.
Teuzi zinawatesa Sana vijana wa Kikwete,mpeni wizara tu Kama January mlivyompa hata Kama Hana uwezo.
 
Hoja ya Mhe. Nape (MB) Bungeni kuhusu kukaguliwa akaunti ya deni la taifa sina shida na hoja na anazo haki zote kwa mujibu wa Katiba, sheria na kanuni za Bunge, isipokuwa nachelea kuamini kwamba uzito wa hoja hii unaweza kutambuka wigo wa mhimili wa Bunge na kuleta shida kwenye mhimili wa serikali (japo Bunge linaisimamia serikali). Shida iko hivi:-

1. Uelewa wangu unanishawishi kwamba hoja inaweza kuwa kizungumkuti kwa VP.

2. Anayeshikilia nafasi ya VP kwa sasa ndiye alikuwa jikoni wakati wa awamu ya 5 hivyo kwenye awamu ya 6 yeye ni Institutional Memory wa yaliyotokea kwenye awamu ya 5 kwa awamu ya 6.

3. Je, kwenye uchunguzi huo wa akaunti hiyo ya deni la taifa kwa awamu ya 5 siyo kwamba utamuhitaji VP akae pembeni kupisha uchunguzi huru huo? Je, Tz tunao utamaduni huo?

4. Chama cha mtoa hoja kinawezakuwa salama kweli kama ukaguzi huo ukifanyika na kuthibitika kwamba utaratibu haukufuatwa. Ikumbukwe kwa chama cha mtoa hoja mchakato wa uchaguzi mkuu unaofuata huwa unaanza pale serikali inapomaliza kuundwa; ya uchaguzi mkuu unaokuwa umemalizika, kwa maana ya kwamba hata muda huu hoja inapotolewa tayari chama kiko kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu unaofuata.

5. Kama uchunguzi wa Bunge ukigundua madudu kwenye akaunti ya deni la taifa kwa wakati wa awamu ya 5 je, siyo kwamba hoja ya mtoa hoja inawaweka pabaya Ma-CAG wa awamu za 5 na 6?

6. Je, kama awamu ya 6 ikimaliza muda wake, nani anajuwa kama awamu ya 7 nayo itakuja na watoa hoja wa aina hii kwenye hoja hii ya akaunti ya deni la taifa? Taifa litakuwa linajenga utamaduni gani wa kutafutana mchawi kila awamu?

7. Je, mahusiano mazuri yaliyoko baina ya wakuu wa mihimili ya Bunge na Serikali yanawekwa rehani endapo taarifa ya ukaguzi/uchunguzi itathibitisha mashaka ya mtoa hoja?

NB.
Wiki iliyopita nilisoma gazeti moja kwamba deni la taifa limefika Tzs.64 tr hoja ya mtoa hoja ilitaja Tzs.9 tr kama ndicho kiasi kilichokopwa na awamu ya 5. Sasa kama awamu ya 5 ilikopa Tzs.9 tr je, awamu ya 6 imekopa kiasi gani katika hiz Tzs.64 tr? Mtoa hoja ni kiongozi wa awamu hii kwa nafasi yake ya Ubunge kama alivyokuwa pia kwa awamu ya 5 anayotaka ichunguzwe. Aidha, kati ya Tzs.9 tr za awamu ya 5 na hizo za awamu ya 6 (ambazo mtoa hoja hakuzitaja) (kuleta jumla ya deni la taifa la Tzs.64 tr awamu gani imekopa zaidi? Japokuwa hoja ya mtoa hoja imejikita katika kutilia mashaka juu ya uwazi na matumizi ya awamu ya 5 kwenye akaunti hiyo ya deni la taifa na siyo nani kakopa kiasi gani).

Lakini pia hoja hiyo ya mtoa hoja inatambuka zaidi na kuwateta wataalam wa mipango kwasababu kama awamu ya 6 imekopa basi ni kwa ajili ya kumalizia miradi mikubwa ya maendeleo ya awamu ya 5 maana miradi mipya ya awamu ya 6 haijawa mingi kiasi cha kulifikisha deni la taifa Tzs.64 Sasa hapa wataalam wa mipango ndiyo wamekosea au kiongozi wa mhimili wa serikali ambayo mtoa hoja ndiyo alikuwa kinara wa kuiweka madarakani?

Nadhani tupime kina kabla hatujavua nguo kuvuka mto.
 
Tilioni 55 za za awamu ya 6 ndani ya miezi saba ya uwepo wake. Heko awamu ya tano, kwa kutumia tilioni 9 katika miaka 5, na kilichofanyika, kikaonekana kwenye macho ya kila mtanzania.
 
Kwa maoni yako;

1.Fedha iliwe tu kwa sababu ikichunguzwa Mpango atalazimika kukaa pembeni kupisha uchunguzi.

2.Fedha iliwe tu maana ikichunguzwa itawatia matatizoni maCAG waliopita. Unamwongelea CAG yupi? Kama umelenga Assad anzisheni tu yuko tayari hata kesho kutoa ushahidi kuhusu ununuzi wa ndege, SGR, Nyerere Dam, Ununuzi wa Wabunge na Madiwani.

