Hongera Waziri Ummy Mwalimu kwa mkakati mpya wa kupambana na COVID19

Hongera Waziri Ummy Mwalimu kwa mkakati mpya wa kupambana na COVID19

Great Thinkers, ujumbe unaofuata unaonesha jinsi wizara ya afya ilivyojipanga kukabiliana na COVID19, kikao alichofanya na chama cha Madakitari (chini ya rais wao Dr Osati) kinatoa matumaini mapya kwa watanzania.

Mrejesho wa kikao cha wanataaluma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Habari za leo

Jana tarehe 27 Aprili, 2020; vyama vya kitaaluma vya afya nchini kikiwemo MAT tulikutana na timu ya Wizara ya Afya kujadiliana kuhusu mwenendo wa wa COVID-19 nchini. Kikao hiki ni matokeo ya mkutano wa vyama vyote wa tarehe 26 Aprili, 2020 kilichofanyika kupitia "zoom ". Tulijadili yafuatayo.

1. Upatikanaji wa PPEs Wizara

Mheshimiwa. Waziri Ummy Ally Mwalimu alisema tayari wameagiza mzigo wa PPEs unaotosheleza matumizi ya mwezi mzima; mzigo huo unategemewa kufika wakati wowote wiki hii. Pia wizara imepata fedha kiasi cha shilingi za kitanzania 9.6Billioni walioielekeza MSD kwa ajili ya kuagiza mzigo mwingine wa PPEs.

2. Wagonjwa kukataliwa kwenye hospitali mbalimbali

CMO na RMOs wameagizwa kushughulikia swala hili mara moja. Hii itaambatana na kuangalia upya mwongozo wa utumiaji wa PPEs bila wafanyakazi kuambukizwa. Sambamba na hilo watumishi wamehimizwa kufuata mwongozo wa IPC ili kuepuka maambukizi na hivyo wasiwakatae wagonjwa wanaopewa rufaa au kuja kwenye vituo vyao.

Kikao pia kiliridhia kwamba mafunzo ya IPC lazima yaendelee kwenye kila kituo cha kutolea huduma za afya. Pamoja na hayo tulikubaliana kuwa isolation centers ziongezeke hata kwenye hospitali za binafsi (private hospitals); kwa kuanzia hospitali hizi kupitia kwa Association of Private Health Facilities in Tanzania (APHFTA) wamekubaliana kutenga isolation za level 3 (level1, 2 and 3) katika kila wilaya ya mkoa wa Dar es Salaam na baadae mikoani, kwa ajili ya kuwaweka wagonjwa.

3. Ucheleweshwaji wa majibu ya COVID-19

Wizara imekubali kuongeza vituo vitatu kati ya tisa zenye uwezo wa kupima COVID-19. Kuanzia Jumanne ya wiki ijayo ya tarehe tarehe 5 May, 2020; maabara ya NIMR Dodoma itaanza kutoa majibu, ikifuatiwa na Mwanza na Mbeya. Changamoto imekuwa ni uwepo wa wataalam wanane tu wa maabara wanaoweza kuchakata majibu ya COVID-19. Kwa hiyo Mafunzo kwa wataalam wengine yameanza na watasambazwa kwenye vituo husika.

4. Mazishi ya waliofariki

Ikitokea mgonjwa amefariki kwenye hospitali, ndugu inabidi wahusishwe iwezekanavyo chini ya uangalizi wa wataalam wa afya kutoka manispaa husika kuhusu mazishi na eneo la kuzikia. Mganga mkuu wa wilaya (DMO) husika ataarifiwe kwa msaada zaidi ikiwa ni pamoja na magari na utaratibu wa mazishi bila kupoteza muda zaidi.

