Mr Q
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 18,046
- 38,598
Endelea kidogo mkuuUchaguzi Mkuu wa 2025 umeisha jana, kimebaki ni matokeo tu ya uchaguzi kutoka
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Endelea kidogo mkuuUchaguzi Mkuu wa 2025 umeisha jana, kimebaki ni matokeo tu ya uchaguzi kutoka
RO ni nini?Pia Diwani Athumani usimsahau naye sasa ni RO!
Kwa 'ubobezi wao' baadhi yao hawa walipaswa kubakia 'potential material' kwenye ngazi za u-RC n.k badala ya baadhi yao wale waliojidhirisha kua ni ni makapuku haswaa .... mfano juha mmoja sasa yuko Dar, na waliomtangulia pale.Nimejaribu tu kuwaza hivi kama kustafu au kutenguliwa kwao kuna leta shida kwa nchi maana yake uadilifu wao ni mdogo sana.
Wanaweza kufanya chochote kibaya hata wakiwa ofisini bado
Trump kura hazikutosha banaNyerere alikuwa kidume. Nakumbuka nikiwa mtoto. Jumbe akatua uwanja wa Musoma. Hata akusalimia kamati ya ulinzi mkoa aliwapungia tu mkono na kuingia garini kuelekea Butiama.
Nakumbuka alionekana mtu mwenye mawazo sana. Muda mwingi alikuwa amejiinamia. Japo na utoto wangu nikajiuliza kwanini huyu amekuja kwa ghafla na dhararu wakati ni Makamu wa Rais na pia Rais wa Zanzibar?
Kikawaida wakati ule kila kiongozi anae fika Musoma. Alipokelewa na chipukizi na kuvishwa skafu pia kukabidhiwa mauwa.
Nikiwa wakati huo miongoni mwa chipukizi wa kudumu kupokea wageni wa kitaifa na kimataifa. Nilisogea karibu na kamati ya ulizi na usalama ili kupata umbea.
Wengi hawakuwa na furaha, nilipata habari kuwa anaweza ondolewa au kuvuliwa Urais. Nilirejea zangu nyumbani. Kilichoendelea Butiama hakikuwa cha kufurahisha. Abdu Jumbe aliondoka kimya kimya. Na kurudi Dar. Na ilitangazwa kuwa si tena Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na wala si Makamu wa Rais. Ndipo Ally Hassan Mwinyi akateuliwa.
Abdu Jumbe akazuiwa asiende popote. Na kubaki Kigamboni.
Nirudi kwenye mada, kiusalama hasa wa Ikulu na usalama wa Rais, si rahisi na si vizuri kubadili mkurugenzi wa usalama wa Taifa kama ilivyo kwa viongozi wa kisiasa.
Mkurugenzi wa Usalama ndiyo mtu wa kwanza wa karibu kabisa na Rais ambaye anajua mengi si tu usalama bali mfumo mzima wa nchi ulivyo na unavyo kwenda.
Mkurugenzi huyu chini yake ana ma RSO na ma DSO na watumishi wengine vificho kibao. Swali je ameimarikaje ktk kujenga mitandao yake kwa hawa walio chini yake?
Mkurugenzi anawatu wake mpaka huko nje ya nchi balozini. Anawatu wake jeshini, polisi, magereza, na ofisi za umma na hata mashirika binafsi.
Mkurugenzi wa Usalama si mtu mdogo. Uwezi fanya mapinduzi ktk nchi bila kushirikisha watu wa usalama na hasa walio Ikulu.
Hivyo Rais awe makini, aisondoe mtu kisa tu kakataa kukubaliana na unachotaka. Viongozi wetu wanajisahau kuwa Usalama hawapo kutekeleza matakwa ya Rais. Bali wapo kwa matakwa ya nchi na raslimali zake. Watakulinda kiongozi wa nchi kwa sababu upo kulinda maliasili za nchi na kutetea maslahi ya Taifa.
Unapokwenda kinyume na maslahi ya Taifa, au kukiuka Katiba. Wanauwezo wa kutumia namna yoyote kukumaliza au kukuondoa madarakani.
