Home Shopping Centre wazusha taharuki Kariakoo

Home Shopping Centre wazusha taharuki Kariakoo

Tutabishana hadi kiama hapa lakini tutazame source,ni kwa nini watz wengi wameamua kufuata mkondo wa ukwepaji kodi na rushwa?je,hizo kodi,taratibu za serikali pamoja na huduma za wafanyakazi wa sekta hii kama TRA,bandari n.k zinaruhusu mtu wa kawaida kutumia njia za halali kupata mali yake na kufanya biashara kwa mafanikio?hebu jaribu kusafirisha kacorolla kako toka Japan kwa kufuata kila njia halali uone ni kwa nini rushwa haiishi Tz!sasa sielewi kuwa watu kama Said wanatake advantage ya mazingira au wako ndani ya mtandao maalum wa wakubwa wanaohakikisha njia za halali zinakuwa ngumu ili tuwapigie magoti na kuwapa wao "kodi" badala ya serikali.
 
Haya yote ni makelele, mwisho wa siku makontena yataachiwa na huyo Masamaki ataondolewa hapo Bandarini. Hii nchi inaongozwa na mafisadi, usipo kubaliana nao lazima wakutose! Tusubiri tuone!
 
Nataka niwatangazie tangu Said ashtukiwe kariakoo imetulia kwa kupaki olela magari yake kwani kabla alikuwa anapaki anavyotaka magari yake na kuziba njia kariakoo nzima bila kuchukuliwa hatua zozote. sasa kariakoo safi gari zake hazizibi tena njia.
 
Mimi ni mfanyabiashara na nimefanya biashara na maagent wengi na hawa maclering wanazingua sana mambo yangu hapa ni machache kama ifuatavyo...
1. Hapa tusichanganye mambo ya vita za madaraka ya ukamishna wa tra, vita ya maclearing na maisha ya maskini
2. Hakuna asiyejua masamaki alikuwa manager wa mafuta na alivyokuwa anapitisha mafuta bure! Leo mafuta yanapita na mzigo wote anahamishia kwenye makontena
3. Hakuna asiyejua ubabaishaji, wizi, utapeli na rushwa wa BAADHI ya maclearing, kama ametokea clearing mwaminifu lazma biashara itahamia kwake
4. Maclearing wengi ni mawakala wa rushwa za macustom officer ! Hawawezi kumpenda mtu straight.
Sasa vita zao wasiingize na sisi maskini watuache tufanye kazi vita zao wamalizane wao wenyewe ...
kitu kinachoitwa umasikini wa Watanzania ni kukosa huduma stahiki za kijamii (shule, matibabu, barabara, maji, umeme, makazi, chakula nk) ambavyo inabidi vitolewe na serikali. Serikali haina miradi wala haifanyi biashara, pesa yake inatokana na watu wake kulipa kodi - halali. Na kodi ispokusanywa ndio matatizo unayoyaona hivi leo.
Kama kweli ikithibitika kuwa hawa jamaa wanafanya mchezo wa kukwepa kodi basi hiyo ni sawa na uhaini, na kibaya zaidi isije kuwa sio Watanzania.
Kwa maana hiyo unachotaka kusema ni kama mtu ambaye anafaidika na mfumo wa ujambazi. Kwamba waporaji wanakugawia kiasi cha mali walizopora lakini hujafikiria wanaoporwa (wananchi wa kawaida) wana machungu kiasi gani.
Fuatilia Ulaya, Marekani, Brazil, China, India, Uarabuni wote hawa ni jinsi gani walivyo makini kwenye suala la kutoza kodi na sio ajabu ndio maana wanaendelea. Ukiseme kuwa serikali iachie wajanja wachache waunde 'TRA 'B' zao hatutaenda popote.
Yote haya yategemee ushahidi kama kweli kuna mchezo mchafu kama haupo basi apewe biashara zake aendelee

