I f you know the meaning of collective responsibility then you cannot exonerate her from the decisions that were taken when she held the number two spot.
Kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa JMT anaweza tuu kushauriwa na yeyote, wasaidizi wake, wamshauri wake, baraza la Mawaziri, lakini kwenye kufikia maamuzi, ni yeye kama yeye, halazimiki kufuata ushauri wa yeyote, hivyo hata kama Samia alikuwepo kwenye cabinet ya JPM na uamuzi uliofikiwa kwenye kila jambo ulihesabika ni uamuzi wa pamoja, lakini all the responsibilities and the consequences of uamuzi huo, lies with the president kwasababu ndie the final decision maker na the responsible one, wengine wote wanatekeleza Kwa niaba ya Rais wa JMT.
Ndio maana hata JPM alikuwepo kwenye cabinet ya JK iliyo ipitisha bandari ya Bagamoyo, lakini alipoingia yeye aliipiga chini. Hata JPM alikuwa ni mjumbe wa NEC iliyopitisha ilani ya uchaguzi ya CCM yenye kipengele cha kukamilisha mchakato wa katiba mpya, na akainadi ilani hiyo, lakini baada ya kuwa rais aliitosa katiba mpya kwa hoja kuwa "sio kipaumbele changu".
Vivyo hivyo kwa Samia, japo alikuwa ndie number 2 wa JPM, na alikuwa sehemu ya maamuzi ya pamoja ya JPM, lakini kuna mambo yaliyokuwa yanafanyika, yalikuwa sio, na alikuwa hakubaliani nayo, lakini anayanyamazia kwa kutungwa na kipengele cha uamuzi wa pamoja lakini sasa baada ya yeye kuwa ndiye number 1, top, ameyafumua fumua na kuyatosa.
Hivyo hata kama Samia alikuwa sehemu ya JPM, lakini asihukumiwe kwa madhambi ya JPM, kwenye mazuri, yes ni pamoja Sana, lakini kwenye mabaya na madhambi, kila mtu aubebe msalaba wake mwenyewe.
Wananchi hatuwezi kawa FIDUCIARY kwa RAIS, if I understand the meaning of the word, The president has a FIDUCIARY responsibility to the citizens by taking their interest first and not her own interests!
Fiduciary relationship, ni mahusiano yenye kuwajibika kisheria, kama mzazi na mtoto, mwalimu na mwanafunzi, padri na muumini, daktari na mgonjwa, mfungwa na Bwana jela, etc, hivyo kwenye good citizenship, Samia kama rais wetu, has a duty of care kututumikia, na sisi kama raia wema tuna wajibu wakumsaidia as a duty of care ili aweze. Mimi part yangu ni kwa kuongea kwenye vipindi vyangu, na Kwa kutumia kalamu yangu kama kuandika humu na kwenye makala zangu,na wewe kwenye sehemu yako, and together we can if everyone will play his part. Play your Part.
P.