Hoja ya Spika Ndugai: Nitawafukuzaje wabunge ambao Rufaa zao hazijasikilizwa na Baraza kuu kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA?

Hoja ya Spika Ndugai: Nitawafukuzaje wabunge ambao Rufaa zao hazijasikilizwa na Baraza kuu kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA?

Hao chadema wako very very selfish Yani wew mwanaume unapigania mwanamke afukuzwe kazi yake kisa wew huna that's very foolishness and stupidity,, Spika kawajibu kwa hoja sana sana huwezi tu kumfukuza kazi mtu hivi hivi bila a fair justice never..
Mkuu ni kweli kabisa huoni tatizo kwenye hii issue ya uviko19?
 
Kwahiyo ukifungwa jela, halafu ukakata rufaa mahakamani kuhusu hukumu yako.

Kabla rufaa yako haijasikilizwa , hukumu yako inafutwa na unakuwa free?
Kuna order inayotolewa inayoitwa stay for execution kuna baadhi zinazo operate automatically baada ya ku appeal na suala lolote linakuwa res sub judice na kuna nyingine lazima u apply mahakama itoe zuio caviat
 
Hoja kuu sio kufukuzwa. CDM wanadai hawajawateua hao wabunge kupitia vikao vyao vya kikatiba. Hapo Mh Dugai mbona anapakwepa? Kufukuzwa likikuwa ni zao la kukiuka utaratibu za chama.

Chama chao kimesema hakijawateua kwa kuwa hakuna vikao vilivyokaa. Mbona hakikusikilizwa? Vikao vya rufaa ndio muhimu sasa?

Hata kama utaratibu wa kuwafukuza haukufuatwa, lakini hilo la kuteuliwa na vikao ama la ni factual issue. Kwa hivyo hoja kuu ni kuwa hawakuteuliwa na cdm kama sheria inavyotaka.....hiyo ya kutokuwa wanachama wa chama cha siasa ni nyongeza ambayo haina athari kwenye hoja kuu.

Pathetic!

Umesema jambo la msingi sana...

Na kwa kuongezea tu, mimi kwa ishu hii huwa najiuliza maswali kadhaa nashindwa kupata majibu kabisa na badala yake huishia kuamini tu kuwa, these are one of the dirty CCM political games kwa kutumia watu wenye mamlaka kama huyu Spika kwa manufaa ya CCM kuendelea kuishi na kutawala kwa kitambo kidogo..

#1. Spika anakuwa pale kwa ajili ya kutekeleza na kulinda katiba ya nchi au ya vyama vya siasa?

#2. Wenye wajibu wa kujitetea na kuthibitisha uhalali wa uanchama wa chama cha siasa fulani ni nani? Ni mtu wa tatu (kwa scenario hii ni Spika Ndugai) au mwanachama mwenyewe mwenye mgogoro na chama chake?

#3. Ni chombo gani kisheria chenye kutoa haki kwa watu kwa mujibu wa sheria na katiba ya JMT? Obviously, ni mahakama... au siyo? Je, mbona hapa Spika anaonekana kama anafanya kazi ya "UWAKILI WA KISHERIA" kwa kina mama hawa 19 nje ya utaratibu wa kimahakama?

#4. Je, ni kwanini hawa kina mama 19 kama wanadhani hawatendewi haki na chama chao kwa hiki kinachoitwa "natural justice" wakaenda mahakamani kuishtaki CHADEMA kwa kutotenda haki ili waendelee kuulinda ubunge wao kwa muda fulani? Na kwa ninavyofahamu Mimi, wanaweza kufungua shauri pia mahakamani kuiomba iamuru CHADEMA kusikiliza rufaa yao iwapo tu wanaamini chama kinafanya infringement ya haki zao za kikatiba..

#5. Mwisho kabisa mtu anaweza kujiuliza, kwamba, ina maana Spika Ndugai hajui kabisa kuwa haki za kisheria za watu wakiwemo wabunge hushughulikiwa na mahakama kwa utaratibu huu?

Spika Ndugai nadhani ina matatizo ya akili, siyo bure..

Anachotaka CHADEMA wafanye, anajua kabisa hawatafanya ujinga wake...

Na kwa lugha rahisi kabisa, ni kuwa, Spika anataka kufunika udhaifu na makosa yake kwa kuendelea kufanya mlolongo wa makosa mengine ya kisheria na kikatiba...

Akumbuke jambo moja, kuwa, ALWAYS KARMA IS A BITCH, na haina msamaha kwa watu dizaini ya Ndugai mwenye cheo cha U - Spika kwa leo...

Sijui ni kwanini wanasiasa wakatili na wasiotenda haki hawajifunzi kwa Hayati John Pombe Magifuli....!!
 
