Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Huna hoja mkuu Zanzibar ina ukubwa wa wilaya mbili za huku bara, hicho kinachopelekwa huko kimeanza kwenda jana au juzi?.

Unapalilia chuki na madhara yake yanaweza kabisa kuja kuwa sumu kama sio leo basi hata muongo mmoja ujao.
Tunayosema hapa ni mageni?
Maalimu Seif kayasema hadi anaingia kaburini
OMO, Jussa, Duni wanayasema kila siku achiia mbali walioko mitandaoni
Wazanzibar wanamlaani Nyerere '' Lanatullah' aliyeleta Muungano kila siku. Mbona hutkuwahi kukisikia
Wazanzibar ndio wamerudisha Utanganyika tena kwa jina

Mbona hatukwahi kusikia ukikemea?

Kuhusu Ukubwa wa Zanzibar, nitajie Wilaya moja mja tu ya Bara yenye Mbunge aliyechaguliwa na watu 3,300!
Tupe SqKM za Zanzibar halafu tafuta Wilaya moja tu ulinganishe
 
Hakiuna kulipa kisasi, Tanganyika ni dude kubwa sana haliwezi kulingana na Zanzibat. Kinachotokea sasa hivi ni kuchoshwa na kelele na madai ya kipuuzi ya Wazanzibar. Mfano, wameondoa Uhamiaji katika mambo ya Muungano, unaelewa hilo? Zanzibar wanapokuwa juu ya katiba ya JMT na kuwa raia wa daraja la I kwa upendeleo wakati hawana mchango wowote kwa maendeleo ya Tanganyika inakera! Tunahitaji muda wa kufikiri mambo muhimu si kaeneo ka watu laki 5 milioni 1 wakiishi Tanganyika.

Yes tulimpinga kwasababu alifanya hayo na mfano mmoja ni Uwanja wa Chato ambao ni hasara.
Tulimpinga kwa kauli zake za kipuuzi kuhusu watu wa kanda fulani ''watusubiri'
Watu wote waliompinga ni wale wanaotaka umoja. Na hata Kikwete Tulimpinga kwa kuendekeza ufisadi.
Mkapa tulimpinga kwa kupallilia ufisadi. Mwinyi tulimpinga kwa sera zake hasa za uchumi.
Nyerere tunamsema kila siku na mimi ni mmoja wao hasa kuua vyama ya ushirika na ujamaa
Samia atapingwa without exception!

Kwahiyo unadhani kama hayo yapo Wanaozuia ni Wazanzibar!

Hapana tumewavumilia na sasa ni kero kwetu, tunahitaji muda wa kufikiri namna ya kushirikiana na nchi zinazotuzunguka zenye population ya 100M. Kila siku wao wanataka hawana cha kuwajibika! hapana

Nimekuuliza, tushawishi hapa jamvini kwanini Tanganyika inahitaji Muungano kiasi cha kutoa rasilimali nyingi kiasi hicho. OMO kasema 54% ya bajeti ya Zanzibar inategemea pesa za Tanganyika, na bado wanataka kupewa zaidi.
Rasilimali zinatolewa kila eneo la Tanzania cha muhimu tuongeze pato la taifa ili na zenyewe ziongezeke kwa wingi wake.

Bado haujanishawishi kuachana na visiwa hivi kwa hoja za mgao wa kinachopatikana hapa Tanzania. Ukikaa na mzenji atakuja na mawazo tofauti yenye kudhani kuwa mtu wa bara anamuonea mzenji.

Ni hisia binafsi za kila mtu kadri ya uelewa wake. Muungano ni muhimu kuliko chochote. USA wana miaka 247 ya uwepo wao na ni kwa sababu ya umoja wao.

Hata kama jimbo la Los Angeles linazalisha mara tano zaidi ya jimbo la Mississipi wanaendelea kuwa pamoja wakijua kuwa ule umoja wao ndio silaha yao muhimu dhidi ya kina Russia na China.
 
Yes tunaungana kwasababu za Uchumi1 matatizo mengi duniani yanatokea kwasababu za uchumi.
Ni uchumi tu! Tunahitaji mshiriki wa Muungano. Zanzibar wanadai hadi inakera! Sasa hivi wanataka eti kuwe na formula ya kugawana rasilima za Tanganyika. Wao kila siku ni kugawana hutawasikia wakishiriki kuchangia au kujenga.