 
Tutabishana hadi kiama hapa lakini tutazame source,ni kwa nini watz wengi wameamua kufuata mkondo wa ukwepaji kodi na rushwa?je,hizo kodi,taratibu za serikali pamoja na huduma za wafanyakazi wa sekta hii kama TRA,bandari n.k zinaruhusu mtu wa kawaida kutumia njia za halali kupata mali yake na kufanya biashara kwa mafanikio?hebu jaribu kusafirisha kacorolla kako toka Japan kwa kufuata kila njia halali uone ni kwa nini rushwa haiishi Tz!sasa sielewi kuwa watu kama Said wanatake advantage ya mazingira au wako ndani ya mtandao maalum wa wakubwa wanaohakikisha njia za halali zinakuwa ngumu ili tuwapigie magoti na kuwapa wao "kodi" badala ya serikali.
juve2012, umeyanena vizuri haya mambo.
Kama tulivyoua elimu, afya na nyanja nyingine na sasa tunaua uti wa mgongo wa taifa ambao ni mfumo wa kodi. Hawa wanaoitwa wakubwa ni wanasiasa, na wanasiasa mpaka sasa tumeshaona kuwa uwezo wao wa kufikiri ni wa chini sana lakini wameendelea kuwapo hivyo kuthibitisha kuwa tatizo sio wao bali ni Watanzania kwa ujumla wao.
Sio ajabu Benki ya dunia iansema tumepoteza Us $1.2 billion mwaka jana kwa bandarini tu. Sasa hapa watu wanavyoongea kuwa huyu mtu mmoja tu anasimamia kiasi kikubwa hivi cha mizigo na yupo zaidi ya miaka kumi unapata picha gani kama si TRA kwa kipindi hicho kupoteza $ trillion 70!!??
Wanaosema tatizo ni mfumo wana hoja na tusisahau kuwa mfumo hauna jina lingine zaidi ya CCM

 
HOME SHOPPING CENTRE WAPO VIZURI WAPEWE PONGEZI ZAO.

Maadui wakubwa wao ni Wafanyabiashara Wakubwa waliojijengea MONOPOLY ktk Biashara Fulani na KATU KWA UDIKTETA hawataki Mwingine yeyote Aingilie!

Untouchables Vijana hawa Wamevunja Mwiko huu na wanachokipata sasa Kuchafuliwa ni Matokeo ya Mipango ya Muda mrefu ya watu hawa kupitia Vikundi,Magazeti na Watu Mbalimbali Kuwachafua,
Pia Baadhi ya Mawakala sio wote ambao Wanalalamikia Kuporwa sijui kazi zote na Hawa Vijana,Hivi ht ingekuwa Kweli ktk Zama hizi za Soko Huru ,Unaweza Kweli Kulalamika kwanini Kampuni fulani Wananunua Maji yake kuliko ya Kampuni yako na Kuanza Kuchafua kujenga UHALALI
Nilikuwepo ktk Kikao kimoja cha waziri na mawakala Nawachallenge Mawakala wa Nyuma waweke Hadharani Kuona wao wanalipa vp na hawa HSC wanalipa vipi!???
Ni Majungu Matupu tu kwa wasiojua wanakimbilia Kuhukumu tu,Nendeni TRA Mkaangalie rekodi kontena ya Bidhaa Tofauti walicholipa wao na wengine km Kuna Tofauti yoyote? Ulongo mtupu na Majungu WANAPATA KAZI TOKANA NA SERVICE YAO NZURI DOOR TO DOOR sio jambo linginelo lolote
 
HSC WANAJUA WANACHOKIFANYA...WATANZANIA WENGI WAVIVU UBUNIFU WA HAWA JAMAA UNAWACHANGANYA
DONT HATE THE PLAYER, HATE THE GAME...
Wakurugenzi wa Kampuni Hii wana Asili ya Saudia na Yemen,Wana Uhusiano wa Karibu na Viongozi wa Saudia Mtakumbuka alipokuwepo Balozi aliyepita wa Saudia waliwahi kupitia yeye HSC kutoa Pampu 800 Za Maji Zilizosambazwa Nchi Nzima Kusaidia Mama Zetu na Dada Zetu Vijijini kwa USHAWISHI wao
Mmoja kati ya Matajiri wa Dunia hii wa Kisaudia TRILIONAIRE PRINCE TALAL AL SAUD AL WALEED alipozuru Nchini Walikuwa Wenyeji na Ndio walimpokea Airport na ht Kumpeleka Kwa Viongozi wa Serikali na walihudhuria Mazungumzo ya Uwekezaji
Sasa Ajabu gani kwa Mtu anayejua Medani za Biashara za kimataifa Vijana hawa kuwa Matajiri??!
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.
 
