Hongera Rais Magufuli kuipendezesha Ikulu yetu kuliko enzi za Nyerere, Ikulu iwe kivutio cha utalii, restrictions ziondolewe watalii wafurike

Pamoja na kupendezesha Ikulu kwa wanyama pori lakini kuna mambo mengine ya kuangaliwa mfano wanyama hawa wanatoa uchafu kwa maana nyingine wanakunya hovyo sasa kwa Ikulu tunavyofahamu ni mahala panapotakiwa kuwa na usafi wa hali ya juu, Je hili suala litasimamiwa vipi?

Pili wanyama hawa wanahitaji majani mengi sana kwa ajili ya chakula chao nina wasiwasi na majani yaliyopo ndani ya Ikulu kama yatatosha.

Nimewaona wanyama wengi pale Ikulu kama pundamilia, swala, ngedere nk. Kwa ushauri wangu kuwa angalau tungekuwa na wanyama wachache angalau hata watano ili kuwaonyesha watu kuwa Tanzania tuna fursa ya utalii kuliko kuweka wanyama wengi pale Ikulu na matokeo ni kuharibu mazingira.
 
Nyerere hawezi kulinganishwa na Rais yoyote, ni sawasawa na kumlinganisha baba yako mzazi na baba mwingine na kuanza kumsifia kuwa yeye ni bora zaidi. Na ndo maana kila kiongozi anafanya reference kwa Nyerere maana yeye ndio Benchmark
 
Mbona Magufuli ndio kinara wa kuuza nyumba za umma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ikulu inahamia dodoma, why hawajapelekwa Dodoma ili wazoee mazingira?
 
Pasiko, umeandika vizuri sana na sifa stahili ila tu hapo kwenye kusafiri kwenda nje ndipo umeharibu kila kitu, akajifunze nini kwa mabeberu kwanini wao wasije huku kujifunza ukizingatia hawana wanyama.
 

!
Hivi pale nii Dodoma au Dar! Samahani lakini
 
Mfute kabisa huyo namba moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mawazo mazuri, ila sioni kama kuna haja ya yeye kwenda huko ulaya physically kuona mambo yakoje, siku hizi technology iko juu sana, kwa nafasi yake kama raisi sidhani kama anashindwa kuona live videos zinazoonyesha ikulu ya SA au USA akiwa nyumbani kwake kinyume na kuwa akienda itagharimu pesa nyingi, na afterall kama ni swala la exposure anayo kubwa kiasi cha kutosha sana, tukumbuke kabla ya kuwa raisi ameshakuwa waziri kwa muda mrefu sana na ukumbuke kipindi chao cha uwaziri kwenda ulaya ilikuwa ni kama kumsukuma mlevi, kwahiyo cha muhimu ni kuzidi tu kumuombea heri raisi wetu ili nchi izidi kusonga mbele na mikakati yake ya kuipaisha nchi yetu...
 
Inahitaji "AKILI KUBWA" kuelewa post za Mayala. Msome vizuri na ujipe muda wa kutafakari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Pongezi kwa mweshimiwa kwakuipendezesha ikulu kwa zoo..lakn pendekezo la yeye kutawala mpaka mungu atakapo amua..nipo kuenda kinyume kabisa na katiba raisi ana ukomo wa madaraka..hata awe mzuri namna gani lazima katiba iheshimiwe...kipindi cha JK watu walilia aendelee lakn katiba ilieshiwa...na ndo maana kwenye viapo vya kuhudumia uma lazima wahusika waape kuitunza na kuilinda katiba yetu and not otherwise..

Kuhusu DSM RC kwenda US...labda abebwe kama kwenye mikoba kama docs...personaly hawezi kuingia..na kama wakienda nae kilazima au kwa kificho our relatioship with US will be over...

Tupunguze sifa za kijinga...am out..
 
Nimepitia comments nyingi nikagundua wengi humu JF hawajawahi kumuelewa Mayala. Kuna haja ya kunoa bongo zenu na mrudi kupitia upya nyuzi zake.

Mayala ana akili kubwa kuliko wengi wenu, anang'ata mara tatu na kupuliza mara moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…