Hakuna chuki ni hisia zako. Maalim Seif alidai mamlaka kamili miaka zaidi ya 20, mbona hujasema ni chuki
Jussa , OMO na Duni kila siku wanatukana Muungano mbona hujaona ni chuki
Sasa hivi wanataka twende Zanzibar kwa passpor, hujaona ni chuki
Wanasema wao si Watanzania huoni kama ni chuki
Wazanzibar wanamtukana Mwl Nyerere wakisema ''Laanatullah' kila siku huoni ni chuki
Hawataki hata ndizi ivuke bahari lakini mkono wa tembo kutoka Mombasa ni sawa, huoni ni chuki
Wana vitambulisho vya kuwabagua Watanganyika, huoni kama ni chuki

Kwa taarifa yako waliorudisha neno Tanganyika wakisema '' Watanganyika wamelala' ni Wakoloni weusi , wanaiba rasilimali (wanaiba zero) ni Wazanzibar!

Kwanini Mtanganyika akisema yaishe mnasema ni chuki! Yaani yote hapo juu hukuwahi kuyasikia.
Hapana, wapewe mamlaka kamili sisi tunahitaji Tanganyika. Ikiwa watataka muungano ni wao waje waombe, Tanganyika haina cha kupoteza
Ningekuwa na uwezo visiwa hivi ningevisogeza mbali kabisa kutoka hapo vilipo, kauli ya Mwalimu Nyerere miaka ile ya mwanzoni mwa uwepo wa Tanzania.


Kuvumiliana ndio mpango mzima.
 
Tunayosema hapa ni mageni?
Maalimu Seif kayasema hadi anaingia kaburini
OMO, Jussa, Duni wanayasema kila siku achiia mbali walioko mitandaoni
Wazanzibar wanamlaani Nyerere '' Lanatullah' aliyeleta Muungano kila siku. Mbona hutkuwahi kukisikia
Wazanzibar ndio wamerudisha Utanganyika tena kwa jina

Mbona hatukwahi kusikia ukikemea?

Kuhusu Ukubwa wa Zanzibar, nitajie Wilaya moja mja tu ya Bara yenye Mbunge aliyechaguliwa na watu 3,300!
Tupe SqKM za Zanzibar halafu tafuta Wilaya moja tu ulinganishe
Hawajielewi wazenji wanadhani kuwa wajomba zao waarabu watawasaidia siku wakiachana na bara, ni roho za uislamu zinawasumbua.
 
Wanaodhoofisha muungano si OMO, Jusa, Duni na wengine wenye kauli kama zao. Ni CCM walioshika kila kitu wanaobadilisha katiba. Cheo cha Makamo wa kwanza ni ceremonial.
 
Wameondosha lini uhamiaji kwenye muungano. Nadhani bado ipo chini ya Wizara ya Mambo ya ndani.
Hayo ya kuondoa Uhamiaji si maneno yangu, ni maneno ya makamu wa kwanza wa Rais Othman Masoud (OMO)

Rejea bandiko 196 nimeweka habari kwa hisani ya gazeti la Mwananchi. Soma kipande chini kabisa kinachosema ' giza neno mbele''. OMO anasema hivi ' kuna mambo yameondolewa katika Muungano lakini akija Kiongozi mwingine anaweza kuyarudisha' na kwamba kuondolewa ni hisani.
OMO akataja haya
Ushuru wa Forodha
Bandari
Uhamiaji
Mafuta na Gesi

OMO ametupa uhakika wa kile tulichohoji siku nyingi kwamba Rais wa Zanzibar ana mamla gani kikatiba kutoa Uraia?
Rais Mwinyi alitoa Uraia kwa raia wa kigeni. Sasa kwa maneno ya OMO kumbe Uhamiaji imeondolewa kinyemela.

Lakini OMO kasema ukweli, mapato ya Uhamiaji Zanzibar si ya Muungano , na hii ni kwasababu Uhamiaji imeondolewa kwa siri kama ilivyokuwa Bandari, mafuta na gesi.

Pascal Mayalla nilikuuliza kama unajua makusudi kabisa kwasababu wewe husema '' Uraia ni wa Tanzania'' kumbe nyuma ya pazia Uhamiaji haimo, kwa mujibu wa OMO na ushahidi wa gazeti upo.

Mag3
 
Ningekuwa na uwezo visiwa hivi ningevisogeza mbali kabisa kutoka hapo vilipo, kauli ya Mwalimu Nyerere miaka ile ya mwanzoni mwa uwepo wa Tanzania.