MAJUNGU HAYAFAI HSC WAPO VIZURI WAUNGWE MKONO
Vijana hawa Fedha Nyingi Wanappata Nje ya Nchi lakini Wanawekeza hapa Tanzania mfano kutokana na Uaminifu wao na Kuaminiwa na Watanzania wengi wanakusanya Kontena Nyingi sana kwa Mwezi na kupewa SPECIAL RATES na wenye MELI,Hivyo wanapata Faida kidogo kwa Kila kasha na kwakuwa Mizigo ni Mingi Hutengeneza Faida kubwa(NJE YA NCHI)
Wanatoa Misaada Mingi kwa Jamii Kuliko hao Wafanyabiashara Matycoon Wanaofyonza Nchi kwa Mabilioni na mmekaa Kuwatukuza,Maskini vijana hawa Wanashambuliwa ajili ya Mafanikio yao ya Muda mfupi,Tufanye Kazi na Kuacha Majungu
 
Mada ni Home Shopping Centre au mada ni makontena kukwama bandarini?

Hivi hawa kina Rished Bade hili limewashinda kabisa?
 
mkuu kipasta, hili suala sasa naanza kuliogopa maana sikujua kama lilikuwa na maelezo haya yote.
Hebu linganisha maelezo yako na haya ya kwenye gazeti la Tanzania Daima then utupe mwanga zaidi ya muendelezo wa hili suala.
HSC WANAJUA WANACHOKIFANYA...WATANZANIA WENGI WAVIVU UBUNIFU WA HAWA JAMAA UNAWACHANGANYA
DONT HATE THE PLAYER, HATE THE GAME...
Wakurugenzi wa Kampuni Hii wana Asili ya Saudia na Yemen,Wana Uhusiano wa Karibu na Viongozi wa Saudia Mtakumbuka alipokuwepo Balozi aliyepita wa Saudia waliwahi kupitia yeye HSC kutoa Pampu 800 Za Maji Zilizosambazwa Nchi Nzima Kusaidia Mama Zetu na Dada Zetu Vijijini kwa USHAWISHI wao
Mmoja kati ya Matajiri wa Dunia hii wa Kisaudia TRILIONAIRE PRINCE TALAL AL SAUD AL WALEED alipozuru Nchini Walikuwa Wenyeji na Ndio walimpokea Airport na ht Kumpeleka Kwa Viongozi wa Serikali na walihudhuria Mazungumzo ya Uwekezaji
Sasa Ajabu gani kwa Mtu anayejua Medani za Biashara za kimataifa Vijana hawa kuwa Matajiri??!
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.
TanzaniaDaima said:
Kikao cha Waziri Mgimwa, TRA balaa
MAWAKALA wa ushuru wa forodha (clearing agents) wenye uzalendo wameshtukia njama za kuwatumia kukwepa kodi kifisadi kupitia bandari ya Dar es Salaam na kuibua kiwewe kwa wahusika, imefahamika.
Hayo yalibainika katika kikao cha mawakala hao wakiwakilishwa na maofisa waandamizi wa kampuni zao na Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, kikao kilichohudhuriwa pia na wakuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kwamba mawakala hao wapatao 150 walishtukia njama za wenzao waliojaribu kumpotosha waziri ili wazuie operesheni ya TRA ya kuhakiki upya makontena yaliyokuwa yapitishwe bila kukaguliwa.
Baada ya kuwasikiliza mawakala hao na TRA, Waziri Mgimwa ambaye awali alionekana kutaka kulainika, alitaka sheria ifuate mkondo wake na operesheni ya kukagua upya makontena uendelee ili kujiridhisha hakuna ukwepaji kodi wowote na watakaobainika wachukuliwe hatua.
Baada ya Tanzania Daima kuandika habari za ukwepaji kodi kutumia utaratibu halali wa TRA kutoa mizigo inayolipiwa kodi bila kukaguliwa, mamlaka hiyo ilisitisha ghafla utaratibu huo ili kuchunguza madai ya kuwapo ukwepaji kodi mkubwa unaotajwa kuwahusisha vigogo ndani ya serikali na watu wazito.
"Wenzetu waliingia katika kikao hicho wakiwa na mbinu chafu za kutaka kumtumia waziri awatishe TRA ili makontena yao yanayokaribia 500 yatoke. Tukashtukia na kumwambia waziri utaratibu ufuatwe na yote yakaguliwe upya kujua yana nini ndani.
"Wamedanganya kuwa baadhi ya makontena wamedanganya yana viatu toka Dubai lakini ndani kuna magari, mengine wanasema kuna nguo za watoto kumbe kuna vitenge na vifaa vya electronics. Sasa kisheria ukishusha thamani ya mzigo TRA wanapandisha lakini udanganyifu wa aina ya mzigo ni kosa la jinai unataifishwa na kushtakiwa," anasema mtoa habari wetu.