Jumbe aliagiza watu wa usalama kwa mamlaka yake. Lakini hao hao ndo walio mnyang'anya passport na kumuweka chini ya ulinzi. Na kuzuiwa kigamboni.
Rais uwezi ukapewa kila kitu cha TISS. Utapewa habari ile wao watakayo amua ujulishwe. Lakini wanapokuchunguza wewe Rais uwezi pewa taarifa zako. Hizo ni zao wao wenyewe.
Trump aliondolewa na haohao watu wa usalama.
Mama Rais wetu, nakuona unavyojimwambafai, ukidhani huko salama saana. Ukidhani waokupa ushauri wanajua kila kitu. Kuwa makini.
Mageuzi uletwa na watu wa chini kabisa hata kama ni wanajeshi uwa si wale wajuu wenye vyeo, bali wa ngazi ya chini. Na hao wakubwa wanapata info zote toka kwa hawa wa nchini.
Utawabadili sana hao wakurungezi wa TISS, ila fahamu humo humo TISS mama umechokwa. Kwanza unaupendeleo. Kuna namna fulani unawatu wako unao wapa kipaumbele. Kuna watu hawafurahii. Usije muondoa mtu amabe alikuwa kesha jenga mifumo yote vizuri, na pengine ndo angekuwa msaada wako mkuu. Unapo mtoa kuna baadhi watabaki na vinyongo na hasa waliokuwa wanamsujudu.
Si kweli kwamba mtu akistaafu au kuachishwa ndo kwaheri hapati info. Ha ha ha! Hawa watu kumbuka wamekaa wakajijenga wanaelewa nini kinaendelea. Uwezi koswa wafuasi.
Magufuli alipomuondoa Kipilimba roho tu iliniuma ghafla. Nikajiuliza huyu alikuwa tayari kesha jenga mizizi. Anae kuja ni mgeni kwenye ofisi. Mpaka aanze kujijenga, lolote au chochote chaweza tokea. Penye mabadiliko ndo mara nyingi kunakuwa na mianya ya chochote. Matokeo uwa ni baadae.
That's The boy wonderHOW TO DEAL WITH A ROGUE & CORRUPT INTELLIGENCE AGENCY
1. A PLAY-BOOK FROM PEOPLES REPUBLIC OF CHINA
Hili linalotokea Tanzania liliwahi kutokea Uchina mwaka 2013 baada ya Raisi Xi Jinping kuchaguliwa kuongoza nchi. Duniani kote walitegemea Bo Xilai ndiyo awe Raisi wa Uchina, maana alikuwa na uzoefu wa ujasusi, diplomasia na alikuwa ndani ya MTANDAO wa Raisi Mstaafu Jiang Zemin ulioitwa The Shanghai Clique. Jiang Zemin na genge lake ndiyo walikuwa wameshika rimoti ya nchi na wao ndiyo walikuwa wanaongoza hata wakati Raisi Hu Jintao yupo madarakani.
Ubaya ni kwamba Bo Xilai katika harakati za kutaka kuwa Raisi alitengeneza maadui wengi sana wakiweme Raisi Hu Jintao, Waziri Mkuu Wen Jibao na Makamu wa Raisi Xi Jinping. Jamaa alikuwa na MTANDAO mkubwa ambao ulishikilia vyombo vya habari, lakini kubwa sana alikuwa analiongoza shirika la kijasusi (Ofice 610) ambalo lilikuwa linadukua mawasiliano ya mahasimu wake akiwemo Raisi Hu Jintao. Kiukweli alichezewa mchezo mbaya baada ya kutambulika kwamba mke wake alikuwa na mahusino ya kimapenzi na Jasusi wa MI6, hivyo akafukuzwa uanachama wa CCP.