5. Contact tracing

Kwa upande wa Dar es Salaam ambapo tayari kuna maambukizi mengi kwenye jamii ni changamoto kuendelea na kuwatafuata "contacts" na pia ni vigumu kuwa weka wote ‘’isolation’’. Wizara walishauri kwa hatua tuliyo nayo sasa kwa mkoa wa Dar es Salaam kama mtu anahisi kuwa na dalili za COVID-19 aende kwenye kituo husika kwa ajili ya kuchukuliwa vipimo, na kurudi nyumbani huku wakiendelea kuchukua tahadhari zote ikiwemo kuvaa Barakoa na kujitenga na wengine. Mikoa mwingine ambayo ugonjwa haujasambaa sana waendelee na utaratibu wa "contact tracing".

6. Kuweka wagonjwa wenye dalili ndogo ndogo kwenye isolations

Kuhusu hili tulijadiliana na hatukufikia muafaka. Mheshimiwa Waziri akaomba wanataaluma tujadiliane halafu tumshauri kwenye hili. Maswali yakiwa; Je ni sahihi kuwa weka wagonjwa wenye dalili ndogo ndogo kwenye isolation ambazo tayari zimejaa au tuwape ushauri halafu wajitenge nyumbani mpaka Ikitokea wana dalili za hatari?. Hii itabidi tuitolee maoni sisi kama wanataaluma

7. Upungufu wa Damu salama kipindi hiki

kumeonekana kuna upungufu mkubwa sana wa damu salama katika benki za damu hasa kwa Dar es Salaam. Wito umetolewa kwa hospitali zote kupunguza kufanya/kutoa huduma ya upasuaji usio wa dharura ili kupunguza matumizi ya damu.

8. Utafiti kwenye eneo la COVID-19

Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) tayari inaendelea na tafiti tatu juu ya COVID-19 na pia imetoa mwongozo wa utafiti kwa wakati huu wa COVID-19. Utafiti pia unahusisha dawa za miti Shamba (tiba mbadala) ikiwa ni pamoja na kujifukiza.

9. Ufafanuzi ya juu ya kauli ya waziri kuwa hakuna watumishi walioambukizwa

Mheshimiwa Waziri alisema alichomaanisha ni kuwa hakuna mtumishi anayehudumia wagonjwa kwenye isolations aliyeambukizwa. Kwa sababu labda walipewa Mafunzo zaidi ya namna ya kujikinga. Alisema anajua kuwa kuna watumishi wameambukizwa wakiwa EMD/Mapokezi na OPDs (idara ya magonjwa ya nje). Kwahiyo ameomba Mafunzo zaidi yaelekezwa kwa watumishi wote.

NB: Tunaomba maoni yenu juu ya kipengela Namba 6 hapo juu.

Nawasilisha

Dr Elisha Osati, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT).

Kuna mikakati ya mazishi lakini hakuna ya kuzuia maambukizi?

Tunataka mikakati ya kuzuia maambukizi haya mengine ni kelele tu.
 
Wakuu naona wengi tuna criticize badala ya kutoa maoni nini kifanyike. Imefika hatua tunashutumiana, kukashifiana na kutoka nje ya mada.

Nilitegemea tusisitize upatikanaji wa vifaa kinga na tiba (tunaambiwa hakuna tiba lakini watu wanapona). Mfano, kupata vipimo sahihi ni muhimu sana kwa sasa. Hivyo kila hospitali ya mkoa iwe na huduma hiyo.

Kuwa na mashine za kusaidia kupumua za kutosha ingawa hata wenzetu walioendelea hiyo ni changamoto, kujenga wodi za dharura hata kwenye viwanja vya michezo, tumeona vilabu Fulani huko Uingereza wamejitolea viwanja vyao vitumike ktk kutoa huduma. Tunao wataalam wa majengo ya dharura au hata jeshi linaweza kutumika. Tuache siasa.
 
Great Thinkers, ujumbe unaofuata unaonesha jinsi wizara ya afya ilivyojipanga kukabiliana na COVID19, kikao alichofanya na chama cha Madakitari (chini ya rais wao Dr Osati) kinatoa matumaini mapya kwa watanzania.