Katika kikao hicho, mawakala hao walimpongeza Kamishna Mkuu wa TRA na wizara kwa kazi nzuri, lakini walilalamikia kitendo cha baadhi ya vigogo wa juu kuwaingilia katika kazi zao na hivyo kusababisha uhalifu unaofanywa na wakwepa kodi kuendelea kufanyika.
"Waliondoka wakiwa wameinamisha vichwa chini ila wanachofanya sasa ni kueneza propaganda kwenye magazeti kwamba kuna usumbufu unaosababishwa na TRA bandarini kumbe ni kuwabana wasikwepe kodi, hata kama kunakuwa na usumbufu, lakini ni vizuri kuokoa kodi," anasema.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, wahusika walikuwa wakitumia mwanya huo kwa kuficha thamani halisi ya mizigo na wakati mwingine kudanganya hata aina ya mizigo iliyomo ndani ya makontena na mara nyingi kwa kutumia nyaraka za kughushi.
Kampuni inayotajwa kuhusika kwa kiasi kikubwa ni ile maarufu kwa uuzaji wa bidhaa za nyumbani na wahusika wanaelezwa kujisahau sana na kufanya hadharani kwa kutumia majina ya vigogo wa juu serikalini.
"Nasikia mpango wa haraka walionao ni kuwahonga maofisa wa TRA wanaopangwa kwenda kufanya ukaguzi ili wakubaliane na kilichokuwa kimeandikwa kwenye nyaraka zao," anaeleza mtoa habari wetu.
Hata hivyo hali inaelezwa kuwa tete ndani ya TRA kutokana na taarifa hizo kuvuja na kuwafanya vigogo kuhaha na baadhi kutaka hata kuitelekeza mizigo yao na wengine kuwasababishia hasara kubwa wafanyabiashara waliowatumia.
"Waziri Harrison Mwakyembe aliambiwa haya yote alipokutana na wakurugenzi wa Clearing & Forwarding lakini pamoja na kujiita mpambanaji wa ufisadi alipuuzia kwa sababu zake mwenyewe mpaka vyombo vya habari viliporipoti na ndipo TRA wamechukua hatua," anaeleza mtoa habari huyo.
Kwa takriban miaka mitatu iliyopita serikali kama njia ya kuondoa mizigo bandarini mapema kwa kuepusha mlundikano na msongamano wa mizigo bandarini iliruhusu baadhi ya mizigo ya wateja wakubwa iwe inachukuliwa bandarini bila kukaguliwa.
Kitendo hiki japo kilionekana kuwa na lengo zuri kilikosolewa na wengi kwa madai kuwa kingeweza kutumika vibaya na baadhi ya hao wateja wakubwa kwa kukwepa kodi.
Mmoja wa wateja wakubwa aliyelalamikiwa hata na baadhi ya vyombo vya habari ambaye anajishughulisha na biashara ya vifaa vya nyumbani, sasa anafanya biashara ya uwakala wa mizigo.
Katika kikao ambacho waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe alifanya na wakurugenzi wa makampuni ya mawakala wa forodha moja ya mambo yaliyojitokeza ni kutaja kwa majina kampuni za mfanyabiashara huyo na nyingine yenye kumiliki Bandari kavu (ICD), kuwa zinalindwa na wakubwa.
Wakati ICD hiyo ya kuweka magari ikituhumiwa kwa utawala wa kudhalilisha na kuwatisha Watanzania bila aibu, kampuni hiyo ya vifaa vya nyumbani inatuhumiwa na mawakala wa forodha kwa ukwepaji wa kodi.
Inadaiwa kampuni hiyo inayomilikiwa na ndugu wawili wenye asili ya Kiarabu kuwa imekuwa na mtindo wa kuingia makubaliano na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na wadogo hasa wanaofanya kwenye eneo la Kariakoo kwamba mara waagizapo mizigo yao hasa kutoka China na Dubai watumie kampuni yake au kampuni zake dada ambazo zingine zina leseni za kutolea mizigo bandarini kama njia ya kulipa kodi kidogo.
Wateja wanaokubali kutumia mpango huu haramu hulipa kwao sh milioni 17 kwa kontena moja la futi 40 na sh milioni 12 kwa kontena moja la futi 20.
Kampuni hizo zinazodaiwa kulindwa na wakubwa zinalipia TRA sh milioni nane kwa kontena la futi 40 na milioni nne kwa kontena la futi 20 pamoja na gharama za bandarini ambazo si zaidi ya sh milioni 1.2.
"Inashangaza serikali kila siku inahaha kutafuta vyanzo vipya vya kuongeza mapato wakati hiki kilichoko tena chenye uhakika kikidhalilishwa na walafi wachache kwa kushirikiana na wenye mamlaka," alisema mtoa habari wetu.
 