Mambo yalivyokuwa magumu kwenye chama, ikabidi CCP wamempe Uraisi Xi Jinping mtu ambaye alikuwa hana makundi. Kumbe bwana genge la Jiang Zemin na Bo Xilai halikuridhika na lilikuwa linapanga UHAINI dhidi ya Xi Jinping. Kule kwenye jimbo la Xinjiang na Tibet kuna maelfu ya wanajeshi na makomandoo ambao wamewekwa kuwadhibiti waislamu. Bahati mbaya mno vile vikosi vilikuwa vinaongozwa na mtu mwingine kutoka MTANDAO (The Shanghai Clique)wa Raisi Mstaafu Jiang Zemin aitwaye Zhou Yongkang.
Bo Xilai na Zhou Yongkang walianza kuviondoa vikosi kwa kisingizio cha mazoezi, huku wakishirikiana na wanajeshi majenerali wakubwa tu. Bahati mbaya waliwahiwa mapema na kuwekwa kizuizini. Baada ya hapo Xi Jinping akavunjilia mbali shirika la kijasusi (Office 610) ambalo lilikuwa ndiyo chombo cha genge la Raisi Mstaafu Jiang Zemin kuongoza serikali na kuwaendesha viongozi wa nchi ili kufanikisha dili zake za kifisadi. Jiang Zemin na familia yake nao waliwekwa kizuizini.
Hivi mpaka kufika mwaka 2016, Xi Jinping alikuwa ameshughulikia maafisa usalama na makada wa CCP waliokuwa ndani ya mtandao wa Raisi Jiang Zemin wasiopungua milioni 4 (4,000,000). Angecheza tu, nakwambia wangemuua na Raisi angekuwa Bo Xilai. Huu ndiyo ukweli mchungu.
==============================================
2. A PLAY-BOOK FROM THE USSR
Kule USSR, baada ya Stalin kuwa Raisi alikuwa shirika la kijasusi (The Cheka) limejaa WAYAHUDI ambao walikuwa wafuasi wa Raisi Vladmir Lenin na Leon Trotsky. Stalin alifahamu fika, kwamba ili aongoze nchi vizuri ni aidha yeye aende, au hili genge liende. Akaanzisha THE PURGES, ambapo alianza kusafisha chama (CCCP), shirika la kijasusi la jeshi (The GRU), shirika la kijasusi la chama (COMINTERN), shirika la kijasusi la mambo ya nje (INO) na shirika la kijasusi la kiraia (The Cheka).
Mashirika yote makubwa ya kijasusi ya USSR yalianzishwa na Wayahudi wakiwemo Leon Trotsky na Felix Dzerzhinsky, ambao hawakuwa wanamkubali kabisa Stalin. Mpaka kufika mwaka 1935, shirika la kijasusi (The Cheka) lilikuwa limepunguzwa maofisa 150000, ambao aidha walipigwa risasi za kichwa au walipelekwa Siberia kwenye Gulag. Baada ya hapa, ndiyo Stalin alianza kuongoza nchi kiurahisi hadi kuifanya USSR liwe taifa lenye nyuklia na kuwabagaza Wajerumani.
Stalin aligundua jambo la msingi kabisa: USITEGEMEE SHIRIKA MOJA LA KIJASUSI NDANI YA NCHI. Baadaye akaamua kuunda mashirika mengi ya kijasusi ambayo yalikuwa yanafanya kazi moja na kushindana. Mwishowe haya mashirika yakaundiwa wizara moja ya uratibu iitwayo, THE KGB, ilhali hata hayashirikiani hata kidogo.
==============================================================
3. A PLAY-BOOK FROM REVOLUTIONARY FRANCE
Kule Ufaransa baada ya mapinduzi ya mwaka 1789, wajamaa walitambua jambo moja muhimu kabisa. Hawawezi kutawala endapo wafuasi (The Royalists) wa Mfalme Louis XVI wangeendelea kuwepo. Kabla ya Vatican kuunda mwaka 1929, Ufaransa ndiyo kilikuwa kitovu cha Ukatoliki duniani. Mapadri ndiyo walitumika kuusaidi ufalme kufanya Ujasusi dhidi ya wanamapinduzi (The Jacobins). Baada ya wanamapinduzi kufahamu hili walifanya jambo rahisi kabisa, nyonga mfalme Louis XVI, pamoja na kubomoa mfumo mzima wa kijasusi wa Kanisa Katoliki.
