Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Katika maswali ya hovyo kabisa kuulizwa jana na wanahabari ni lile lililotoka kwa Pascal Mayala.

Unawezaje kuuliza ni kwa mamlaka gani aliyopata rais ndani ya mihimili 3 iliyopo yaani bunge, serikali na mahakama kwa yeye kujitwalia mamlaka ya kubana matumizi?

Kwanza napenda ifahamike kuwa pamoja na kuwepo kwa mihimili 3 inayojitegemea bado ifahamike kwamba inaingiliana Katika Utendaji.

Na Katika muingiliano huu ifahamike kwamba katiba yetu inamtambua rais kama:

1. Sehemu ya bunge na anawakilishwa na Waziri mkuu Bungeni.

2. Rais ndiye msimamizi mkuu wa mipango yote ya ukusanyaji na matumizi ya fedha za umma Katika nchi yetu.

3. Rais ndiye msimamizi mkuu wa Utendaji kazi kwa watumishi wote wa umma Katika nchi yetu. Iwe ni kwenye fedha, afya, ulinzi, usalama, Elimu n.k.

Bunge na mahakama ni taasisi za umma na watendaji wake ni watumishi wa umma wanaowajibika kuteleza sera zinazopangwa na kusimamiwa na raisi Katika matumizi ya fedha za umma.

Hivyo Swali la Pascal Mayala hali kuwa bora bali lilionyesha hafaham vema katiba yetu na majukumu ya rais wetu.

Alipaswa ajifunze kabla ya kuuliza.

Kwa wale mnaomshangilia mnaonyesha pia mnahitaji kufahamu haya.
Sawa mkuu mpaka 2020 (m2020 ). Tumekulewa _ kwa nini unahalalisha lakini separation of powers ina maana tofauti na hii tafsiri yako na mkulu.
 
Rejea swali la Mayala!
Mayalla aliuliza kwamba Rais kapata wapi mamlaka ya kuwaambia Majaji na Wabunge kuomba kibali kabla ya kusafiri. Huo siyo uingiliaji wa mihimili mingine. Ndio maana Rais akauliza mbona hawakuhoji siku aliyoipa Mahakama hela za kuendesha kesi na pia mbona hawakuuliza siku ambayo Rais alihutubia Bunge na kueleza sera zake za kubana matumizi.

Hivi Jaji Mkuu anaweza kwenda kulihutubia Bunge kwa mujibu wa Sheria? Hivi Bunge lina ruhusa ya kubatilisha hukumu ya mahakama?
 
Kwakweli kauliza swali zuri japo halijajibiwa hata kidogo, eti mwenye chungu, mara fedha za bunge.....

Mara ohoo mayalla maana yake njaa yaani swali lilikuwa gumu kweli kweli kiasi sura ilianza kubadilika.Nampongeza sana Pasco Mayalla ingawa namhofia uenda asipewe tena mwaliko wa kweli kula bata Ikulu kwa ukosefu wa nidhamu uliotukuka.Nasema yale maswali yalilenga kumjaribu na kumdrive Mheshimiwa ambaye mwisho wa alisisitiza yeye ndio Rais sijui nani kamwambia yeye si Rais.
 
Kweli kwa swali gumu kama lile la Jana lazima alambishwe wapi Slow Slow na zile kelele zake
 
Wajameni tuache kutoa mapovu. Pascal Mayala haelewi utendaji serikalini ukoje ndio maana aliuliza ili aeleweshwe. Kuuliza si ujinga pamoja na.kwamba yeye niwanasheria. Hajawahi kuwa mtumishi wa umma na hivyo haelewi namna gani serikali na mihimili mingine inafanya kazi. Sidhani kama ni busara kumsifia kauliza swali la maana wakati swali lile lilikua wazi tu. Ni suala la kueleweshwa tu.
 