kitu kinachoitwa umasikini wa Watanzania ni kukosa huduma stahiki za kijamii (shule, matibabu, barabara, maji, umeme, makazi, chakula nk) ambavyo inabidi vitolewe na serikali. Serikali haina miradi wala haifanyi biashara, pesa yake inatokana na watu wake kulipa kodi - halali. Na kodi ispokusanywa ndio matatizo unayoyaona hivi leo.
Kama kweli ikithibitika kuwa hawa jamaa wanafanya mchezo wa kukwepa kodi basi hiyo ni sawa na uhaini, na kibaya zaidi isije kuwa sio Watanzania.
Kwa maana hiyo unachotaka kusema ni kama mtu ambaye anafaidika na mfumo wa ujambazi. Kwamba waporaji wanakugawia kiasi cha mali walizopora lakini hujafikiria wanaoporwa (wananchi wa kawaida) wana machungu kiasi gani.
Fuatilia Ulaya, Marekani, Brazil, China, India, Uarabuni wote hawa ni jinsi gani walivyo makini kwenye suala la kutoza kodi na sio ajabu ndio maana wanaendelea. Ukiseme kuwa serikali iachie wajanja wachache waunde 'TRA 'B' zao hatutaenda popote.
Yote haya yategemee ushahidi kama kweli kuna mchezo mchafu kama haupo basi apewe biashara zake aendelee


Hata wewe pia unachangia kuangamiza Taifa hili kwa kutumia JF ambao pia hawalipi Kodi! Hakuna wa kumnyooshea Kidole mwingine TZ!

 
hsc wako vizuri tuache majungu.....
Vijana hawa Fedha Nyingi Wanappata Nje ya Nchi lakini Wanawekeza hapa Tanzania mfano kutokana na Uaminifu wao na Kuaminiwa na Watanzania wengi wanakusanya Kontena Nyingi sana kwa Mwezi na kupewa SPECIAL RATES na wenye MELI,Hivyo wanapata Faida kidogo kwa Kila kasha na kwakuwa Mizigo ni Mingi Hutengeneza Faida kubwa(NJE YA NCHI)
Wanatoa Misaada Mingi kwa Jamii Kuliko hao Wafanyabiashara Matycoon Wanaofyonza Nchi kwa Mabilioni na mmekaa Kuwatukuza,Maskini vijana hawa Wanashambuliwa ajili ya Mafanikio yao ya Muda mfupi,Tufanye Kazi na Kuacha Majungu
 
kumbe tunaonewa sisi wanyonge kuhusu kulipa kodi wakati wageni wanaididimiza nchi yetu jamani tunakwenda wapi je serikalli yetu haioni haya jamani
Wadau,kuna habari za uhakika chini kutoka kwa wadau wangu wa karibu kuwa hali ya mfanyabiashara said wa home shopping center si nzuri kibiashara...
kama thread moja iliyowahi kuandika habari zake humu ndani,inasemekana zaidi ya makontena 860 yamezuiwa bandarini kwa kile kinachoelezwa kufanya uchunguzi zaidi,mengi ya makontena haya yamewekwa bidhaa nyingine huku documents zikionyesha bidhaa nyingine.

hv karibuni amekuwa na ugomvi na mfanyabiashara mwingine Said salim bakhresa,na pia ameshagombana na Manji na yule muhindi mwingine tajiri zakaria,pia amekorofishana na subhashi Patel pale alipoanza kuingilia biashara ya mabati yanayofanana na ya kiwanda cha subash.

kuna wachina kama mia mbili hv nao mizigo yao iko kwenye hiyo ya huyu bwana so sad,kumbe na wao wanakwepa kodi

ukwepaji kodi huu wa Said,unajulikana wazi na kila mtu,hata serikalini,sijafahamu hasa kwann this time wameamua kumgeuka mwenzao! labda ndio yale maneno ya magufuli kuwa anaeweza kumtoa ni rais tu,maana huyu jamaa keshahamisha maafisa wa tra kama mia na hv!