Maxmiliien Robespierre na wenzake wakaanzisha kamati ya usalama wa nchi (Committee of Public Safety) ambapo walianza kushughulika na wote wanaopinga mapinduzi. Maaskofu wakajichanganya wakaanza kupiga propaganda kupinga mapinduzi, eeh bwana eeh, kumbe walikuwa wanatafutiwa sababu. The Committee of Public Safety ilikamata mapadri zaidi ya 30,000 waliokuwa wanashirikiana na serikali ya kifisadi ya mfalme Louis XVI na kuwapiga risasi au kuwanyonga hadharani (Guillotined) ndani ya siku moja.
Baada ya hapo hata Napoleon Bonaparte anashika madaraka, alikuta hakuna upinzani mkubwa kivile na mifumo yote ya kijasusi ya Mfalme Louis XVI ambayo iliratibiwa na Kanisa Katoliki ilikuwa ishabomolewa. Ndiyo chanzo cha Ufaransa kuwa taifa lenye nguvu Ulaya yote hadi kufika mwaka 1814.
======================================================
4. A PLAY-BOOK FROM THE UNITED STATES OF AMERICA (CIA vs JF. KENNEDY)
Raisi John Kennedy amechukua nchi alikuta kuna mambo hayaelewi kabisa. Tena yeye ndiye Raisi wa kwanza Mkatoliki kuwahi kushika nyadhifa hiyo nchini Marekani. Wakubwa wengi ambao ni Waprotestanti na Walokole walikuwa hawamtaki kabisa. Ile ameingia madarakani, amemkuta Allen Dulles kama Mkurugenzi wa CIA ambaye amekaa kwenye nafasi hiyo siyo chini ya miaka 9. Huyo Dulles familia yake ilikuwa kubwa nchini Marekani, wakati yeye ni Mkurugenzi wa CIA, kaka yake John Foster Dulles alikuwa ni Secretary of State. Alianza kipindi cha Eisenhower hivyo Kennedy alimkuta tu.
Mwaka 1961, Raisi Kennedy anapigiwa simu na Mkatoliki mwenzake, Raisi wa Ufaransa Charles De Gaulle na kuulizwa kwanini CIA inaivuruga Ufaransa hasahasa kusababisha vurugu kwenye makoloni yake kama Algeria. Raisi Kennedy anashangaa kwasababu hakutoa amri ifanyike oparesheni yoyote ile. Kumbe CIA na Allen Dulles wanajifanyia mambo wanayotaka huku wakijinufaisha binafsi bila serikali ya Marekani kujua. Wanaua watu, wanapindua viongozi wa nchi na kuteka wakisingizia kupambana na ukomunisti, kumbe dili zote za uwekezaji ni zinazofanikishwa na CIA kwenye nchi za watu ni mali ya matajiri akiwemo Allen Dulles.
Mwaka 1961, JF Kennedy alimfukuza kazi Allen Dulles na kusema hivi "I will splinter the CIA into athousand pieces." Alitaka kuivunja CIA na kuisuka upya na kuwashughulikia mafisadi. Kumbe kauli hii iliwaudhi wakubwa, miungu watu kama Allen Dulles na wenzake akina Edgar J Hoover. Bahati mbaya JF Kennedy hakufahamu, jinsi gani CIA inaendeshwa. Allen Dulles alijifanya amestaafu na kwenda kukaa kwenye nyumba yake nje ya Virginia, kumbe ile siyo nyumba binafsi, ila CIA BASE OF FOR CLANDESTINE/COVERT OPERATIONS. Bado Dulles akawa anaendesha CIA kwa mlango wa nyuma.
Wakamvutia kasi Kennedy, siku ameingia kwenye kumi na nane zao, wakamtafuta muhitimu wa MK-ULTRA bwana Lee Harvey Oswald afanye yake na kumuua Kennedy. Haikuishia hapo, waliua hadi ndugu na jamaa wa karibu wa Kennedy kimya kimya. Baada ya Kennedy kufariki bunge la Marekani likaunda tume ya uchunguzi, bahati mbaya mwenyekiti akawa ni mkurugenzi mstaafu wa CIA, Allen Dulles ambaye alisema kwamba aliyemuua Kennedy alikuwa anaumwa kichaa. Ndiyo nitolee hivyo, wao wakapona. Allen Dulles alinukuliwa akisema, "That man Kennedy, thought he was a god."
