Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

1. Nanukuu: "Sikuja kufukua Makaburi, bali kuanzia nilipoikuta nchi na kuipeleka mbele".
Mwisho wa Kunukuu
Nadhani wale mliokuwa mnaropoka Kama Lowassa ni fisadi apelekwe Mahakamani mmejibiwa. Muhimu ni kutokubali Watu wa aina ya LOWASSA kutopewa nafasi tena nchi hii , matendo yao sasa yanatosha. Tumuunge mkono rais wetu.
2. Nanukuu: " Mifuko ya jamii na Mabenki imefilisika lakini wakopaji wakubwa ni wanasiasa, UKAWA wamo, CCM wamo , lakini utakuta wao ndiyo wapiga kelele na waongeaji wakubwa sana" mwisho wa kunukuu.

Kwa ujumla kama vyombo vya habari kesho havitakuja na headline kuhusiana na mambo haya mawili ujue hatuna wana habari. Mabenki kuwa na hali mbaya na hata kupelekea mengine kuwa chini ya uangalizi wa BOT ni mambo ambayo yamekuwa ni viashiria vya hali mbaya uchumi na ndiyo habari ya mjini hivi sasa, lakini kumbe wale wanaopiga kelele kuilaumu serikali ndiyo hao hao wanaopelekea hali hiyo. Hii ni hatari sana.
Ni tabia ya kutanguliza maslahi binafsi ndiyo iliyotufikisha hapa. Kutoshughulika na Watu waliohusika kuihujumu uchumi wa nchi yetu huko nyuma isiwe sababu ya kuamini kwamba hao watu hawakulihujumu taifa. Jambo la muhimu ni kutowapa nafasi tena watu wa aina hiyo katika taifa hili. Tumuunge mkono rais ili altujengee taifa lenye watu wa kutanguliza uzalendo mbele badala ya maslahi yao binafsi. Kwa kifupi tuseme tunataka taifa jipya na tusema SASA BASI kwa wale waliolihujumu taifa.
NAMUUNGA MKONO RAIS JPM .
Nice words...
 
Kamuuliza kuwa kapata wapi mamlaka ya kuzuia safari za watumishi nje wakati kuna mihimili mitatu na yote inajiongoza yenyewe? Pia kwa nini mikusanyiko ya kisiasa inatambulika na katiba lakini yeye kaizuia wakati aliapa kutumikia nchi kwa mujibu wa katiba?
Kama wangekuwepo hata watano tuu wenye mwelekeo wa Pasco hakika angependa hayo masaa mawili ya ishe aondoke, lakini kwa vile waliopo wengi ni makanjanja basi kawaambia waulize mpaka wachoke wenyewe.
Kungekuwa na maswali ya kufikirisha Rais angeomba muda uishe haraka aondokane na waandishi lakini kwa udhaifu wa maswali yaliyosinyaa hata dakika mbili za mapumziko kazikataa na hata mwishoni kasema waendelee hata mpaka saa nane.

Loo wandishi wa Tanzania kweli waliishajichokea.
 
Hakika nimefurahishwa sana na Mwandishi huyu Pascal Mayalla wa kipekee aliyemuuliza swali Rais lenye msingi na hata rais kajibu kwa ubabaishaji. Natafuta clip au mwenye nayo aiweke.

Kwanza kaanza kwa kuitaja JamiiForums kwa kusema ni mwanachama mwandamizi wa JamiiForums.

Naungana na wewe kutoa pongezi kwa paskali wa Jamiiforums.

Lakini kabla ya mkutano wa Rais na waandishi wq habari tuliaminishwa humu kuwa huo mkutano ni usanii tu maswali yameishapangwa.

Na haya maswali ya Paskali wa Jamiiforums yalikuwa yameishapangwa au?
 
Kuna wakati nilikuwa nafuga mbwa wanne kwa ajili ya ulinzi, lakini nikaja gundua kuna mmoja ana tabia ya kubweka hovyo bila sababu ya msingi. Nikamuona ni mwehu tuu.
Lakini hata watu wapo wa aina ile ya mbwa wangu, anaweza kuropoka lolote pasipo sababu ya msingi
Hata hivyo umempatia heshima kubwa sana kumjibu. Mimi nimempuuza huyo.
 
Na uccm wangu ila hapa mh. Presida kazurula mbaya...! Ingekuwa necta angeangukia pua yaani zero.([emoji778] %)
 
Pascal mayalla ameiwekea heshima nchi akumuogopa tembo uchwara
 
Swali kutoka kwa Mr. Mayala.
Mh. Rais uliapa kulinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa TZ, Je ulipata wapi mamlaka ya kuzuia mikutano ya siasa wakat katiba haikupi nafas ya kufanya hivyo?
Jibu....
Mayala kwa kisukuma ni njaa! Yawezekana ww Mayala ulizaliwa kipindi cha njaa! Wote wakacheka[emoji16], akaendelea....
Mh. Mayala uliwahi kujiuliza kwa nn hotuba yangu ya kwanza ya kubana matumizi niliitolea Bungeni Mbele ya Spika? Ukijua mpikaji wa chakula ni nan na mgawaji wa chakula ni nan bas utanielewa.

