Hongera Rais Samia kilo 1 ya Korosho yafika shilingi 4120

Hongera Rais Samia kilo 1 ya Korosho yafika shilingi 4120

Lione hili Kwahiyo korosho za samia? wakulima waliotoa jasho lao kuzilima huwajui?
Tehe tehe tehe teheeeeee! Chadema hawaamini kama wamepigwa kanzu, kidali na tobo kabisa!! Poleni, siku nyingine muwe na adabu na watu wanaotunukiwa u-dr
 
Lione hili Kwahiyo korosho za samia? wakulima waliotoa jasho lao kuzilima huwajui?
Hata wewe wa Samia.
. Au una Rais mwengine Tanzania?

Wakulima wa korosho wa mama Samia wanafaidika kwa bei nzuri mwaka huu.
 
Hakikisha 2025 kura yako inaenda kwa Samia
1000012674.jpg
 
SAafi sasa wananchi wafanye uwekezaji mzuri, mkoa unyanyuke kiuchumi
 
Una Rais wako mwengine Tanzania hii, ukipenda usipenda wewe Rais wako ni mama Samia Suluhu Hassan.

Au kuna kondoo mwenzako Rais?
 
Una Rais wako mwengine Tanzania hii, ukipenda usipenda wewe Rais wako ni mama Samia Suluhu Hassan.

Au kuna kondoo mwenzako Rais?
 
Wakazi wa Mkoa wa Mtwara wanasherehekea kwa furaha kubwa hatua ya kihistoria ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kupandisha bei ya korosho hadi shilingi 4,120 kwa kilo.

Haya sio tu mabadiliko ya bei, bali ni ushahidi wa dhamira ya Rais Samia ya kuwainua wakulima na kuleta mabadiliko chanya katika maisha yao.

Wakulima wanasherehekea kwa kusema, “Mama Samia ni rafiki wa wakulima, ni kiongozi anayejali!”

Katika sanduku la kura, wakulima hawawezi kuficha shukrani zao, wakitangaza kwa sauti moja: “Tutampa Mama Samia VEMA, TIKI ni ndogo mno, haimtoshi kwa wema aliotutendea Mtwara.”

Hii inadhihirisha jinsi Rais Samia alivyoweza kuungana na wakulima, kuleta matumaini na mabadiliko ya kweli katika kilimo chao.

Wakulima wanasema kwa ujasiri, “Mama Samia ametuwezesha kuona mwanga wa maendeleo, na kwa kupitia uongozi wake, tumejifunza kuwa na matumaini.”

Hakika, Mama Samia ni kiongozi anayeonesha mfano wa jinsi ya kuleta maendeleo ya kweli katika jamii.

Wakulima wa Mtwara wakiwa na dhamira thabiti, wanajipanga kutetea maendeleo yao kwa kumchagua Mama Samia katika uchaguzi ujao.

Huu ni wakati wa kuimarisha uongozi wa Mama Samia, ambaye si tu mkombozi wa wakulima, bali pia ni chaguo sahihi kwa mustakabali wa Taifa letu.

Tumaini letu liko mikononi mwa Rais Samia.

View: https://www.instagram.com/reel/DBHCq_9qMT4/?igsh=MWdycDE2b2ZkbDJ0Yw==
 

Attachments

  • VID-20241014-WA0037.mp4
    5.8 MB
Yeeeerrrrreeeeh!

Baada ya bei ya korosho kupaa na kuchanganya mwaka huu mbuzi kuanza kunyweshwa soda tena kama ilivyokuwa awali.

Nyau de adriz member mwenzetu yuko huko Lindi anabangua na kulangua korosho. Toka mwezi wa sita ananiringia kafanya mtihani sasa anajishughulisha na kilimo nikaja kugundua kumbe korosho.

Halafu kuna reply flani kwenye comment yangu humu aliniringishia ataoa mwarabu.

Yani huyu dogo ndo wale watanywesha mbusii soda za kutosha.

Mashirika ya kutetea haki za wanyama ingilieni kati mbusii wasinyanyasike kwa kunyweshwa sumu (soda) na hawa matajiri uchwara watarajiwa.