Mrejesho wa kikao cha wanataaluma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Habari za leo

Jana tarehe 27 Aprili, 2020; vyama vya kitaaluma vya afya nchini kikiwemo MAT tulikutana na timu ya Wizara ya Afya kujadiliana kuhusu mwenendo wa wa COVID-19 nchini. Kikao hiki ni matokeo ya mkutano wa vyama vyote wa tarehe 26 Aprili, 2020 kilichofanyika kupitia "zoom ". Tulijadili yafuatayo.

1. Upatikanaji wa PPEs Wizara

Mheshimiwa. Waziri Ummy Ally Mwalimu alisema tayari wameagiza mzigo wa PPEs unaotosheleza matumizi ya mwezi mzima; mzigo huo unategemewa kufika wakati wowote wiki hii. Pia wizara imepata fedha kiasi cha shilingi za kitanzania 9.6Billioni walioielekeza MSD kwa ajili ya kuagiza mzigo mwingine wa PPEs.

2. Wagonjwa kukataliwa kwenye hospitali mbalimbali

CMO na RMOs wameagizwa kushughulikia swala hili mara moja. Hii itaambatana na kuangalia upya mwongozo wa utumiaji wa PPEs bila wafanyakazi kuambukizwa. Sambamba na hilo watumishi wamehimizwa kufuata mwongozo wa IPC ili kuepuka maambukizi na hivyo wasiwakatae wagonjwa wanaopewa rufaa au kuja kwenye vituo vyao.

Kikao pia kiliridhia kwamba mafunzo ya IPC lazima yaendelee kwenye kila kituo cha kutolea huduma za afya. Pamoja na hayo tulikubaliana kuwa isolation centers ziongezeke hata kwenye hospitali za binafsi (private hospitals); kwa kuanzia hospitali hizi kupitia kwa Association of Private Health Facilities in Tanzania (APHFTA) wamekubaliana kutenga isolation za level 3 (level1, 2 and 3) katika kila wilaya ya mkoa wa Dar es Salaam na baadae mikoani, kwa ajili ya kuwaweka wagonjwa.

3. Ucheleweshwaji wa majibu ya COVID-19

Wizara imekubali kuongeza vituo vitatu kati ya tisa zenye uwezo wa kupima COVID-19. Kuanzia Jumanne ya wiki ijayo ya tarehe tarehe 5 May, 2020; maabara ya NIMR Dodoma itaanza kutoa majibu, ikifuatiwa na Mwanza na Mbeya. Changamoto imekuwa ni uwepo wa wataalam wanane tu wa maabara wanaoweza kuchakata majibu ya COVID-19. Kwa hiyo Mafunzo kwa wataalam wengine yameanza na watasambazwa kwenye vituo husika.

4. Mazishi ya waliofariki

Ikitokea mgonjwa amefariki kwenye hospitali, ndugu inabidi wahusishwe iwezekanavyo chini ya uangalizi wa wataalam wa afya kutoka manispaa husika kuhusu mazishi na eneo la kuzikia. Mganga mkuu wa wilaya (DMO) husika ataarifiwe kwa msaada zaidi ikiwa ni pamoja na magari na utaratibu wa mazishi bila kupoteza muda zaidi.

5. Contact tracing

Kwa upande wa Dar es Salaam ambapo tayari kuna maambukizi mengi kwenye jamii ni changamoto kuendelea na kuwatafuata "contacts" na pia ni vigumu kuwa weka wote ‘’isolation’’. Wizara walishauri kwa hatua tuliyo nayo sasa kwa mkoa wa Dar es Salaam kama mtu anahisi kuwa na dalili za COVID-19 aende kwenye kituo husika kwa ajili ya kuchukuliwa vipimo, na kurudi nyumbani huku wakiendelea kuchukua tahadhari zote ikiwemo kuvaa Barakoa na kujitenga na wengine. Mikoa mwingine ambayo ugonjwa haujasambaa sana waendelee na utaratibu wa "contact tracing".