Hilo jibu la swali lililoulizwa , cjui kama ni vinaendana.
 
Swali la Pasco lilikuwa swali hasa ila wengine mhhhhhhhh.Hadi kilimo cha mihogo hilo si RC tu.
 
Mayala hakufanya follow up
Akaogopa kufuatilia swali
 
Paschal Wewe ni jembe,kwanini Tido kazingua? Rais hajajibu swali lolote pale
 
Unachokisema si kweli....rais hawezi kubugudhi mihimili mingine namna hiyo unayotaka kutuaminisha.

Kukitokea migongano rais hataweza tawala....mihimili mingine ikiamua ku-exercise their power against executive kwa pamoja nchi haitatawalika.

Executive kupeleka hela kwenye hii mihimili mingine sio eti ndio wana mamlaka zaidi ya hiyo mihimili,hii ni myopic view.

Kupeleka hela ni wajibu wa executive kwa hii mihimili,hakuna mambo ya kuomba...nani kakwambia ni hisani ya executive kupeleka hela judiciary na parliament?

Mnajua nyie mna matatizo...huwezi kuhemea mihimili mingine namna hii as if hii mihimili ni wake wako unaweza fanya utakacho...

Unaweza jenga ego na hasira kwenye hii mihimili mingine na hiyo ikulu ukaicha ukaenda Chato kulima...tatizo mnajifanya nyie executive ndio mna ego kubwa sana,mtasababisha friction na nyie ndio mtafeli..

Kwanini masiendeshe nchi kwa inclusion na power brokerage kila mtu akajiona anatakiwa kichangia na yupo included na anaheshimika?Nchi huwezi ijenga peke yako,huwezi,nguvu hizo hamnazo.Nchi ni watu kama wewe na wana uwezo kama wako au zaidi,treat people with respect and honest.Acheni kulewa madaraka mapema hivi.
Rais kasema hivi ''Katika mihimili mitatu upo mmoja uliozama zaidi'' Ukielewa hilo hoja zako zote hapo juu zinakosa mashiko
 
Kajibu mihimili inalingana urefu ila mmoja umechimbiwa zaidi kwa kwenda chini, eleweni
 
ASANTE SANA MAYALLA HAKIKA UMEWEKA UNAFIKI PEMBENI NA KUSEMA AU KUULIZA SWALI LA MBOLEA TENA YENYE RUTUBA KWA WEREVU TUMEKUELEWA ILA KWA WEHU WATAKUWA HAWAJAKUELEWA NA DAIMA HAWATA KUELEWA KISA KUFIKIRI KWA KUTUMIA TUMBO BADALA YA KICHWA.
FUMBO MFUMBIE MJINGA MWEREVU ATALING'AMUA,UJUMBE UMEFIKA SAWIA BIN SAWIA AND THIS IS LIVE AND DIRECT.
BADO MTKUFU HAKUTOAA JIBU AME DIVERT QNS NA KUTOA MAJIBU ANAYOJISIKIA NA SIYO KAMA SWALI LILIVYOTAKA KUJIBIWA.
MUNGU AZIDI KUKULINDA KIJANA MAYALLA KWANI KILA MTU ATATOA HESABU YAKE SIKU ZA MWISHO,JE HAO WAANDISHI WANAFIKI NA MAKANJANJA AMBAO HAWAKUITENDEA HAKI TAALUMA ZAO KISA WOGA NA MASLAHI BINAFSI WATAMJIBU NINI MUUMBA WAO????
 
..hakuna mhimili wenye upper hand, uess mhimili mmojawapo umeamua kutokutekeleza wajibu wake wa kikatiba.

..huwezi kusema Raisi ni nambari 1 wakati anaweza kushtakiwa bungeni na kuondolewa madarakani.

..ningekuelewa, tena kwa kujilazimisha, kama ungesema bunge ni nambari 1. Kwasababu bunge likigoma kupitisha bajeti basi linaweza kupelekea kuitishwa kwa uchaguzi mkuu.

NB.

..Raisi anateua majaji lakini hana mamlaka ya kuwafuta kazi. Jaji anafutwa kazi baada ya kuchunguzwa na tume maalum.
Separation of powers haina ukuu

Hapa tukubaliane tu kuwa dhana nzima hakuielewa, hilo halina mjadala

Kwamba mhimili unaotoa pesa ndio superior! serious!
 
Unachokisema si kweli....rais hawezi kubugudhi mihimili mingine namna hiyo unayotaka kutuaminisha.

Kukitokea migongano rais hataweza tawala....mihimili mingine ikiamua ku-exercise their power against executive kwa pamoja nchi haitatawalika.