JF Kennedy angefanya kama alivyofanya Abraham Lincoln huenda angemaliza muda wake vizuri tu. Wakina Jeff Davis walitoa majeshi na kutaka kumtishia Abraham Lincoln, kilichofuatia yeye akapeleka majeshi na kuwatandika kweli majimbo ya Kusini hadi wakatia adabu. Walikufa watu wengi lakini Lincoln alinukuliwa akisema hivi " I will bring respect to the Union " Angecheka tu ula mwaka 1861 Marekani ingekuwa ishagawanyika vipande viwili na ingefutika kwenye uso wa dunia.
Hata Raisi Andrew Jackson alipopinga kutaka kuanzishwa kwa The Federal Reserve, walitaka kumuua ila wakashindwa. Kilichofuata ni kwamba aliwanyoosha kweli vibaraka wa matajiri wakubwa hadi wakakimbia nchi na kutupilia mbali kabisa mpango wa kuanzisha The Federal Reserve.
==========================================================
Uziri hapa Tanzania NYOKA wanafahamika, tena tunaishi nao kabisa. JOHN wetu aliwachekea akidhani angeweza kulala kitanda kimoja na nyoka halafu yasimkute. Alidanganywa kwamba wanamuogopa na hawawezi kumgusa tena. Akaanza kuwaiga kuchota mapesa, akawajengea nyumba na kuwapa hadi Ubunge kumbe wenyewe wanasubiri ajae kwenye 18. Haya kiko wapi sasa, ???
Binafsi huwa nampenda sana General Paul Kagame, ukiwa ndani ya Rwanda ukajifanya unaleta fyoko-fyoko yaani itakula kwako. Hata uwe Raisi Mstaafu, Jenerali Mstaafi au Afisa Usalama Mstaafu, lazima ile kwako. Huwa natamani Tanzania ipate mtu wa aina ya PAUL KAGAME walau miaka 7 tu, hawa machekibobu waliopo TISS, PCCB, TPDF, PT, BOT, FOREIGN AFFAIRS ambao wameenda kwa vimemo na mbeleko za wazazi halafu wanatuletea ujinga wa DP WORLD, tungekuwa tunawakuta gerezani au tunawaokota kule mabwepande kila siku.
Leo mijitu inaingea udini na ukabila hadharani halafu inaachwa tu, mingine inaiba hela na kuhonga mahawala V8 halafu inapewa kabisa uwaziri. Sehemu kama Marekani, Uchina, Uingereza na Urusi huwezi kufanya mambo kama haya halafu ukaachwa tu. Binafsi huwa nawatamani mno watanzania, nasomaga comments hapa jukwaani halafu nasema, Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, I WISH I KUDU BE THE PRESIDENT, kuna watu wangepata shida mnoo.
Watanzania hawajawahi kukutwa ndiyo maana linchi halina adabu kabisa. Ila ipo siku tu...
Nilijuwa tu lzm uje na LinkThanks for this, nimemkumbuka Hutaki Unaacha!. Siku za nyuma niliwahi kuuliza Wimbi la maofisa Polisi, Jeshi na Usalama wa Taifa, kustaafu kwa mpigo, sio tishio kwa usalama?
RO yupo, Jack Zoka yupo, Kipilimba yupo, it's very true hawa jamaa wanakuwa wengi!.
P
Wamasai wakomae nae wasiondoke! Hawa watu gani wanawatoa wananchi sehemu ya jadi yao kwasababu wajomba wa Samia wanalitaka hilo eneo!Hawa uliowataja ni panya road wa mtandaoni. Hapa nimepata jambo moja. Loliondo tatizo lake ni Samia akiwakingia kifua wajomba zake.