6. Kuweka wagonjwa wenye dalili ndogo ndogo kwenye isolations

Kuhusu hili tulijadiliana na hatukufikia muafaka. Mheshimiwa Waziri akaomba wanataaluma tujadiliane halafu tumshauri kwenye hili. Maswali yakiwa; Je ni sahihi kuwa weka wagonjwa wenye dalili ndogo ndogo kwenye isolation ambazo tayari zimejaa au tuwape ushauri halafu wajitenge nyumbani mpaka Ikitokea wana dalili za hatari?. Hii itabidi tuitolee maoni sisi kama wanataaluma

7. Upungufu wa Damu salama kipindi hiki

kumeonekana kuna upungufu mkubwa sana wa damu salama katika benki za damu hasa kwa Dar es Salaam. Wito umetolewa kwa hospitali zote kupunguza kufanya/kutoa huduma ya upasuaji usio wa dharura ili kupunguza matumizi ya damu.

8. Utafiti kwenye eneo la COVID-19

Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) tayari inaendelea na tafiti tatu juu ya COVID-19 na pia imetoa mwongozo wa utafiti kwa wakati huu wa COVID-19. Utafiti pia unahusisha dawa za miti Shamba (tiba mbadala) ikiwa ni pamoja na kujifukiza.

9. Ufafanuzi ya juu ya kauli ya waziri kuwa hakuna watumishi walioambukizwa

Mheshimiwa Waziri alisema alichomaanisha ni kuwa hakuna mtumishi anayehudumia wagonjwa kwenye isolations aliyeambukizwa. Kwa sababu labda walipewa Mafunzo zaidi ya namna ya kujikinga. Alisema anajua kuwa kuna watumishi wameambukizwa wakiwa EMD/Mapokezi na OPDs (idara ya magonjwa ya nje). Kwahiyo ameomba Mafunzo zaidi yaelekezwa kwa watumishi wote.

NB: Tunaomba maoni yenu juu ya kipengela Namba 6 hapo juu.

Nawasilisha

Dr Elisha Osati, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT).
Nchi hii imejaa wajinga watupu kuanzia juu mpaka chini .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afya kama sekta kuna madaktari, manesi na wengine. Mna vyama vikiwamo vya madaktari (MAT), manesi nk.

Hivi kweli mmesalimisha utaalamu wenu kwa wanasiasa. Mkafumbwa midomo mkafumbika na kuwa watazamaji tu wa ugonjwa huu hadi kufikia hali ilivyo sasa?

Sekta hii imekumbwa na nini?

Kwanini mmeshindwa kuwa wazi cha nini kifanyike hali utaalamu mnao?

Ndugu zetu mnatuangusha.
 
Jitihada nzuri hadi hapo, naomba tusiwe watu wakupinga na kubeza kila kitu. Hii ni hatua muhimu sana na kipekee nimpongeze Waziri wa afya kwa kushirikisha wataalam na kuomba ushauri wa nini kifanyike kwa wakati huu.

Hapo kwenye namba sita inahitaji elimu ya kutosha, kuna watu wenye dalili ndogondogo wananchi waelimishwe namna ya kuishi na hawa watu majumbani bila kueneza maambukizi zaidi ikiwa mazingira yanaruhusu.

Tuonyeshe u great thinker wetu kwenye kutoa mapendekezo na ushauri ya nini kifanyike.
 
Habari za chini nilizopata 3dys ago kuwa wahudumu kama 80 wameugua rona...! Na serikali haitak kukiri!...hatarious..
 
Wakuu naona wengi tuna criticize badala ya kutoa maoni nini kifanyike. Imefika hatua tunashutumiana, kukashifiana na kutoka nje ya mada.

