Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Hakika nimefurahishwa sana na Mwandishi huyu Pascal Mayalla wa kipekee aliyemuuliza swali Rais lenye msingi na hata rais kajibu kwa ubabaishaji. Natafuta clip au mwenye nayo aiweke.

IMG_0341.JPG


Kwanza kaanza kwa kuitaja JamiiForums kwa kusema ni mwanachama mwandamizi wa JamiiForums.

Hayo yameelezwa na Mh Rais wakati akijibu swali la mwandishi wa habari wa kujitegemea ndugu Mayalla , alipo muuliza mh Rais kuwa alipata wapi mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa kutoa maoni yao , na kudhibiti bunge ambapo bunge likitaka kusafirisha wabunge kwenda nje ya nchi waende wakaombe kibali kwa mheshimiwa Rais , haya mamlaka umeyatoa wapi ? kwakua uliapa kuilinda katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Majibu ya Rais "kwanza naomba ndugu mayalla unapo jiuliza kuhusu mihili hii pia jiulize kuwa nani anatafuta pesa na nani anayetoa pesa kwenye mihili hii mingine ya bunge na mahakama kama ukifahamu haya unaweza kufahamu kuwa ni mhimili gani ambao unaweza kuwa unamamlaka kwenye mihili mingine , kwa mfano nilipoenda bungeni kuhutubu niliwahutubia wabunge wabane matumizi mbele yao, na vilevile nilienda kwenye sherehe za mahakama wakaniambia kuwa hawatoi hukumu mapema kwa sababu hawana fedha niliamua muda huo huo kuwapatia fedha mhakimu na wao hawakuenda mahala popote kulalamika kuhusiana na hilo...

Nimemsikia Pasco Mayalla akiuliza swali kwamba Rais amepata wapi mamlaka ya kuwaambia Wabunge (legislature) na Mahakama (Judiciary) waombe ruhusa kwake watakapo kusafiri?

Hoja ya Pasco ni kwamba kuna separation of powers yaani Executive, Judiciary na Legislature ambazo zinatakiwa zifanye kazi bila kuingiliana. Hilo ni sawa ila Pasco kweli hafahamu kwamba Rais wa Jamhuri ni mkuu wa dola na chini ya dola ndio unapata executive arm, judiciary arm na legisleture?

Hajui kwamba Rais wa Jamhuri ni Head of Government na wakati huohuo ni Head of the State?
 
Kamuuliza kuwa kapata wapi mamlaka ya kuzuia safari za watumishi nje wakati kuna mihimili mitatu na yote inajiongoza yenyewe?

Pia kwanini mikusanyiko ya kisiasa inatambulika na katiba lakini yeye kaizuia wakati aliapa kutumikia nchi kwa mujibu wa katiba?

Kama wangekuwepo hata watano tuu wenye mwelekeo wa Pasco hakika angependa hayo masaa mawili yaishe aondoke, lakini kwa vile waliopo wengi ni makanjanja basi kawaambia waulize mpaka wachoke wenyewe.
 
Nimemsikia Pasco Mayalla akiuliza swali kwamba Rais amepata wapi mamlaka ya kuwaambia Wabunge (legislature) na Mahakama (Judiciary) waombe ruhusa kwake watakapo kusafiri?

Hoja ya Pasco ni kwamba kuna separation of powers yaani Executive, Judiciary na Legislature ambazo zinatakiwa zifanye kazi bila kuingiliana. Hilo ni sawa ila Pasco kweli hafahamu kwamba Rais wa Jamhuri ni mkuu wa dola na chini ya dola ndio unapata executive arm, judiciary arm na legisleture?

Hajui kwamba Rais wa Jamhuri ni Head of Government na wakati huohuo ni Head of the State?
 
Ila Kajibiwa Kisiasa!
"Unajua Ni Kwanini Hotuba ya Kusitisha Mikutano na Shughuli za Kisiasa Bungeni?Mpiga Chakula na Mgawaji Ndie Ajuaye Chungu Kilivyo!Soma Katiba Ujue Katika Mihimili Yote Mitatu ni Upi Wenye Nguvu"
 
Back
Top Bottom