Naandika andiko hili nikiwa ndani ya Ofisi yangu ya mpya ya Centre for Strategic Intelligence and Clandestine Operation hapa ndani ya kijiji chetu hiki kdogo.
Rais wangu Samia Suluhu, najua kazi ya Urais ni Ngumu Sana, ila TRUST me kwamba ni kazi rahisi sana. Tatizo wanoko ni wengi na wanaoitaka pia ni wengi.
Hata hivyo leo sizungmzii cheo chako cha URAIS bali nazungumzia Uteuzi wako wa Mkurugenzi wa TISS. Kwa uelewa na uzoefu wangu. TISS ni kama Serikali ndani ya serikali. Kwa lugha nyingine Unapoteua Mkurugenzi wa TISS ni sawa na Umeteua Alternative Preseident au Rais mbadala kwani nyenzo alizo nazo ni sawa na nyenzo ulizo nazo isipokuwa yeye anakuwa hana Political Accoutability na wakti huo huo anakuwa na njia za kutengeneza Mazingira ya Plausible Deniability.
Sasa hili ni somo ambalo unahitaji muda na utulivu ili ulielewe. Ila nataka ufahamu kwamba Mkurugenzi wa TISS kwa chini huwa anakuwa na mamlaka sawa na uliyo nayo wewe. Kama ambavyo wewe unaweza kumtengua wakati wowote basi hata yeye ana uwezo na resources za kufanya hivyo.
Sasa nimesikia umetengua na kuteua mwingine. Unachosahau ni kwamba "Once a spy, always a spy"Ukishateua Mkuu wa TISS anapata clearance kubwa sana katika masuala ya taarifa na usalama wa nchi. Anakuwa na access ya resources zote za nchi. Zaidi mwaka huu mmewatungia sheria ya kuwapa kinga ya kutowajibika kisheria which means matendo yao hata kama yatakuwa ya kihalifu bado wanaweza kuepuka wajibikaji wa kisheria.
Sasa iko hivi, kwa sasa TISS ina spy masters watatu ambao wako around na wako nje na ndani ya Mfumo, Kipilimba, Diwani, na Masoro na sasa huyu bwana Siwa.
Iko hivi hawa wote ni Spy masters whether wako nje au ndani ya mfumo.
Ndio maana unapowatoa uhakikishe kwamba unaweza kuundoa Uspy master wao na hilo unajua kwamba huwezi.
Ndio maana huwa unapotaka kumtoa usimtoe kwasababu ya Makosa ya kiusalama au kwa sababu ya umbea au kwa sababu ya kukosa uvumilivu.
Spy masters hawajibishwi kama anavyo wajibishwa waziri au DC,Spy Craft ni mchezo tofauti sana.Ukitaka kufahamu hilo JIULIZE kilichofanya Imran Kombe akauwawa kama JAMBAZI ilihali wengine waliowahi kuwa wakuu wa kitengo waliendelea kuwepo ingawa baada ya wao na kujaribu ku activate mitandao yao walipigwa na kitu kizito.
Sasa umeteua DG mpya ambaye bila shaka unalo file lake na huenda linakuvutia hasa ukizngatia kwamba alishakaa kwa PAKA so anaweza kuwa na ka cv kazuri ila TRUST me huenda kwenye MEZA yako kuna mafili ambayo bado hujayasoma na kuyapitia vizuri na ukija kuyafikia unaweza kushawishika kufanya uteuzi mwingine tena ambalo nalo litakiwa kosa la KIMKAKATI.
Hawa jamaa wote wanaweza wa "Kagang UP" against you na hakuna unachoweza kufanya kwa sababa wanayo access ya taarifa na resources ambazo ww unajua uwezo wake.
Sasa lengo sio kuleta hofu bali kuchokoza mjadala tu kuhusu tatizo lililoko katika IDARA yetu ya USALAMA wa TAIFA.
