Pre GE2025 Hongera January Makamba, Waziri mwenye weledi mkubwa sana kuzungumza na kuongea lugha ya Kiingereza

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
tudai unamfanyia kampeni za nini? kamwambie yeye na upara wake ikulu wataishia kuiskia tu
 
Tumkosoe Makamba tusimkosoe. Sio kwamba nampigia debe kwani Kuna vitu tunapishana lakini ndiyo rais wetu 2030.
2025 atakua waziri mkuu.
Hongera January.
 
Hata hicho kizungu hakijui hata kidogo,huwezi msimamizsha January hata kidogo kwa Polepole kwenye kupanga hoja na kuzungumza hicho kizungu
 
Huyu ni Makamba mwenyewe unajipigia debe! Hatuwezi kuwa na rais wa hovyo hivyo!
 
Tumeshatoka huko Kiingereza tumewaachia akina junior kindergarden watu tunapiga kifaransa,kichina na kiarabu
 
Ushenzi Nyerere aliotuachia, leo kuongea Kiingereza ndo elimu, mjinga wewe, nenda Kenya, ongea unayoisifia huko nisawa na mtoto wa darasa la kwanza...
 
Tanzania hata walevi wakilewa huongea Kiingereza. Kwa hiyo English language is not a big deal.

Ila Januari hana management skills ni FAILURE. Kama angeendelea kuwa Waziri wa NISHATI naamini TANESCO wangekuwa wanaendelea na mgawo.

Uteuzi wa Dotto Biteko umeonyesha ni NAMNA gani Januari Makamba yuko overrated na chawa wake. Otherwise ni kiazi mbatata, bila msaada wa kusukumwa na JK anabaki ni Msambaa wa kawaida kama Wassmbaa wengine wa Mlalo, Soni na Bumbuli
 
Acha utumwa ipende lugha yako mkuu ! Kujuwa kiingereza hata wanao wanaongea hiyo siyo lugha ya kumsifia mtu Zaidi ya utumwa
 
Kwenda kule wewe kujua kingereza huku mtu mpigaji mkubwa ndio itatusaidia nini. Mtu mwenyewe kiitikadi ni kusujudia wazungu na kuwaamini kila aina ya hadaa zao na pia uwezo na maarifa hana. Peleka huko ujinga wako. Wananchi wanataka mtu mwenye ujasiri mzalendo mwenye maono. Umma wa wananchi wanataka kiongozi mtu ndani ya moyo ni mpenda haki na usawa.
 
Huyu ndiye aliyeiua TANESCO. Hafai kabisa kuchaguliwa kuwa kiongozi Mkubwa nchi hii
 

Kingereza pekee hakitusaidii kama nchi.nadhani substance na maadili ndiyo kitu mhimu cha kukiangalia going forward.by the way watu wenye vingereza ngerza vingi siyo watendaji
 
....anayeimudu lugha ya Kiingereza kwa weledi mkubwa
Hivi majuzi Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Alisema baadhi ya matatizo yanayokwamisha maendeleo ya Afrika ni kuwa na "neocolonial civil servants ". Na Mimi kwa mlengo huo huo nasema kuwa Kuna Kila dalili Hata hapa jukwaani tunao baadhi yetu ni "neocolonial JF members".
Huko uraini sina hakika kama wapo pia "neocolonial citizens!"

Kwa nini mnabinya ukubwa wa Tanzania?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…