3.Fedha iliwe tu maana ikichunguzwa CCM itavuliwa nguo.

4.Fedha iliwe tu maana waliohusika wana mamlaka na wakichunguzwa itajenga utamaduni wa kufukua makaburi.

Hizi akili CCM huwa mnatoa wapi? Mbona wengine ni Wasomi wakubwa tu nchini lakini mnajenga hoja Kama darasa la 4B?
 
Kwahiyo unapuuza hoja ya Nape kwa kumhurumia Philipo?
 
Nape anafikiri anamchafua Jiwe alifanya miradi mikubwa zaidi kuliko waliomtangulia,anasahau
Kuwa rais wa Sasa ndiyo alikuwa msaidizi wake.
Teuzi zinawatesa Sana vijana wa Kikwete,mpeni wizara tu Kama January mlivyompa hata Kama Hana uwezo.
Achana na Nape personally jadili hoja yake iliyoko mezani. Wewe unajua mikopo ya awamu ya nne na ya tano imefanyia miradi gani?? SSH ametangazia umma wa watanzania jinsi mkopo wa 1.3 Trilioni zilivyotumika nchi nzima, tena mpaka mgao wa wenzetu akina yakheee kule Zenji.

Hawa wengine pesa wanakopa kwa siri na matumizi pia ni siri yao, imagine hata wabunge hawajui matumizi ya mikopo.

Halafu hili jambo litungiwe sheria kabisa kwamba mikopo yoooteee Kabla ya kuchukuliwa maombi yapelekwe bungeni ili ijulikane inachukuliwa kwa ajili gani, kutoka wapi na riba ya kiasi gani.
 
Tilioni 55 za za awamu ya 6 ndani ya miezi saba ya uwepo wake. Heko awamu ya tano, kwa kutumia tilioni 9 katika miaka 5, nakilichofanyaka, kakonekana kwa macho ya kila mtanzania.
Hujaelewa mkuuu, unafanya mchezo na Trilioni 55?
 
Mbona unamuongelea makamu wa rais wa sasa kwa nafasi yake ya wakati huo kama waziri wa fedha tu.
Na umekwepa kuongelea popote kuhusu aliyekuwa bosi wake makamu wa rais wa wakati ambaye sasa ni rais wa JMT?

Je, unadhani kuna wizi kweli ulitokea au unawasikiliza hao wasaka tonge kina Nape ambao wanatafuta upenyo wa mamlaka kuwaona.

Je, bunge nalo liombe taarifa ya kamati ya uhakiki wa mali za CCM iliyosimamiwa na Bashiru isomwe hadharani tuone kama kuna wasafi kati ya hao wapiga kelele?

Nape ana madudu kibao na sio msafi linapokuja suala la mali za CCM hasa chanel ten na ule mtambo wa uchapishaji.
Sasa hapa ndio umefanya utetezi au umeongeza idadi ya majizi hadharani?
 
Achana na Nape personally jadili hoja yake iliyoko mezani. Wewe unajua mikopo ya awamu ya nne na ya tano imefanyia miradi gani?? SSH ametangazia umma wa watanzania jinsi mkopo wa 1.3 Trilioni zilivyotumika nchi nzima, tena mpaka mgao wa wenzetu akina yakheee kule Zenji.

Hawa wengine pesa wanakopa kwa siri na matumizi pia ni siri yao, imagine hata wabunge hawajui matumizi ya mikopo.

Halafu hili jambo litungiwe sheria kabisa kwamba mikopo yoooteee Kabla ya kuchukuliwa maombi yapelekwe bungeni ili ijulikane inachukuliwa kwa ajili gani, kutoka wapi na riba ya kiasi gani.
Hangaya aliyotangaza pesa ya sherehe za muungano zigawanywe nusu kwa nusu Kati ya watu 60m.na 1m.Bunge liliidhinisha lini?
 
Je, unadhani kuna wizi kweli ulitokea au unawasikiliza hao wasaka tonge kina Nape ambao wanatafuta upenyo wa mamlaka kuwaona
Uchunguzi huwa sio kupima wizi ila hata mambo ya performance audit na accountability tu. Mfano kuna kuchelewesha malipo hadi interest rate zinacompound tu deni linakua na malimbikizo makubwa ama kukopa kwenye sources zenye interest rate kubwa ilihali kulikua na cheaper option etc.

Sasa mwizi anaweza asiwepo yaani hakuna hela iliyoibwa ila kuna hasara kwa serikali so itasaidia kuweka sera zenye ufanisi na kufanya hta Mama Samia/mawaziri wa fedha kuwa makini maana anajua akitoka naye watamkagua!! And so on....

Hata sheria za madini zilibadilishwa baada ya uchunguzi kwanini mnataka iwe siri siri hivi eti kisa tu Nape aliyehoji ni mchafu??
 