Ila uelewe vizuri nitakukumbusha hadithi ya bwana Mdogo Ole Sabaya ambaye aliwahi hata kufoji kitambulisho ka cha TISS na kujiita Afisa Kipenyo wakati akiwa mwenyekiti wa UVCCM Arusha na wapo wengi kama yeye, So unapobadili Wakurugenzi Jiulize iwapo Tatizo ni TISS au ni Wakurgenzi wa TISS?
Madam President, Fahamu kwamba TISS sio CID wala sio Military Intelligence UNIT ingawa kimajukumu, TISS anaweza kuingia katika hayo maeneo yote ila sio CID wal MIU wanaweza kuingia katika maeneo ya TISS so ni muhimu tukajiuliza iwapo TISS imevamiwa na KIRUSI na inahitaji kupigwa Immune Booster nani ataipiga immune booster?
Kuna kipindi mm binafsi niliona au kuhisi kwamba Utawala wako uliamua kutumia JU(Jeshi la kupambana na Ujangili kama TISS mpya so nikafikiri umegundua TATIZO na unalitafutia Suluhu kama Ulivyo wewe.
Tatizo kwa sisi wenye macho ya Rohoni tuliingia katika Sala, maombi na kufunga na tukagundua kwamba kulikuwa tu na mambo fulani ya wajomba zako ulikuwa unawatumia jamaa wa juu kuyaweka Sawa. Anyway hiyo issue kila mtu atakuwa ameshaijua hasa tukisikia stori za Loliondo
Sasa fahamu hili, huwezi kupata TISS bora kwa kutumia TISS katika muundo na utaratibu wake wa Sasa. TISS ambayo ilifanya kazi enzi za Mwalimu sio Sawa na TISS ambayo inafanya kazi enzi hizi. Imagine mimi hapa nilipo nawez kuona patern of errors unazofanya bila hata kuwa na taarifa za jikoni unadhani hao ambao wana access ya taarifa za jikoni wanaona nini kama sio zaidi ya haya.
Sasa nataka ujilulize. Je unafikiri TISS ni kama wizara ambapo unaweza kubadili katibu mkuu na kazi ikaendelea? Hapana.SPIES are trained not TRUST.
So kadiri unavyoleta na kubadili wakuu wa TISS ndivyo idadi ya MOLES inaongezeka ndani ya IDARA na Badala ya kuwa idara ya Usalama wa Taifa na inakuwa ni Idara ya Kupika Majungu, vijembe, fitna na kukomoana. TRUST me ikiendelea kuwa hivyo hata wewe utapewa Majungu, utapigwa vijembe utafanyiwa Fitna na hata kukomolewa mwishoni Utakumbuka Kamsemo "WHo will Watch the Watchers"
Nimechokoza mjadili, hayo mengine sijui kama ni ya kweli niko hapa pembeni ninaendelea kupata Madini wala sijajificha.
Moyo wa nchi unapitia magumu mengi. Idara haijawahi kufanyiwa mabadiliko ya kiwango hiki. Tumuombee mzee Siwa airudishe nchi kwenye mstari. Hawa wazee wanaweza kumsaidia mama, let's hope tunaweza kuanza kuona mabadiliko
Mada kama hizi wanakuja kuchangia akina mwijaku na kitenge what do you expect??
Huu uzi ulindwe usije kuvamiwa na Chawa
Na Steve Nyerere.Mada kama hizi wanakuja kuchangia akina mwijaku na kitenge what do you expect??
Samia tunae kwa mipango ya mungu hadi 2030...Hivi ni lazma Samia awe Rais? Mbona Abudu Jumbe alitolewa
msomi kama nani sasa,mwabukusi au?Uko mbele hizi nafasi 2 za juu wakae wasomi kwa kweli. Namba 1 sidhani kama anaelewa lolote pale juu kiukweli. Yeye ni kuwa briefed tu.
Wahuni tu hao,hawana lolote.Duh
Ngoja waje Pascal Mayalla na Yericko Nyerere
[emoji23][emoji23] witoMa DGIS wote wakitenguliwa hupostiwa nje ya nchi, ubalozini, wakistaafu ndipo hurejea nyumbani kuishi under supervision kusubiria kuitika ule wito, na kusibdikizwa kwa heshima zote.
P