Nyau de adriz
 
Kanda ya kusini kuchele Ndanda kuchele.
CCM kwani imekuwaje? Hela izunguke mikoa yote Madalali wa korosho waondoke.
Kusini tumeona

#MAMA SAMIA KAUPIGA MWINGI KAMA ALIVYOUPIGA UNCLE 2017/2018

kiufupi kila mkulima na kangomba afurahi.

Mnada wa kwanza 4,090 kwa newala na tandahimba

Hii bei ni kubwa sana kwa jinsi watu walivyokuwa wamekata tamaa hata YA kulima na kulizia lorosho zao.

Kumbe miaka ya nyuma mlikuwa mnatuhujumu kwa kiwango kikubwa namna hii .Mwaka jana minada ilifika hadi 1600 ila mwaka huu bei imepaa zaidi.

Kangomba tulio nunua chache kwa kuogopa bei itakuwa chini tumehuzunika sana.

Walio jilipua kwa 1500 wameona matunda yake..

Korosho ni dhahabu yakusini korosho inaweza kukutoa mchana kweupe korosho ni utajiri.

TUNAWASHUKURU CCM KWA KUWAONDOA MADALALI WENU WA KOROSHO.

Soma Pia: Rais Samia umetuteIekeza Wakulima wa Korosho?

======
Leo Oktoba 11, 2024, historia imeandikwa katika mikoa ya kusini baada ya kufanyika mnada wa kwanza wa korosho ulioandaliwa na Chama Kikuu cha Ushirika Tandahimba na Newala (TANECU).

Katika mnada huo, jumla ya tani 3,857 za korosho zimeuzwa kwa bei ya juu ya shilingi 4,120 kwa kilo, huku bei ya chini ikiwa shilingi 4,035. Haya ni mafanikio makubwa kwa wakulima wa korosho ambao wamekuwa wakisubiri kwa hamu bei nzuri ya zao hili muhimu.

Wakulima wa Tandahimba na Newala wameonyesha furaha kubwa kwa hatua hii, huku wakimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada zake katika kuhakikisha bei za korosho zinapanda na kuwa na tija kwa wakulima. Wamesema kuwa mnada huu wa kwanza umewapa matumaini makubwa kwamba kilimo chao sasa kinaleta faida zaidi, na maisha yao yataboreka kutokana na ongezeko hili la kipato.

Akizungumza mara baada ya mnada huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Newala, mmoja wa wakulima wa korosho,alisema:
"Tunamshukuru sana Rais Samia kwa juhudi zake za kuhakikisha tunapata bei nzuri kwa mazao yetu. Hii ni hatua kubwa kwa wakulima wa korosho, na tunaamini kwamba serikali itaendelea kutusaidia ili tuendelee kuuza kwa bei nzuri kama hii."

Aidha, wakulima hao wameiomba serikali kuendelea kusimamia bei hizi kwenye minada ijayo, huku wakionyesha imani kwamba chini ya uongozi wa Rais Samia, sekta ya kilimo cha korosho itaendelea kuimarika na kutoa tija kwa wananchi wa mikoa ya kusini.

Mnada huu umeleta nuru mpya kwa wakulima ambao wamekuwa wakitegemea korosho kama chanzo kikuu cha mapato. Serikali imeonyesha dhamira thabiti ya kuimarisha bei za mazao ya kilimo, na hatua ya leo ni ishara tosha kwamba wakulima wanapewa kipaumbele ili kuinua uchumi wa mikoa ya kusini.
Rais amefanya mambo mengi sana kwenye Kilimo.

Bei zimevunjwa na kuweka rekodi kwenye mazao ya Kakao,korosho,tumbaku,ufuta.

Hii bei ya koroshi ingekuwepo mwakanizkusini kulikuwa hakuna haja ya kampeni hope pia utakuwepo.

Mwisho kina Bashe futeni Yale makato wanayolalamikia pamoja na kuwapa pembejeo za Bure Kwa wakati.
 
Nyie matahira mbona nyama ilivyopanda bei hamkumpongeza huyo Samia?
Dola ilivyoshuka thamani hamkumpongeza?
Mafuta yalivyopanda bei hamkumpongeza?
 
Back
Top Bottom