my take:crime doesn't pay
 
hsc wako vizuri tuache majungu.....
Vijana hawa Fedha Nyingi Wanappata Nje ya Nchi lakini Wanawekeza hapa Tanzania mfano kutokana na Uaminifu wao na Kuaminiwa na Watanzania wengi wanakusanya Kontena Nyingi sana kwa Mwezi na kupewa SPECIAL RATES na wenye MELI,Hivyo wanapata Faida kidogo kwa Kila kasha na kwakuwa Mizigo ni Mingi Hutengeneza Faida kubwa(NJE YA NCHI)
Wanatoa Misaada Mingi kwa Jamii Kuliko hao Wafanyabiashara Matycoon Wanaofyonza Nchi kwa Mabilioni na mmekaa Kuwatukuza,Maskini vijana hawa Wanashambuliwa ajili ya Mafanikio yao ya Muda mfupi,Tufanye Kazi na Kuacha Majungu

Ndo hao sasa doc.za container la nguo zimeandikwa toilet paper
 
Nchi hii SAMAKI mkubwa humla samaki mdogo....... Hapo kuna masilahi ya VIGOGO !! nawe tafuta kigogo wako mambo yako yaende vizuri... GOOD LUCK.
 
i am curious to know, hivi wewe @Mr Ethos na wewe @kipasta ni mtu mmoja multiple ID's? wote mnamtetea Home Shopping Center, wote mmejiunga JF siku Moja.....is that coincidence? Kama jamaa hawalipi kodi wacha wabanwe, misaada kitu gani mkuu?yaani watuibie matrilion ya pesa halafu waje warudishe vi-million ndo tuwasifu? Kulipa Kodi ni Jambo la kiungwana, walipe kodi, porojo waache.
 
kwa kifup tu hawa jamaa mimi nimefanya nao kaz tangu mwaka 2007 wananisafirishia mizigo yangu toka china na dubai. Ukwel kama alivyosema jamaa mmoja hapo juu ni kwamba kwa kias flan wanawasaidia wtz masikin kupata hela na matajir pia ila njia anazotumia kuwapa utajir ni kwa kukwepa kodi kwa kusaidiana na baadhi ya watumish wa tra wale wakubwa. Wakat huo yeye kwa kuwaweka watu kati huko juu anapiga hela nyingi mno yaan unaibiwa mwenye mzigo na serikali hasa serikal. Conteiner la nguo ni tshsmilion 17 kwa futi 20 lakn yeye anakuambia ni milion 19 au 20 lakn unatolewa on the sport ikifika. So kinachojitokeza serikalin wanabadilisha document wakishirikiana na watu wa tra conteiner la nguo linabadilishwa linakuwa la cement so analipia milion 5 mpaka 7 za juu anawapa kidogo watumish nyingine zake. Huu mchezo ameuanza cku akisaidiwa na zakhia megi kipindi akiwa wazir wa fedha. Walichofanya wamemuuzia riz 0ne hisa so wanaiba hela nyingi ni mungu anajua. Ingawaje ukwel mwingine mchungu ni kwamba kampun yake ndio inasuply karibu mizigo yote kkoo na posta so kumfungia ni kusababisha ombwe la mizigo sokon na pesa kupungua serikaln ushahd ni juz mwakiembe kakamata conteiner zake mia moja leo hii wamezuiliwa kutoa mizigo wk hiz mbili tu tayar imebid wazir wa fedha awaite wafanyabiashara aongee nao tatizo liko wapi. Coz hazina haisomeki. Na kwa kuwatonya nasikia hata mtoto wa mshua wakat anakamatwa china kama ni kweli hawa jamaa ofic yao ya china ndio iliratibu mazungumzo ya kuachiwa kwao.

mwana jamii forums tunashukuru kwa kuwa muwazi kwa nia ya kuweka jambo hili lieleweke kwetu.
Kumbe kuna wizi mkubwa namna hii jamani?. Hivi jamani kweli watu tumewapa dhamana watuongoze wanageuka kula mapato ya wanannchi wa tanzania?

Mimi nasema jamani tumwachie mungu maana kila neno na tendo litaletwa hukumuni
mungu atahukumu sawa sawa na matendo yao
 
Back
Top Bottom