Na huo ndo ukweli, walijipanga wenyewe eti wamyumbishe kwa kumtumia mwendesha kipindi chao waliyemuandaa lakini wapi.......mwamba alikomaa na alikuwa ngangari kweli kweli. Aliwapa ukweli 'live' na umewaingia kweli.
Walipoona jamaa amewafunika kipoints, wakakimbilia jukwaani humu haraka kuanzisha viuzi vye vichwa vikuuubwa vinavyotisha....oh, muliro achanganya habari! Oh, muliro ashindwa --- na ----. Nilipoenda kuangalia Yale mahojiano yake ya dakika kama 28 hivi; naona mwamba kumbe alisimama vema kabisa. Na kwamba kumbe ni nyumbu ndio waliochemka.