kauliza swali zuri na bila uoga kwa sababu ana uhuru wa kifedha pia yupo huru kikazi(mwandishihuru) ,sasa imefahamu kwamba ili journalist awe huru ni lazima afanye kazi yake independently, mkuu Pasco au Pascal Mayalla hongera,naamini ni mtu mmoja ila kama nimechanganya samahani
 
kauliza swali zuri na bila uoga kwa sababu ana uhuru wa kifedha pia yupo huru kikazi(mwandishihuru) ,sasa imefahamu kwamba ili journalist awe huru ni lazima afanye kazi yake independently, mkuu Pasco au Pascal Mayalla hongera,naamini ni mtu mmoja ila kama nimechanganya samahani
ni mtu mmoja hujachanganya
 
binafsi napenda kuwa huru kwa kazi zangu binafsi,ajira ya kupewa na ambayo muda wowote naweza aibishwa na kutenguliwa hapana,pia na naamini kwa mtu wa aina yangu hawezi kubali ajira za kupewa kama unazozitaja
 
Wakuu kama mnakumbuka mdau mbishi wa Katiba ya Warioba Bwn.Humphrey Polepole alipewa ukuu wa Wilaya.Hii ilitafsriwa kuwa ni kumziba mdogo bwana huyu kwa kutumia kipande cha keki.Bwana yule hakuna na uwezo wa kutema kile kipande utamu ukamzidia Leo hii ni DC wa Ubungo cheo ambacho alikipinga sana akiwa timu ya Warioba.

Sasa from Nowhere amekuja Mwana JF mwenzangu Pasco,amevuma sana Leo mitandaoni.Paskali amehoji mambo magumu sana na hayakupata majibu,si kwa bahati mbaya,bali hakukuwa na majibu.

Je,mbinu iliyotumika kumrambisha udambwi-dambwi H.Polepole au Dr. Ryoba utatumika kwa Msukuma Paskali?

Ombi:Kwa kuwa Paskali amewahi kutuambia humu kuwa yeye hana shida na cheo kwa kuwa ana kipato kinachomtosha,Je uyaendelea na msimamo wako. Je,unamshauri nini Polepole kwa yale majibu ya Rais Hakuna katiba mpya?
Next time na wewe nenda kamuulize Maswali yasiyokua na majibu ili akuzibe mdomo! Haya ya jana hebu tuyaacheni maana wao wamejichimbia shimo ambalo litakuja kuwa kaburi lao siku si nyingi, makofi yale waliyopiga kwa vicheko siku si nyingi yatabadirika kuwa mapigo ya Mapambio
 
Mayalla aliuliza kwamba Rais kapata wapi mamlaka ya kuwaambia Majaji na Wabunge kuomba kibali kabla ya kusafiri. Huo siyo uingiliaji wa mihimili mingine. Ndio maana Rais akauliza mbona hawakuhoji siku aliyoipa Mahakama hela za kuendesha kesi na pia mbona hawakuuliza siku ambayo Rais alihutubia Bunge na kueleza sera zake za kubana matumizi.

Hivi Jaji Mkuu anaweza kwenda kulihutubia Bunge kwa mujibu wa Sheria? Hivi Bunge lina ruhusa ya kubatilisha hukumu ya mahakama?
Mkuu Kimbunga, utakuwa ama hufuatilii au umeamua tu kujenga hoja kwa kusimamia kile alichojibu rais. Si kweli kwamba watu hawakuhoji au kuuliza mheshimiwa Rais alipoipa hela mahakama. Kulikuwa na mjadala mkali sana uliojielekeza katika hofu ya Rais kuingilia uendeshaji wa kesi. Suala la kubana matumizi halia tatizo, na wananchi wanaunga mkono, wanachohoji wananchi, na bila shaka Mayala alisaidia wananchi kuhoji kiko wazi. Maswali yako ya mwisho sioni mantiki yake katika hoja ya msingi!
 
Asee uyuu jamaa ni shujaa japo swalii haljajibiwa kama inavyotakiwa ila hongera kwake
 
Back
Top Bottom