Kuvumiliana ndio mpango mzima.
Sikubaliani na kauli hiyo hadi utakapoleta ushahidi Mwalimu alisema lini na wapi
 
Wee Mayala unasema hakuna utanganyika wala uzanzibari wote watanzania, sasa kwanini mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar, yaani Raisi katoka Zanzibar na anaweza kumiliki ardhi Zanzibar lakini anaotuongoza hatuwezi kumiliki ardhi Zanzibar kama Raisi wetu, huoni Hilo ni tatizo? huo sio muungano
 
Bado haujanishawishi kuachana na visiwa hivi kwa hoja za mgao wa kinachopatikana hapa Tanzania. Ukikaa na mzenji atakuja na mawazo tofauti yenye kudhani kuwa mtu wa bara anamuonea mzenji.
Huu ulikuwa upuuzi wa Wazanzibar zama hizo, siku hizi tunakwenda na namba. Kwamba kwa uchumi wa Zanzibar wanaonewa wapi? Mwenyekiti wa ACT kasema 54% ya mapato ya uchumi yanatoka Muungano ambao ni Tanganyika.

Hizi hadithi za Wazanzibar tulishamalizana nazo, hakuna ulinganifu hata kwa bahati mbaya.
Kuna watu walikuwa wanawasomea vitabu .

Waulize, bajeti ya Ulinzi ni 3.3, wao wamechangia kiasia gani?
Waulize Bajeti ya mambo ya ndani mwaka jana ilikuwa 1.3 T, wao wanachangia nini
Waulize, ukiache kelele za kutaka nafasi za ubalozi, mambo ya nje wanachangia nini
Waulize, Muungano na Wizara na taasisi zake wao wana mchango gani
Waulize ile 4.5% ya Bajeti ya Tanganyika ni kiasi gani ukilinganisha na Bajeti ya SMZ
Waulize pesa za mikopo wanalipa kutoka bajeti gani ya SMZ
Kuna fedha nyingi sana wanapata kutoka bara wao wakisema Muunganp

Kwasababu wao wanalalamika, tunawaambia wana hiari! Tanganyika haina cha kupoteza!
Muungano ni muhimu kuliko chochote. USA wana miaka 247 ya uwepo wao na ni kwa sababu ya umoja wao.
Yes Muungano ni muhimu lakini lazima uwe muungano wenye tija, muungano usio na kelele
Kwa mfano wa USA, unakubaliana nasi kwamba sasa ni wakati Tanganyika iwepo na Zanzibar iwepo
Kabla ya kuendelea na muungano watasema wao, wapewe kura ya maoni.

Swali langu lipo pale pale, Tanganyika ina fadika na nini, na ina nini cha kupoteza?
Hata kama jimbo la Los Angeles linazalisha mara tano zaidi ya jimbo la Mississipi wanaendelea kuwa pamoja wakijua kuwa ule umoja wao ndio silaha yao muhimu dhidi ya kina Russia na China.
Yes! lakini hakuna mtu anatoka California kwenda Mississipi kwa Passport. Na Muungano wa USA una mambo machache ya Federal mengine ni state zinatawala. Ndicho tunahitaji sasa kwamba tuwe na Tanganyika halafu Wazanzibar kama wanataka waieleze Tanganyika ! Sisi Tanganyika hatuna cha kupoteza
 
Pascal Mayalla nilikuuliza kama unajua makusudi kabisa kwasababu wewe husema '' Uraia ni wa Tanzania'' kumbe nyuma ya pazia Uhamiaji haimo, kwa mujibu wa OMO na ushahidi wa gazeti
Mkuu Nguruvi3, nimeshindwa kabisa kuelewa jinsi akili za baadhi ya Watanganyika wenzetu zinavyofanya kazi.

Karibia nusu ya wanaojitambulisha kama Wazanzibari makazi yao ni Tanganyika na walezi wao ni Watanganyika.

Kama vile watoto wadogo, kwa kauli ya Baba wa Taifa, ingawa tumewapakata wanatunyea na tukiwaacha wanalia.

Inavyonekana sasa baada ya kupata ufadhili upya kutoka wa wajomba zao hawatuhitaji tena Watanganyika.

Ila wakikumbuka maziwa na asali ya mama Tanganyika bado wanasita kwa hadaa za mama wa kambo.

Kwa msaada wa wajomba na kina Pascal Mayalla watakomba kila wanaloweza na kuiacha Tanganyika hoi.

Hakika uvumilivu una mwisho…
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081

Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali

Umenikumbusha kauli ya JPM kuwa Mayala ni jina la kisukuma na maana yake ni njaa. Ila hakuchukua hatua!
 
Huu ulikuwa upuuzi wa Wazanzibar zama hizo, siku hizi tunakwenda na namba. Kwamba kwa uchumi wa Zanzibar wanaonewa wapi? Mwenyekiti wa ACT kasema 54% ya mapato ya uchumi yanatoka Muungano ambao ni Tanganyika.