Spika kwa akili zake finyu anafikiri kuwakingia kifua wabunge feki bungeni ati anamkomoa Mh. Mbowe, BAWACHA na wana mageuzi wote nchini - very low... hajui kwamba anavunja KATIBA ya nchi aliyoapa kuilinda na kuitetea kwa nguvu zote huku akimtaja Mwenyezi Mungu wake kama shahidi.
 
Hoja kuu sio kufukuzwa. CDM wanadai hawajawateua hao wabunge kupitia vikao vyao vya kikatiba. Hapo Mh Dugai mbona anapakwepa? Kufukuzwa likikuwa ni zao la kukiuka utaratibu za chama.

Chama chao kimesema hakijawateua kwa kuwa hakuna vikao vilivyokaa. Mbona hakikusikilizwa? Vikao vya rufaa ndio muhimu sasa?

Hata kama utaratibu wa kuwafukuza haukufuatwa, lakini hilo la kuteuliwa na vikao ama la ni factual issue. Kwa hivyo hoja kuu ni kuwa hawakuteuliwa na cdm kama sheria inavyotaka.....hiyo ya kutokuwa wanachama wa chama cha siasa ni nyongeza ambayo haina athari kwenye hoja kuu.

Pathetic!
Walimtoaje Nusrat Hanje gerezani na kwenda kumuapisha bungeni? CCM ni chama cha hovyo sana
 
lissu alikuwa anajifanya kuwa kila mtu anajuwa kuwa anaumwa kumbe akasahau kuwa taarifa ya maandishi lazima halafu akawa anadanganya bado anaumwa huku anaendelea kuzurura ulaya na kuichafua nchi huyo mhuni
Unaelewa 'principles of natural justice' maana yake au unabwabwaja tu?
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
Ndugai alipelekewa barua ya CHADEMA kwa maandishi, hizo hoja zake za kijinga amezipeleka kwa maandishi?
 
Mimi nadhani Chadema wameshamaliza kazi yao, kazi iliyobaki ni hao walioapa kuilinda na kuitetea Katiba kufanya yao.

Chadema wasije yumba juu ya maamuzi yao kwani Dunia imejionea na Karma itaamua.
Ni swala la muda tu kila kitu kitapata haki yake
 
Spika anatumiwa kuna watoa tamko moja tu wafukuzwe au wasifukuzwe wapo kimya ndugai hana ujanja juu yao
Katiba mbovu sana hii
Suala la COVID-19 ni uhalifu wa kidola. Dola yote imehusika na aliyelifikisha kwenye mkwamo huu ni kibwengo jiwe.

  • Mahakama ( Hanje kutolewa jela mkuku mkuku kwenda kuapishwa )
  • Serikali ( NEC kwa kushirikiana na ikulu kufeki majina na kuyapeleka bungeni kwa Ndugai )
  • Bunge ( Kupokea wabunge wasioleweka na kuwaapisha ). Na kama hilo halitoshi ni kuendelea kuwalinda hata baada ya kufukuzwa uanachama.

Lengo kuu ni MOJA.

- Kuvizia pesa za mabeberu takribani kama trilioni 2.

Wakati Kibwengo anapora uchaguzi wote nchi nzima hakujua kama kuna kamati za bunge mabeberu ili watoe hela zinatakiwa kuwa na wabunge wa upinzani maana hakuwa na akili.
 
Suala la kufukuzwa ni suala la mwisho kabisa,in the first place hao Covid 19 hawakuwahi kuwa proposed na chadema kama wawakilishi wao wa vitu maalum,

ni list ambayo imetoka from nowhere then ikaenda tume ya uchaguz kisha haraka haraka ikakimbizwa bungeni,na chadema walishaiandikia tume ya uchaguz kuyakana hayo majina,SASA why ndugai aache kudeal na root cause ya hilo tatizo anadeal na matokeo?
 
Tukisema Tanzania hatuna SPIKA tuna maanisha - hamna kitu humu!!

 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
ndugai aka sabufa atuambie hao covid-19 waliingiaje bungeni na kwa tiketi ya chama gani
 
Chama chao kimesema hakijawateua kwa kuwa hakuna vikao vilivyokaa. Mbona hakikusikilizwa? Vikao vya rufaa ndio muhimu sasa?
Hii issue ina complications flani. Chama hakijawateua na kuna mtu/watu/kikundi kimefoji barua na kuipeleka NEC then NEC wakaact accordingly na kumjulisha speaker.

Sasa je, CHADEMA wanapaswa kufanya nini? ni sahihi kwao kuandika barua kwa speaker directly kumwambia asiwatambue wale au wanapaswa kuandika barua NEC? Kuandika barua tu inatosha wakati kuna jinai kubwa imefanyika? CHADEMA walipaswa kuchukua hatua gani zaidi ya kuandika barua tu?
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Back
Top Bottom