Hongera na pongezi kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kuifanya Tanzania kuwa Salama muda wote

Hongera na pongezi kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kuifanya Tanzania kuwa Salama muda wote

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Ni wachache wenye kuona na kutambua kazi kubwa inayofanywa na hivi vyombo vyetu katika kuilinda na kuipigania nchi yetu usiku na mchana na hatimaye kufanya watanzania tuishi kwa amani bila hofu Wala mashaka

Msingi wa maendeleo katika nchi yoyote Ile Ni uwepo wa amani na utulivu, msingi wa watu kufanya kazi za kimaendeleo ni uwepo wa usalama katika nchi, msingi wa kushamiri kwa biashara na wafanyabiashara Ni usalama katika nchi, chambo kuu ya kuwavuta wawekezaji au watalii au wafanyabiashara wakubwa toka mataifa mbalimbali ni uwepo wa usalama madhubuti ndani ya nchi

Tanzania imeendelea kuwa kisiwa Cha Amani kwa kuwa Asikari wetu wanapambana muda wote kuzuia uhalifu na kuwakamata wahalifu, Ndio maana Inafika hatua watu wanashangaa inakuwaje kwa wakati mmoja viongozi wakubwa wa juu wawili au wote watatu hawapo nchini? Wanauliza haya kwa kuwa wanajuwa kwa nchi za wenzetu hasa Afrika Jambo Hilo Ni gumu, kwetu linawezekana kwa kuwa tunavyombo imara na madhubuti Sanaaaa vilivyojidhatiti kulinda na kuipigania nchi yetu

Rai yangu kwa vyombo vyetu Ni kuwa natambua kazi ya ulinzi ilivyo ngumu kwa kuwa baba yangu amewahi kuwa mwanajeshi aliyepigana Vita vya Tanzania na Uganda 1978-1979 Tena akiwa mstari wa mbele kabisa na kufanikiwa kukanyaga Aridhi ya Uganda na kurudi mzima Hadi Leo Ni mzima pia, Na hata matunda yake yapo mpaka Sasa maana aliporejea alipewa ardhi kubwa Sana na serikali ya Kijiji Kama zawadi ambayo imenisaidia katika kusoma, Ndio maana naipenda nchi yangu na kuwa mzalendo kwa kuwa Baba yangu alitoa jasho kuilinda na kuipigania Tanzania hii

Hivyo nawaomba Asikari na wanajeshi wetu Kuendelea na moyo huo wa uzalendo kwa nchi yetu Katika kuilinda na kuipigania. msikatishwe Tamaa na maneno ya wachache wanaokuwa wanaongeaa maneno ya kuwakatisha Tamaa, Msijari maneno yao, piganieni Taifa letu, ilindeni mipaka yetu kwa nguvu zenu zote, mamilioni ya watanzania Tupo nanyi na tunawaombea ili Mwenyezi Mungu awalinde muwapo katika majukumu yenu

Tangulizeni moyo wa uzalendo hata pale inapotokea Kuna baadhi ya madai au Mahitaji hamja pewa kwa wakati ,Nawaombeni muwe na Subira uvumilivu utiifu na moyo wa Kuendelea kuilinda nchi yetu kwa uzalendo kwa kuwa serikali yetu imeonyesha muda wote kuwajari na kuwasikiliza, mlipo na malalamiko Tumieni njia nzuri na za kizalendo kufikisha madai yenu

Ushauri kwa Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia Namuomba aendelee kuwajari na kuwaongezea bajeti kila Hali ya uchumi inaporuhusu ili waweze kufanya kazi kwa urahisi hasa kwa kuwa na vitendea kazi Bora na vya kisasa zaidi, lakini pia kuwapa faraja na kuwatia moyo wakati wote,

Kazi iendeleee,Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais wetu,Mungu vibariki vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, Mungu Tubariki watanzania na utusamehe pale miongoni mwetu wanapotokea kukufuru na kukukosea, usituadhibu wote Kama Taifa, Tunaomba utuhurumie na utusamehe,

Lucas Mwashambwa ,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti
 
Kumbe Tanzania iko vitani, hao askari wetu wanaopambana muda wote wanapigana na wakina nani? au ndio panyarodi? lakini sioni kama panyarodi wanahatarisha usalama wa mipaka yetu.