Nilitegemea tusisitize upatikanaji wa vifaa kinga na tiba (tunaambiwa hakuna tiba lakini watu wanapona). Mfano, kupata vipimo sahihi ni muhimu sana kwa sasa. Hivyo kila hospitali ya mkoa iwe na huduma hiyo. Kuwa na mashine za kusaidia kupumua za kutosha ingawa hata wenzetu walioendelea hiyo ni changamoto, kujenga wodi za dharura hata kwenye viwanja vya michezo, tumeona vilabu Fulani huko Uingereza wamejitolea viwanja vyao vitumike ktk kutoa huduma. Tunao wataalam wa majengo ya dharura au hata jeshi linaweza kutumika. Tuache siasa.
Ubarikiwe mkuu kwa ushauri, wewe ni muungwana sana. Ni muhimu kushirikiana kipindi hiki, umetoa maoni mazuri sana
 
Kwenye UKIMWI mliambiwa muavoid unsafe sex, blood transmission nk..

Covid 19 tumeambiwa tukae ndani kama hakuna ulazima wa kukutoa nje ukishindwa mkuu kasema tujifukize
 
Jitihada nzuri hadi hapo, naomba tusiwe watu wakupinga na kubeza kila kitu. Hii ni hatua muhimu sana na kipekee nimpongeze Waziri wa afya kwa kushirikisha wataalam na kuomba ushauri wa nini kifanyike kwa wakati huu.

Hapo kwenye namba sita inahitaji elimu ya kutosha, kuna watu wenye dalili ndogondogo wananchi waelimishwe namna ya kuishi na hawa watu majumbani bila kueneza maambukizi zaidi ikiwa mazingira yanaruhusu.

Tuonyeshe u great thinker wetu kwenye kutoa mapendekezo na ushauri ya nini kifanyike.
Ni kweli maana ukiangalia hosp kwenyewe hapatoshi, nadhani jamii inaweza kuelemishwa
 
Ndukidi hayo mambo ya kupanikishana tuachane nayo, tuweke mikakati ya mass testing ila hakuna mambo ya kutoa taarifa, kwa sababu hatuna briefing ya HIV au Kisukari so why iwe COVID19???? Kwanini tukopy kila kitu?

Je kuna umuhimu wa kutaja maambukizi ya malaria? Cancer??? Au kuna umuhimu wa kutaja vifo vya malaria??? Nadhani mikakati ya kujikinga ni bora zaidi. Tuungane kumpongeza Waziri Ummy kwa hatua aliyochukua
Good!
 
Tupunguze kulalamika..Hii ni vita ya Mtu moja moja..
Hata tuandike magazeti Hapa JF haibadilishi kiti,
cha msingi nunua satinaiza(Sanitaizer), Barakoa wagawie wasio Nazo,
usichoke kutoa elimu ya kujikinga.
 
Loud and clear
Ndukidi hayo mambo ya kupanikishana tuachane nayo, tuweke mikakati ya mass testing ila hakuna mambo ya kutoa taarifa, kwa sababu hatuna briefing ya HIV au Kisukari so why iwe COVID19???? Kwanini tukopy kila kitu?

Je kuna umuhimu wa kutaja maambukizi ya malaria? Cancer??? Au kuna umuhimu wa kutaja vifo vya malaria??? Nadhani mikakati ya kujikinga ni bora zaidi. Tuungane kumpongeza Waziri Ummy kwa hatua aliyochukua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu naona wengi tuna criticize badala ya kutoa maoni nini kifanyike. Imefika hatua tunashutumiana, kukashifiana na kutoka nje ya mada.

Nilitegemea tusisitize upatikanaji wa vifaa kinga na tiba (tunaambiwa hakuna tiba lakini watu wanapona). Mfano, kupata vipimo sahihi ni muhimu sana kwa sasa. Hivyo kila hospitali ya mkoa iwe na huduma hiyo. Kuwa na mashine za kusaidia kupumua za kutosha ingawa hata wenzetu walioendelea hiyo ni changamoto, kujenga wodi za dharura hata kwenye viwanja vya michezo, tumeona vilabu Fulani huko Uingereza wamejitolea viwanja vyao vitumike ktk kutoa huduma. Tunao wataalam wa majengo ya dharura au hata jeshi linaweza kutumika. Tuache siasa.