Executive kupeleka hela kwenye hii mihimili mingine sio eti ndio wana mamlaka zaidi ya hiyo mihimili,hii ni myopic view.

Kupeleka hela ni wajibu wa executive kwa hii mihimili,hakuna mambo ya kuomba...nani kakwambia ni hisani ya executive kupeleka hela judiciary na parliament?

Mnajua nyie mna matatizo...huwezi kuhemea mihimili mingine namna hii as if hii mihimili ni wake wako unaweza fanya utakacho...

Unaweza jenga ego na hasira kwenye hii mihimili mingine na hiyo ikulu ukaicha ukaenda Chato kulima...tatizo mnajifanya nyie executive ndio mna ego kubwa sana,mtasababisha friction na nyie ndio mtafeli..

Kwanini masiendeshe nchi kwa inclusion na power brokerage kila mtu akajiona anatakiwa kichangia na yupo included na anaheshimika?Nchi huwezi ijenga peke yako,huwezi,nguvu hizo hamnazo.Nchi ni watu kama wewe na wana uwezo kama wako au zaidi,treat people with respect and honest.Acheni kulewa madaraka mapema hivi.
Hodi hodi mwana wane naingia kupitia mlango wa nyuma..

Jamani kwanza mfahamu ya kwamba Katiba yetu imeandikwa kwa muundo gani kisha ndio tujenge hoja zetu kwa sababu NENO KUTOINGILIA halina maana kuweka USAWA wa KIMAMLAKA. Nachoelewa mimi ina maana kwamba mhimili mmoja hauwezi kuingilia shughuli za mhimili mwingine hivyo rais kama kiongozi wa Serikali ataifanya kazi yake ya shughuli za serikali pasipo kuingiliwa na Bunge ama Mahakama.

Mfano:- Bunge linalokaa na kujadili sheria ama kupitisha Muswada, rais na Mahakama hawana mamlaka ya kuingilia shughuli hiyo. Pia Mahakama inapofanya shughuli zake za kimahakama Rais na Bunge hawaruhusiwi kuingilia maamuzi ya Mahakama. Tofauti na Katiba ya Marekani ambayo Bunge na Mahakama zimeundwa ili kupunguza nguvu za kimamlaka (Power) ya rais na hivyo kwa kila shughuli za Serikali kuu vyombo hivyo vinahusika kwa njia moja ama nyingine (President Executive order or Proclamation)

Kwa wenzetu huwezi kuona mikataba ikiwekwa na nchi za nje pasipo Bunge au Mahakama kupitia, sisi majuzi tu Magufuli katangaza kughairisha sikuu za Uhuru na Muungano na ikawa. Tumeingia mikataba 21 na Morocco, ni mhimili gani umehusishwa? ama ni kifungu gani cha sheria kinachomkataza ama kusema Bunge linaweza kuingilia? Bila shaka sheria inasema wasiingilie sio waingilie. Sijui kaa nakosea lakini ndivyo nachoelewa mimi. Toka mikataba ya Buzwagi, Bulyanhulu hadi Richmond walihusishwa?

Leo hii ndio tumegundua kumbe hata mkataba wa India kuna mazao ambayo tunatakiwa kuzalisha nchini soko limeshapatikana India na fedha zipo mikononi mwetu, nani alijua hayo?. Labda nirudi nyuma kidogo, Magufuli alipopitisha Elimu bure hadi Sekondari lilijadiliwa lini bungeni? Kwa hiyo, kwetu sisi ilani yachama ikisha pita na wananchi kumchagua rais, kinachojadiliwa ni FEDHA TU. Wizara gani imepata kiasi gani na sio mambo gani yatafanyika.

Leo hii tumetangaziwa nchi ya Viwanda! Nini lengo la kuanzisha viwanda nchini ikiwa hatuna masoko nje? Je ni kukimu mahitaji yetu kwa nini wawekezaji watoke nje ama kuuza nje na kama nje tutauza vipi? tumejiandaa vipi kwa masoko nje ya EAC.inaonyesha wazi kwamba wananchi wengi walikuwa hawajui kinachoendelea, hata hao waandishi wa Habari. Kwa maana pana zaidi Bunge lipo pale kupitisha Bajeti tu ya serikali, nimeshangaa hata incentives zinazotolewa waandishi wa habari hawazijui wakaulize wapi vile!.
 
Rais kasema hivi ''Katika mihimili mitatu upo mmoja uliozama zaidi'' Ukielewa hilo hoja zako zote hapo juu zinakosa mashiko

Umezama zaidi kwenda wapi?

Kauli za kujitapa sio nzuri,hiyo kauli ni ya intimidation,sio sawa,itahamsha complexes kwa mihimili itakayojiona "midogo",yote ya nini?Ndio maana inatakiwa busara ya kiutu uzima.
 
Back
Top Bottom