Wacha kudanganya watu, amani yetu inasababishwa na ukondoo wetu, hata tukiwekwa kidole jichoni, sisi tutalia, tukinyamaza tunaenda nyumbani kulala.
 
Kumbe Tanzania iko vitani, hao askari wetu wanaopambana muda wote wanapigana na wakina nani? au ndio panyarodi? lakini sioni kama panyarodi wanahatarisha usalama wa mipaka yetu.

Wacha kudanganya watu, amani yetu inasababishwa na ukondoo wetu, hata tukiwekwa kidole jichoni, sisi tutalia, tukinyamaza tunaenda nyumbani kulala.
unataka ukiwa umelala na kujifunika mablanketi yako uje uamushwe kwamba twende huku tukapambane na majambazi? Unazani Kama siyo kazi kubwa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ungepata muda wa kuja kuandika hayo madudu yako Hapa?
 
Umeshaanza kiherehere na kisebengo chako.
Unazani Kama siyo kazi ya Askari na wanajeshi wetu kufanya kazi ya kizalendo usiku na mchana ungepata nafasi ya kuja kuandika madudu yako Hapa? Muda huu ungekuwa unakimbia Hadi unasahau watoto wako nyuma na kubeba mbuzi mgongoni ukizani Ni watoto ili utafute chombo la kujificha
 
Unazani Kama siyo kazi ya Askari na wanajeshi wetu kufanya kazi ya kizalendo usiku na mchana ungepata nafasi ya kuja kuandika madudu yako Hapa? Muda huu ungekuwa unakimbia Hadi unasahau watoto wako nyuma na kubeba mbuzi mgongoni ukizani Ni watoto ili utafute chombo la kujificha
Tatizo lipo kwako.Umeshindwa kulea kwa maadili watoto wako wakakukimbia na kuja mjini.Polisi wanawatandika risasi,unakenua manjino tu.Kwanza ulienda kumzika ndugu yako aliyechinjwa?Au huna nauli kazi kusifusifu wenzako tu?
 
Tatizo lipo kwako.Umeshindwa kulea kwa maadili watoto wako wakakukimbia na kuja mjini.Polisi wanawatandika risasi,unakenua manjino tu.Kwanza ulienda kumzika ndugu yako aliyechinjwa?Au huna nauli kazi kusifusifu wenzako tu?
Kweli wewe haupo sawa maana ulichoandika sizani hata Kama na wewe unakielewa na maana umejibu Ni Kama mtoto mdogo anayeulizwa hiki halafu yeye anajibu kingine
 
Kweli wewe haupo sawa maana ulichoandika sizani hata Kama na wewe unakielewa na maana umejibu Ni Kama mtoto mdogo anayeulizwa hiki halafu yeye anajibu kingine
Sasa,hapo ndiyo umejibu swali?Acha ushankupe wa kila dakika kusifia wanaume.Kwani tangu uzaliwe haujawahi kuwaona?
 
Kwanini nisiwapongeze? Kwani huko Congo wanakoishi kwa hofu unazani Hakuna Asikari na wanajeshi? Sasa wewe kwa akili yako huoni Hawa wa kwetu wanastahili kupongezwa kwa kudumisha amani? Bila Shaka wewe Ni mmoja wapo wa wale wanaotamani kuona nchi yetu inaingia kwenye machafuko lakini kwa bahati mbaya mmekosa mwanya huo baada ya kuwa mmedhibitiwa kikamilifu na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama
Sasa,hapo ndiyo umejibu swali?Acha ushankupe wa kila dakika kusifia wanaume.Kwani tangu uzaliwe haujawahi kuwaona?
 