Hizi hadithi za Wazanzibar tulishamalizana nazo, hakuna ulinganifu hata kwa bahati mbaya.
Kuna watu walikuwa wanawasomea vitabu .

Waulize, bajeti ya Ulinzi ni 3.3, wao wamechangia kiasia gani?
Waulize Bajeti ya mambo ya ndani mwaka jana ilikuwa 1.3 T, wao wanachangia nini
Waulize, ukiache kelele za kutaka nafasi za ubalozi, mambo ya nje wanachangia nini
Waulize, Muungano na Wizara na taasisi zake wao wana mchango gani
Waulize ile 4.5% ya Bajeti ya Tanganyika ni kiasi gani ukilinganisha na Bajeti ya SMZ
Waulize pesa za mikopo wanalipa kutoka bajeti gani ya SMZ
Kuna fedha nyingi sana wanapata kutoka bara wao wakisema Muunganp

Kwasababu wao wanalalamika, tunawaambia wana hiari! Tanganyika haina cha kupoteza!

Yes Muungano ni muhimu lakini lazima uwe muungano wenye tija, muungano usio na kelele
Kwa mfano wa USA, unakubaliana nasi kwamba sasa ni wakati Tanganyika iwepo na Zanzibar iwepo
Kabla ya kuendelea na muungano watasema wao, wapewe kura ya maoni.

Swali langu lipo pale pale, Tanganyika ina fadika na nini, na ina nini cha kupoteza?

Yes! lakini hakuna mtu anatoka California kwenda Mississipi kwa Passport. Na Muungano wa USA una mambo machache ya Federal mengine ni state zinatawala. Ndicho tunahitaji sasa kwamba tuwe na Tanganyika halafu Wazanzibar kama wanataka waieleze Tanganyika ! Sisi Tanganyika hatuna cha kupoteza
Hakuna binadamu zaidi ya wawili wanaoweza kuishi pamoja bila ya kuwepo kelele au kutofautiana, hiyo ni sifa ya kiumbe chenye uhai.

Mchango wao ni kuwa sehemu ya taifa la Tanzania. Watakapoanza kujitenga ndio tutaona kuwa hizo figures hazina faida yoyote kulinganisha na kuwa kitu kimoja kama taifa.
 
Wee Mayala unasema hakuna utanganyika wala uzanzibari wote watanzania, sasa kwanini mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar, yaani Raisi katoka Zanzibar na anaweza kumiliki ardhi Zanzibar lakini anaotuongoza hatuwezi kumiliki ardhi Zanzibar kama Raisi wetu, huoni Hilo ni tatizo? huo sio muungano
Zanzibar ni sawa na wilaya moja ya mkoa wa Tabora, uache kumiliki ardhi tupu iliyojaa huku bara uende ukatake kuimiliki ya Unguja!, hizo ni nongwa tu.
 
Miaka hiyo hiyo ya sitini baada ya kuwa tumeungana, sio kila kinachofanyika ndani ya JMT basi ukitambue wewe kwa ushahidi fulani.
Kuna hadithi za Wazanzibar za kumfanya Nyerere aonekane dhalimu na hii ni mojawapo. Hoja hii ililetwa mwaka 2011 tukawauliza watuambie Nyerere alisema lini, akiwa na akina nani na wapi! hadi leo hakuna anayesema. Ni uzushi tu

Juzi nimesikia akina Jussa wanasema eti Zambia walitaka kuungana na Tanzania, wwalipoona muundo wa Muungano wakakacha. Ni hadithi za kwenye kahawa! ukiuliza nani alisema wanasema '' marehemu Maalimu' alisema

Majungu na upuuzi tu!
 
Kuna hadithi za Wazanzibar za kumfanya Nyerere aonekane dhalimu na hii ni mojawapo. Hoja hii ililetwa mwaka 2011 tukawauliza watuambie Nyerere alisema lini, akiwa na akina nani na wapi! hadi leo hakuna anayesema. Ni uzushi tu

Juzi nimesikia akina Jussa wanasema eti Zambia walitaka kuungana na Tanzania, wwalipoona muundo wa Muungano wakakacha. Ni hadithi za kwenye kahawa! ukiuliza nani alisema wanasema '' marehemu Maalimu' alisema

Majungu na upuuzi tu!
Mpango mzima ni kuungana, kwanini Tanzania tufikirie kuungana na Sudan Kusini walio kilomita zaidi ya 3000 halafu tufikirie wakati huo huo kutengana na Zanzibar?. Ni somo lenye kuhitaji hekima nyingi sana kuliko jazba na visasi.
 
Back
Top Bottom