Hongera Waziri Mkuu kwa kuwasikiliza Wafayabiashara. Kero zao zitatuliwe isiwe zuga tu ya kuwatuliza

Hongera Waziri Mkuu kwa kuwasikiliza Wafayabiashara. Kero zao zitatuliwe isiwe zuga tu ya kuwatuliza

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1684322485248.png

Habari,

Wakuu kama tunafatilia habari na mitandao tunatambua wiki hii nchini wetu imetawaliwa na matukio mengi. Miongoni mwa tukio lililogusa vituo vya habari ni pamoja na Mgombo wa wafanya biashara wa Kariakoo.

Imekuwa sio kawaida kwa viongozi wetu kujitokeza kusikiliza migogoro ya Wananchi na kero za Wananchi. Nampongeza Waziri Mkuu Kasim Majaliwa kwa kujitokeza mbele na kusikiliza madukuduku ya Wananchi kiuwazi.

Pamoja na kumpongeza kujitokeza kusikiliza bado nahimiza kwamba asibaki kusikiliza kero tu ili kutuliza upepo bali iwe ni sehemu ya mchakato wa kutafuta suluhu ya kero hizi.

Zaidi ya hayo pia zipo kero nyingi na sehemu tofauti tofauti zinawakabili Watanzania ni vyema viongozi wetu wasiishie Kariakoo peke yake na pia wasisubiri mgomo na maandamano.

Tanzania bora ya kesho inawezekana.
 
wametulizwa kisiasa tu mambo ayatabadilika nakuhakikishia mkuu.

kumbuka tukio la yule mfanyabiashara wa Kariakoo mzee Ramadhan Ntunzwe swala lake lilifika mpaka kwa Rais na PM lakini leo hii yamejirudia yaleyale.
 
wametulizwa kisiasa tu mambo ayatabadilika nakuhakikishia mkuu.

kumbuka tukio la yule mfanyabiashara wa Kariakoo mzee Ramadhan Ntunzwe swala lake lilifika mpaka kwa Rais na PM lakini leo hii yamejirudia yaleyale.
Juzi nilikua napita huko wilayani Urambo mkoa wa Tabora, nilimuona huyu Ramadhani Ntuzwe akiwa anaiza bidhaa mchanganyiko za nyumbani kwenye duka la kawaida kabisa.

Baada ya kuulizia habari zake, niliambiwa jamaa alifilisika kabisa na akaanza biashara upya kwa kulikimbilia Urambo ili kuokoa maisha yake.
 
Juzi nilikua napita huko wilayani Urambo mkoa wa Tabora, nilimuona huyu Ramadhani Ntuzwe akiwa anaiza bidhaa mchanganyiko za nyumbani kwenye duka la kawaida kabisa.

Baada ya kuulizia habari zake, niliambiwa jamaa alifilisika kabisa na akaanza biashara upya kwa kulikimbilia Urambo ili kuokoa maisha yake.
Kweli kabisa
 
Juzi nilikua napita huko wilayani Urambo mkoa wa Tabora, nilimuona huyu Ramadhani Ntuzwe akiwa anaiza bidhaa mchanganyiko za nyumbani kwenye duka la kawaida kabisa.

Baada ya kuulizia habari zake, niliambiwa jamaa alifilisika kabisa na akaanza biashara upya kwa kulikimbilia Urambo ili kuokoa maisha yake.
Ndio nyuma ya pazia walimfanyia kitu mbaya ndo maana yule mama kwenye mkutano na waziri mkuu alisema awezi kusema yote kuhofia usalama wake.
 
Hii ni serikali sikivu kua na amani jambo jema linaenda kafanywa kiongozi
 
Ukumbuke Wakati Wa Kifo Cha Jiwe.....Alisema Nini Vile.....
Haaminiki Muda Mwingi.....
 

Habari,

Wakuu kama tunafatilia habari na mitandao tunatambua wiki hii nchini wetu imetawaliwa na matukio mengi. Miongoni mwa tukio lililogusa vituo vya habari ni pamoja na Mgombo wa wafanya biashara wa Kariakoo.

Imekuwa sio kawaida kwa viongozi wetu kujitokeza kusikiliza migogoro ya Wananchi na kero za Wananchi. Nampongeza Waziri Mkuu Kasim Majaliwa kwa kujitokeza mbele na kusikiliza madukuduku ya Wananchi kiuwazi.

Pamoja na kumpongeza kujitokeza kusikiliza bado nahimiza kwamba asibaki kusikiliza kero tu ili kutuliza upepo bali iwe ni sehemu ya mchakato wa kutafuta suluhu ya kero hizi.

Zaidi ya hayo pia zipo kero nyingi na sehemu tofauti tofauti zinawakabili Watanzania ni vyema viongozi wetu wasiishie Kariakoo peke yake na pia wasisubiri mgomo na maandamano.

Tanzania bora ya kesho inawezekana.
Kero ni za kimfumo na kisheria ambazo zinahitaji mchakato wa Baraza la Mawaziri na Bunge..

Sijaona madai ya mtu binafsi sana sana labda hao waliopandikizwa na Chadema,mtu anasema eti TRA wanapata kiburi sababu ya Mwigulu,swali how? Anaweza thibitisha? Huo ni uzushi wa kijinga,TRA imekuwepo kabla ya Mwigulu na iliwaumiza watu wengi maana sio taasisi ya Waziri hiyo.
 
Ndio nyuma ya pazia walimfanyia kitu mbaya ndo maana yule mama kwenye mkutano na waziri mkuu alisema awezi kusema yote kuhofia usalama wake.
Dahhhhh......
Hapa nawqza kama wenye pesa kiasikile wanafanyiwa umafia, hii imekaaje kwa akina sisi...🤔
 
Kero ni za kimfumo na kisheria ambazo zinahitaji mchakato wa Baraza la Mawaziri na Bunge..

Sijaona madai ya mtu binafsi sana sana labda hao waliopandikizwa na Chadema,mtu anasema eti TRA wanapata kiburi sababu ya Mwigulu,swali how? Anaweza thibitisha? Huo ni uzushi wa kijinga,TRA imekuwepo kabla ya Mwigulu na iliwaumiza watu wengi maana sio taasisi ya Waziri hiyo.

Mkuu naomba kukuuliza swali moja [emoji4] wewe ni Mwigulu au ni Chawa wake ?
 
Mkuu naomba kukuuliza swali moja [emoji4] wewe ni Mwigulu au ni Chawa wake ?
Kwanza Simtetei ila sipendi chuki na kuongea watu na mie Sio Mwigulu Wala sio chawa wake ila nataka unipe ukweli na logic,yaani kero za TRA , Mwigulu anahusikaje?
 
Back
Top Bottom