Kwanini nisiwapongeze? Kwani huko Congo wanakoishi kwa hofu unazani Hakuna Asikari na wanajeshi? Sasa wewe kwa akili yako huoni Hawa wa kwetu wanastahili kupongezwa kwa kudumisha amani? Bila Shaka wewe Ni mmoja wapo wa wale wanaotamani kuona nchi yetu inaingia kwenye machafuko lakini kwa bahati mbaya mmekosa mwanya huo baada ya kuwa mmedhibitiwa kikamilifu na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama
Endelea kujipendekeza.Utafikiriwa kupewa nafasi ugombee uenyekiti wa kitongoji.
 
Kumbe Tanzania iko vitani, hao askari wetu wanaopambana muda wote wanapigana na wakina nani? au ndio panyarodi? lakini sioni kama panyarodi wanahatarisha usalama wa mipaka yetu.

Wacha kudanganya watu, amani yetu inasababishwa na ukondoo wetu, hata tukiwekwa kidole jichoni, sisi tutalia, tukinyamaza tunaenda nyumbani kulala.
Acha ufala kubwa zima hovyo
 
Endelea kujipendekeza.Utafikiriwa kupewa nafasi ugombee uenyekiti wa kitongoji.
Kuwa mzalendo kwa nchi yetu, haya yote tuyafanyayo hapa kwa amani na utulivu wa kuandika Ni matunda ya kazi kubwa ya kutukuka inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika kuilinda nchi yetu na kuhakikisha ipo salama muda wote kwa uweza wa Mwenyezi Mungu anayetoa maarifa na njia
 
Najaribu kukuwazia tu
JamiiForums915735144.jpg
 
Ndugu zangu Ni wachache wenye kuona na kutambua kazi kubwa inayofanywa na hivi vyombo vyetu katika kuilinda na kuipigania nchi yetu usiku na mchana na hatimaye kufanya watanzania tuishi kwa amani bila hofu Wala mashaka

Msingi wa maendeleo katika nchi yoyote Ile Ni uwepo wa amani na utulivu, msingi wa watu kufanya kazi za kimaendeleo ni uwepo wa usalama katika nchi, msingi wa kushamiri kwa biashara na wafanyabiashara Ni usalama katika nchi, chambo kuu ya kuwavuta wawekezaji au watalii au wafanyabiashara wakubwa toka mataifa mbalimbali ni uwepo wa usalama madhubuti ndani ya nchi

Tanzania imeendelea kuwa kisiwa Cha Amani kwa kuwa Asikari wetu wanapambana muda wote kuzuia uhalifu na kuwakamata wahalifu, Ndio maana Inafika hatua watu wanashangaa inakuwaje kwa wakati mmoja viongozi wakubwa wa juu wawili au wote watatu hawapo nchini? Wanauliza haya kwa kuwa wanajuwa kwa nchi za wenzetu hasa Afrika Jambo Hilo Ni gumu, kwetu linawezekana kwa kuwa tunavyombo imara na madhubuti Sanaaaa vilivyojidhatiti kulinda na kuipigania nchi yetu

Rai yangu kwa vyombo vyetu Ni kuwa natambua kazi ya ulinzi ilivyo ngumu kwa kuwa baba yangu amewahi kuwa mwanajeshi aliyepigana Vita vya Tanzania na Uganda 1978-1979 Tena akiwa mstari wa mbele kabisa na kufanikiwa kukanyaga Aridhi ya Uganda na kurudi mzima Hadi Leo Ni mzima pia, Na hata matunda yake yapo mpaka Sasa maana aliporejea alipewa ardhi kubwa Sana na serikali ya Kijiji Kama zawadi ambayo imenisaidia katika kusoma, Ndio maana naipenda nchi yangu na kuwa mzalendo kwa kuwa Baba yangu alitoa jasho kuilinda na kuipigania Tanzania hii

Hivyo nawaomba Asikari na wanajeshi wetu Kuendelea na moyo huo wa uzalendo kwa nchi yetu Katika kuilinda na kuipigania. msikatishwe Tamaa na maneno ya wachache wanaokuwa wanaongeaa maneno ya kuwakatisha Tamaa, Msijari maneno yao, piganieni Taifa letu, ilindeni mipaka yetu kwa nguvu zenu zote, mamilioni ya watanzania Tupo nanyi na tunawaombea ili Mwenyezi Mungu awalinde muwapo katika majukumu yenu

