Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Nchi tunaipenda ni ya wote na kumbuka Rais ni binadamu siyo Mungu anamazuri yake na mapungufu pia.
 
abe80808f0888be73e1291c515a1f017.jpg

Habar wajamen!!.

Nimetoka hapa Kigamboni nikiwa kwenye daladala,nikakuta watu wanajadili na kubishana kidogo kama mrejesho wa mkutano wa jana kati ya rais na wanahabari;lakini pamoja na maswali mengine watu wengi nimeona wanamtaja sana huyu Mayala,kuwa aliuliza swali zuri japo Rais hakumjibu badala yake akaishia kutafsri jina la Mayala kulingana na kilugha chake.

Mim binafsi huyo Mayala ndio nimeanza kumjua jana ,yaani mkutano wa jana ndio umenifanya nimjue kwani hata kama niliwahi kumskia basi sikuwahi kuchukua muda mwingi kukaa nikafikiria chochote kumhusu.

Swali alilouliza Mayala,basi hapa kwenye daladala(UDA tupo takribani abiria45-56) wote wanaonesha kuunga mkono swali la huyu Mayala,na zaidi kuonesha kuwa hawakurdhika na majibu aliyotoa Rais.

Naskia swali lilimtaka Rais ase me au ajibu kuwa kwakuwa Taifa,linamihimili mitatu,yaani Bunge,Mahakama na Serkali yenyewe kama cjakosea,akaulizwa yeye kama Rais ni mhimili mmoja tu kati ya hizo tatu,na kikatiba mihimili hio inajitegemea,

Rais aliapa kuilinda katiba,je anatumia mamlaka gani kutoa matamko yanayopenya hadi kwenye hio mihimili mingine?..

Lakin pia Rais aliulizwa kuhusu Kutoa matamko ya kuzuia mikutano ya kisiasa.

Rais alioneshwa kuchukizwa na swali hili,na kuthibitisha hili alimshambulia muuliza swali kwa kutafsiri jina lake kuwa lina maana 'njaa' kulingana na kisukuma,na aliendelea kwa kumwambia swali alilotegemea amuulize.


Hii ilitakiwa kuwa ati angemuuliza kwanini alihutubia kwa mara ya kwanza bungeni? Sasa sijui kuhutubia bungeni ndio kulimaanisha amepewa mamlaka ya kuingilia mihimili mengine? Bila shaka hapana..

Jibu lake lilikuwa rahisi kuwa ati "anafanya yote kwa sababu anabana matumizi",
hivi anabana matumizi kwa kuzuia mikutano ya vyama vya upinzani?.....how does this work?
 
Mayala alianza hotuba,kujifagilia na kutangaza kampuni yake na kujipigia debe la kutafuta fursa ikulu .Sehemu kubwa ya aliyonngea yalikuwa hasa ya kujinadi mnadani yeye binafsi.Kwangu naona kama aligeuza Ikulu na ile press conference kama gulio la kujinadi zaidi kuliko kuuliza swali.
Out of order
 
...kwanza ni kupomgeze Pascal Mayalla kwa kuuliza maswali mazuri aka ya msingi...pili,nashindwa kumtofautisha mjibu maswali ya Pascal na yule kijana aliyechora mazombi kwenye karatasi la kujibia maswali ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne...
 
Kifungu kinachompa mamlaka rais ni kuanishwa kwa majukumu yake, kuwa Serikali ndiyo mkusanyaji mapato na msimamizi wa matumizi ya pesa, kwa maana hiyo muajiri mkuu ndiye anayebuni vyanzo na ndiye anayesimamia matumizi ya mapato hayo. Udhibiti wa Safari za nje lengo lake ni udhibiti wa Matumizi ya pesa ya umma ambapo mihimili mingine yote inaomba pesa toka kwa muidhinishaji mkuu ambaye ni rais. Makosa yetu ni kudhani mihimili mingine imeingiliwa kwa kuzuiwa kusafiri tu hatuendi mbali na kujua udhibiti huo wa safari lengo ni kudhibiti matumizi ya fedha za umma ambazo zingeweza kutumiwa kwa shughuli nyingine za muhimu zaidi. Hii NDIYO MAANA YA MAJIBU YA RAIS kwa Pascal Mayalla
Kama katika marking kungekuwa na negative rating ningekupa (-100%) kwa huu UP ulioenda. Chukua 0% yako inakutosha kwa hilo jibu lako
 
mengine alipoulizwa akiambiwa eti ya kichokozi.

lakini mayala nampa bigup sanaaa.

tungekuwa nao kama kumi na yule aliyeuliza wa bbc namwingine kahusisha zanzibar
 
....sidhani kama ataalikwa tena ikitokea mkutano mwingine, na hata akialikwa nahisi atapewa muongozo bhahahhaaaaa....
 
Kuna maswali ukiuliza tuu utajulikana kama umetumwa alafu yanashusha cv yako muda mwingine bora unyamaze ili watu wajue huna swali kauliza upuuzi tuu
 
1.Kuwa head of state maana yake ni kuingilia mihimili mingine? 2. Unakubaliana na kinachofanyika kwa kuwa kinafanywa na head of state?
Kuingilia kwa maana gani? Kwamba wakitaka kusafiri inabidi wapate state house clearance ni kuingilia muhimili mwingine? Hufahamu kwamba utaratibu huo upo siku nyingi?
 