Uko sahihi mkuu, huu ni wakati wa kuweka mbali siasa kwa sasa.

Kwa hali ilivyo sasa hivi, hospitali zote kama sio nyingi kwa sasa wahudumu wote kuanzia mapokezi wapatiwe vifaa vya kujikinga kwa sababu, mgonjwa atakuja kutaka huduma na hajui hali yake ya maambukizi ya Corona na akishaingia hospital hadi kujua ikiwa anaweza kuwa na maambukizi/ dalili tayari wahudumu wa awali tayari watakua wameshaambukizwa.

Kuna haja ya kuanzisha kituo chenye wataalam wakawa wanatoa ushauri iwe kwa simu au mitandao kwa wenye kujisikia dalili za maambukizi. Wakapatiwa ushauri na nini cha kufanya au wapi pa kwenda kupata huduma stahiki.
 
Hivi mtu kama huna cha kuandika si unakaa kimya tu kwani lazima wote tuanzishe siredi

Sent using Jamii Forums mobile app
Khantwe omba msamaha haraka sana kabla sijaweka mambo yako wazi
Niombe msamaha kwa kosa gani? Weka hayo mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨
🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️
 
Uko sahihi mkuu, huu ni wakati wa kuweka mbali siasa kwa sasa.

Kwa hali ilivyo sasa hivi, hospitali zote kama sio nyingi kwa sasa wahudumu wote kuanzia mapokezi wapatiwe vifaa vya kujikinga kwa sababu, mgonjwa atakuja kutaka huduma na hajui hali yake ya maambukizi ya Corona na akishaingia hospital hadi kujua ikiwa anaweza kuwa na maambukizi/ dalili tayari wahudumu wa awali tayari watakua wameshaambukizwa.

Kuna haja ya kuanzisha kituo chenye wataalam wakawa wanatoa ushauri iwe kwa simu au mitandao kwa wenye kujisikia dalili za maambukizi. Wakapatiwa ushauri na nini cha kufanya au wapi pa kwenda kupata huduma stahiki.
Mkuu mass testing linaweza kuwa suluhisho ili mgonjwa akienda hosp ajulikane status yake. Otherwise wauguzi na ma dakitari wakiathirika wote ina maana wataeneza ugonjwa kwa kila anayetembelea hosp na aliyeko hosp.

Serikali ianze mkakati wa kununua vifaa toka kwa wajasiriamali USA, maana kuna zaidi ya 200 approved test kit.
 
😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨😨
🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️🏃‍♀️
Kaja inbox kuomba msamaha
 
Mkuu mass testing linaweza kuwa suluhisho ili mgonjwa akienda hosp ajulikane status yake. Otherwise wauguzi na ma dakitari wakiathirika wote ina maana wataeneza ugonjwa kwa kila anayetembelea hosp na aliyeko hosp. Serikali ianze mkakati wa kununua vifaa toka kwa wajasiriamali USA, maana kuna zaidi ya 200 approved test kit.


Uwezo huo tunao? Na Je, tumeshatengeneza mazingira ya namna ya kukabiliana na hao watakaokua wanagundulika wana maambukizi?
Kwa sasa tu karanteen na self isolation zinatushinda kwa kuwa watu ni wengi.

Mimi sio mtaalam wa afya ila naamini mass testing ikifanyika watakaokua hawana huo ugonjwa ni wachache sana ni vile sio kila mtu daliki ziko wazi na wengine haiwapi homa wala mafua ila wanaambukiza wengine.

Mbaya zaidi uchukuaji wa sample nao hauko rafiki sana, mtu kujitolea inahitaji moyo.

Lakini penye nia pana njia, wataalam wanaweza kuja na njia mbadala.
 
Back
Top Bottom