Tangulizeni moyo wa uzalendo hata pale inapotokea Kuna baadhi ya madai au Mahitaji hamja pewa kwa wakati ,Nawaombeni muwe na Subira uvumilivu utiifu na moyo wa Kuendelea kuilinda nchi yetu kwa uzalendo kwa kuwa serikali yetu imeonyesha muda wote kuwajari na kuwasikiliza, mlipo na malalamiko Tumieni njia nzuri na za kizalendo kufikisha madai yenu

Ushauri kwa Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia Namuomba aendelee kuwajari na kuwaongezea bajeti kila Hali ya uchumi inaporuhusu ili waweze kufanya kazi kwa urahisi hasa kwa kuwa na vitendea kazi Bora na vya kisasa zaidi, lakini pia kuwapa faraja na kuwatia moyo wakati wote,

Kazi iendeleee,Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais wetu,Mungu vibariki vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, Mungu Tubariki watanzania na utusamehe pale miongoni mwetu wanapotokea kukufuru na kukukosea, usituadhibu wote Kama Taifa, Tunaomba utuhurumie na utusamehe,

Lucas Mwashambwa ,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti
Maneno mazito haya!
Kuna watu hawajawahi ktoka nje ya nchi, na umoja wetu, amani na usalama wa raia wanuchukulia poa tu.
Kuna wenzetu inabidi wawe nyumbani kabla giza halijaingia.
 
Kuwa mzalendo kwa nchi yetu, haya yote tuyafanyayo hapa kwa amani na utulivu wa kuandika Ni matunda ya kazi kubwa ya kutukuka inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika kuilinda nchi yetu na kuhakikisha ipo salama muda wote kwa uweza wa Mwenyezi Mungu anayetoa maarifa na njia
Hivi,huwa huwezi kujibu kitu kwa ufupi?Maelezo mengi utadhani unapiga debe stendi ya daladala!
 
Unazani Kama siyo kazi ya Askari na wanajeshi wetu kufanya kazi ya kizalendo usiku na mchana ungepata nafasi ya kuja kuandika madudu yako Hapa? Muda huu ungekuwa unakimbia Hadi unasahau watoto wako nyuma na kubeba mbuzi mgongoni ukizani Ni watoto ili utafute chombo la kujificha
Ile ni ajira kama ajira zingine, ndio maana kuna daktari anakubadilishia figo ili usife; kuna walimu n.k
 
Mpaka kufika leo hii katika kuumaliza mwaka watanzania Tuna kila sababu ya kuvipongeza vyombo vyetu vya Ulinzi na usalama kwa namna vilivyo Imarisha ulinzi pamoja na kudhibiti matukio ya uhalifu na ujambazi , lakini pia kupunguza ajali za Barabarani zilizokuwa zinachukua maisha ya watanzania wengi.

Hongera Sana kwa ushupavu wa Askari wetu wanaonesha wakitulinda watanzania na kulipigania Taifa letu kwa jasho na Damu kuhakikisha kuwa linaendelea kuwa lenye utulivu na Amani pasipo kutoa mwanya kwa adui kuweza kujipenyeza nchini mwetu
 
Ile ni ajira kama ajira zingine, ndio maana kuna daktari anakubadilishia figo ili usife; kuna walimu n.k
Wewe unafikiri Kuna mshahara unaoweza kumlipa mtu aliyejitoa na kujitolea kufa na kumwaga damu take kwa ajili yetu watanzania? Kiasi gani Cha Mshahara chenye kulingana na Thamani ya mtu aliyeamua kwa uzalendo Wake kukesha usiku mzima akipambana na majambazi yenye silaha za Moto? Tuwe wazalendo na tuviheshimu vyombo vyetu vya Ulinzi na usalama
 
Back
Top Bottom