Kuingilia kwa maana gani? Kwamba wakitaka kusafiri inabidi wapate state house clearance ni kuingilia muhimili mwingine? Hufahamu kwamba utaratibu huo upo siku nyingi?
Rejea swali la Mayala!
 
Hahahaha mkuu mi mwenyewe nilikua napata shida nilikua nikidhani ni huyu wa jf, kumbe huyu wa jf ni mropokaji wa humu tu hana lolote, shame on him
Yeye mwenyewe kabla ya maswali yake kwa rais alijitambulisha ni member mwandamizi wa Jamiiforums
 
Ni wawili mkuu, Sami Awami wa BBC naye kamchapa swali la Demokrasia ameshindwa kujibu kifasaha. Maswali magumu anapanic.
Ogopa sana kuujua ukweli na undani wako.Mapungufu yako,kama anayekueleza anaeleza taratibu kama Mayalla.Unaweza anguka ghafla.Mayalla ameuliza baadhi ya mapungufu ambayo kila mtu anayo.Binafsi ningeunga unga tu majibu.Ila ukweli utabaki kama hivi,Baba atimize majukumu ya familia kama ilivyo siku zote.Mama na atkmize wajibu wake kama mama.Na watoto pia wathamini majukumu yao.Hapo ndipo familia huwa bora.Nchii yetu ni mfano wa familia flani hivi.Baba kuwa mkali sana haimaanishi utaogopwa.Hapana wote tutakaa pembeni huku tukiiga ukali wako.Na kusema ngoja tuoone mzee atafikia wapi.Kuongoza watu hasa kizazi hiki cha nyoka.Huhitaji nguvu kubwa ya kuongea na vitisho.Ndio maana kila kukicha mitaa inazidi kubadilika na matatizo hayaishi.Wajifunze kuepuka ushabiki na kuja ghafla na matamko ambayo yana athari kubwa kwa raia.Hasa wasio kuhitaji.
Muda unaenda na hali inazidi kuwa ngumu.Waangalie na hayo pia si kila kitu ni kupinga.Hakuna Mungu hapa Duniani wala asiyekosea.Mkuu wa nchi unafanya mazuri tunayaona.Ila pia pokea mapungufu yako sio dhambi.Sikiliza pande zote na tazama kwa sasa jamii yako inavyoishi.
Tukiendelea na kauli za kuudhi na tukaonekana wachache ndio tunaiongoza nchi.Hata wanaotuzunguka watatuangusha haraka sana,hasa kimaendeleo.Watakuongelea kuwa upo vyema kumbe wanatumia huu muda wa sisi kutokueleweka.Nini tunahitaji.
ANGALIA KUPOLOMOKA KWETU NI FAIDA KWA NCHI JIRANI.NA WATAZIDI KUKUSIFIA ILI MUDA UENDE.TUREKEBISHE TUNAPOKOSEA HARAKA.HII NCHI SI YA MTU MMOJA.
 
Wakuu kama mnakumbuka mdau mbishi wa Katiba ya Warioba Bwn.Humphrey Polepole alipewa ukuu wa Wilaya.Hii ilitafsriwa kuwa ni kumziba mdogo bwana huyu kwa kutumia kipande cha keki.Bwana yule hakuna na uwezo wa kutema kile kipande utamu ukamzidia Leo hii ni DC wa Ubungo cheo ambacho alikipinga sana akiwa timu ya Warioba.

Sasa from Nowhere amekuja Mwana JF mwenzangu Pasco,amevuma sana Leo mitandaoni.Paskali amehoji mambo magumu sana na hayakupata majibu,si kwa bahati mbaya,bali hakukuwa na majibu.

Je,mbinu iliyotumika kumrambisha udambwi-dambwi H.Polepole au Dr. Ryoba utatumika kwa Msukuma Paskali?

Ombi:Kwa kuwa Paskali amewahi kutuambia humu kuwa yeye hana shida na cheo kwa kuwa ana kipato kinachomtosha,Je uyaendelea na msimamo wako. Je,unamshauri nini Polepole kwa yale majibu ya Rais Hakuna katiba mpya?

Kwa nini mnaunganisha matukio juu juu?

Mpaka Humphrey anapewa ukuu wa wilaya alikuwa tayari alishawapiga chini UKAWA, na kwenye kampeni aliongea pumba sana na zile ndo zimempa ukuu wa wilaya.

Alishabadilika zamani sana na kuongea ongea pumba ndo baadae kalipwa.
 
Nimemsikia Pasco Mayalla akiuliza swali kwamba Rais amepata wapi mamlaka ya kuwaambia Wabunge (legislature) na Mahakama (Judiciary) waombe ruhusa kwake watakapo kusafiri?

Hoja ya Pasco ni kwamba kuna separation of powers yaani Executive, Judiciary na Legislature ambazo zinatakiwa zifanye kazi bila kuingiliana. Hilo ni sawa ila Pasco kweli hafahamu kwamba Rais wa Jamhuri ni mkuu wa dola na chini ya dola ndio unapata executive arm, judiciary arm na legisleture?

Hajui kwamba Rais wa Jamhuri ni Head of Government na wakati huohuo ni Head of the State?
mkuu,
vp mahakamani,hoja kama hii inaweza kukubarika?
 
Hakuna njia rahisi ya kummaliza mtanzania kama kumpa cheo/ulaji/uheshimiwa..

Misimamo yake yote inasambaratika na kutokomea kusikojulikana!
 
Back
Top Bottom