Hoja ya Mhe. Nape (MB) Bungeni kuhusu kukaguliwa akaunti ya deni la taifa sina shida na hoja na anazo haki zote kwa mujibu wa Katiba, sheria na kanuni za Bunge, isipokuwa nachelea kuamini kwamba uzito wa hoja hii unaweza kutambuka wigo wa mhimili wa Bunge na kuleta shida kwenye mhimili wa serikali (japo Bunge linaisimamia serikali). Shida iko hivi:-

1. Uelewa wangu unanishawishi kwamba hoja inaweza kuwa kizungumkuti kwa VP.

2. Anayeshikilia nafasi ya VP kwa sasa ndiye alikuwa jikoni wakati wa awamu ya 5 hivyo kwenye awamu ya 6 yeye ni Institutional Memory wa yaliyotokea kwenye awamu ya 5 kwa awamu ya 6.

3. Je, kwenye uchunguzi huo wa akaunti hiyo ya deni la taifa kwa awamu ya 5 siyo kwamba utamuhitaji VP akae pembeni kupisha uchunguzi huru huo? Je, Tz tunao utamaduni huo?

4. Chama cha mtoa hoja kinawezakuwa salama kweli kama ukaguzi huo ukifanyika na kuthibitika kwamba utaratibu haukufuatwa. Ikumbukwe kwa chama cha mtoa hoja mchakato wa uchaguzi mkuu unaofuata huwa unaanza pale serikali inapomaliza kuundwa; ya uchaguzi mkuu unaokuwa umemalizika, kwa maana ya kwamba hata muda huu hoja inapotolewa tayari chama kiko kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu unaofuata.

5. Kama uchunguzi wa Bunge ukigundua madudu kwenye akaunti ya deni la taifa kwa wakati wa awamu ya 5 je, siyo kwamba hoja ya mtoa hoja inawaweka pabaya Ma-CAG wa awamu za 5 na 6?

6. Je, kama awamu ya 6 ikimaliza muda wake, nani anajuwa kama awamu ya 7 nayo itakuja na watoa hoja wa aina hii kwenye hoja hii ya akaunti ya deni la taifa? Taifa litakuwa linajenga utamaduni gani wa kutafutana mchawi kila awamu?

7. Je, mahusiano mazuri yaliyoko baina ya wakuu wa mihimili ya Bunge na Serikali yanawekwa rehani endapo taarifa ya ukaguzi/uchunguzi itathibitisha mashaka ya mtoa hoja?

NB.
Juzi nilisoma gazeti moja kwamba deni la taifa limefika Tzs.64 tr hoja ya mtoa hoja ilitaja Tzs.9 tr kama ndiko deni la taifa lilifika. Sasa kwa hesabu ndogo tu zisizo za kitaalam, kama awamu ya 5 ilifikisha deni la taifa Tzs.9 tr ina maana kwa mujibu wa gazeti hilo na hoja ya mtoa hoja kuna ongezeko la Tzs.55 tr za awamu ya 6 ambayo pia mtoa hoja ni kiongozi wa awamu hii kwa nafasi yake ya Ubunge kama alivyokuwa pia kwa awamu ya 5 anayotaka ichunguzwe. Aidha, kati ya Tzs.9 tr za awamu ya 5 na Tzs. 55 tr za awamu ya 6 (kufanya jumla ya Tzs.64 tr awamu gani imekopa zaidi? Japokuwa hoja ya mtoa hoja imejikita katika kutilia mashaka juu ya uwazi na matumizi ya awamu ya 5 kwenye akaunti hiyo ya deni la taifa na siyo nani kakopa zaidi).

Lakini pia hoja hiyo ya mtoa hoja inatambuka zaidi na kuwateta wataalam wa mipango kwasababu kama awamu ya 6 imekopa basi ni kwa ajili ya kumalizia miradi mikubwa ya maendeleo ya awamu ya 5 maana miradi mipya ya awamu ya 6 haijawa mingi kiasi cha kukopa Tzs.55 tr ndani ya miezi 7 wakati awamu ya 5 ilifikisha deni la taifa kwenye Tzs.9 tr kwa miaka mi-5. Sasa hapa wataalam wa mipango ndiyo wamekosea au kiongozi wa mhimili wa serikali ambayo mtoa hoja ndiyo alikuwa kinara wa kuiweka madarakani?

Nadhani tupime kina kabla hatujavua nguo kuvuka mto.
Mataga bwana,acha mparuane macho.
 
Nyie maccm ni ma-bure kabisa! Hoja kuu ni kuficha uozo tu! Eti vp ataumbuliwa, mara awamu ya 7 nao wataibua madudu ya hawa 6! Ndo maana mkapitisha ile misheria ya kuto kushitakwa mkimliza awamu zenu za wivi?!! Mlaaniwe maccm!
 
Nyie maccm ni ma-bure kabisa! Hoja kuu ni kuficha uozo tu! Eti vp ataumbuliwa, mara awamu ya 7 nao wataibua madudu ya hawa 6! Ndo maana mkapitisha ile misheria ya kuto kushitakwa mkimliza awamu zenu za wivi?!! Mlaaniwe maccm!
Mkuu,
Maumivu-ya-ukweli hayana dawa ya kuyatuliza, vumilia!
 
Back
Top Bottom