Hongereni yanga na simba kwa ushindi wa leo lakini michuano mtaianza hatua itayofuata

Hongereni yanga na simba kwa ushindi wa leo lakini michuano mtaianza hatua itayofuata

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Nawapongeza kwa kufanya vizuri kwenye mechi za mwanzo ni mwanzo mzuri kwa timu zote mbili itawajengea hali ya kujiamini na kujipanga vizuri kwa michezo ijayo,.

Pamoja na kushinda timu zote 2 zimekutana na timu ambazo zina viwango vya chini, ukianzia Nyassa big bullet ya malawi ni timu inayofanya vizuri kwenye ligi yao lakini ni ligi isiyokuwa na ushindani ukilinganisha na ligi ya Tanzania na icho ndicho kilichowahukumu leo.

Unaweza kuwa bora miongoni mwa wabovu na ukatawala eneo lako, kwaiyo ushindi wa simba usiwafanye wakavimba vichwa kwamba wameishinda timu bora na wakajisahau kurekebisha mapungufu yao kuelekea kukutana na Red arrows au Ile timu ya angola, vivyo hivyo kwa yanga wanatakiwa kujipanga kisawasawa kuelekea kukutana na Al hilal au St george ya ethiopia, apo ndipo kuna kipimo sahihi awa zahlan wamewafumbua macho kwamba utakiwi kudharau timu yoyote kwenye michuano hii maana mpaka inafika hapo aikufika kwa bahati mbaya, papara yao na presha ya kutaka kufunga bila mipango ndiyo iliyowakosesha mabao kipindi cha kwanza.

Nafikiri Nabi aliliona hilo akawatuliza kipindi cha pili, Timu zote mbili zinatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kufanikiwa kutinga hatua ya makundi sio lelemama, Timu itakayojisahau kwa kujiona imekamilika baada ya kuwaondoa vibonde basi itakula kwao hatua inayofuata
 
Nawapongeza kwa kufanya vizuri kwenye mechi za mwanzo ni mwanzo mzuri kwa timu zote mbili itawajengea hali ya kujiamini na kujipanga vizuri kwa michezo ijayo, Pamoja na kushinda timu zote 2 zimekutana na timu ambazo zina viwango vya chini, ukianzia Nyassa big bullet ya malawi ni timu inayofanya vizuri kwenye ligi yao lakini ni ligi isiyokuwa na ushindani ukilinganisha na ligi ya Tanzania na icho ndicho kilichowahukumu leo, unaweza kuwa bora miongoni mwa wabovu na ukatawala eneo lako, kwaiyo ushindi wa simba usiwafanye wakavimba vichwa kwamba wameishinda timu bora na wakajisahau kurekebisha mapungufu yao kuelekea kukutana na Red arrows au Ile timu ya angola, vivyo hivyo kwa yanga wanatakiwa kujipanga kisawasawa kuelekea kukutana na Al hilal au St george ya ethiopia, apo ndipo kuna kipimo sahihi awa zahlan wamewafumbua macho kwamba utakiwi kudharau timu yoyote kwenye michuano hii maana mpaka inafika hapo aikufika kwa bahati mbaya, papara yao na presha ya kutaka kufunga bila mipango ndiyo iliyowakosesha mabao kipindi cha kwanza, nafikiri Nabi aliliona hilo akawatuliza kipindi cha pili, Timu zote mbili zinatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kufanikiwa kutinga hatua ya makundi sio lelemama, Timu itakayojisahau kwa kujiona imekamilika baada ya kuwaondoa vibonde basi itakula kwao hatua inayofuata
Sio nyie mlikuwa mnasema big bullet ni unbeaten hadi mechi za kimataifa?
Leo kwa vile Simba kashinda tayari imekuwa timu dhaifu?

Sasa unasemaje timu imesafiri kwa bus na imefika Jana saa 5 usiku inawakazia dk 45 pamoja na kuwa mko nyumbani?

Utopolo bhana,yaani wewe ni wa kuwafundisha Simba kazi yao wanayoijua zaidi?
Pole sana utopolo
 
Sio nyie mlikuwa mnasema big bullet ni unbeaten hadi mechi za kimataifa?
Leo kwa vile Simba kashinda tayari imekuwa timu dhaifu?

Sasa unasemaje timu imesafiri kwa bus na imefika Jana saa 5 usiku inawakazia dk 45 pamoja na kuwa mko nyumbani?

Utopolo bhana,yaani wewe ni wa kuwafundisha Simba kazi yao wanayoijua zaidi?
Pole sana utopolo
Mpira una njia zake sio kindi au kimpumu kufika na kujichotea, kinachoitajika ni ushindi aijalishi umeshinda kipindi gani, sababu ya wao kufika usiku uwezi jua plan yao ilikuwaje kila timu na mbinu zake na haiondoi wala kupunguza ubora wa yanga ata wangekuja juzi bado wangekalia tu tunachosema timu zote ni vibonde kulingana na aina ya ligi zao kwaiyo bwetekeni kuwa mko bora mtakachokutana nacho msije kuanza kupayuka kuwa matola na mgunda wafukuzwe
 
Rivers,Al ahly tripoli n.k zinafahamika...Lkn Kote Ulimwengu Sijawahi Kuisikia timu Inaitwa Zalani..... Ndo timu Ya Wapi.?
 
Acha kujidanganya wewe.
Kama Mimi nadanganya nenda kawaulize wachezaji na viongozi wa Simba watakupa majibu.
Kaduguda alishawahi kusema tangu ameingia Simba Enzi za Sunderland anaona nirahisi kumfunga Ahly ya Misri kuliko kumfunga Yanga.
 
Chimba ni timu ya ukweli haina papara .
Saivi yanga akili zenu ni Chimba tu leo mnafunga kimawazo na kesho yake mnafungwa hadi manara kaona timu ya mazingira ni dili hakuna ni uchawi tu akasepa .
Kwanz walimchanganya akili manara akawa hajielewi alipojitambua akasepa timu ni chimba .
Chimba chimba mnyama
 
Ili kuondoa kidomodomo Caf waruhusu Simba acheze na Yanga, na Zalaani wacheze na Big bullet atakaye shinda asonge mbele.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umeanza kuchanganyikiwa???
Al hilal na St George zinakusubiri Huko, poleeeeeeh.
 
Ili kuondoa kidomodomo Caf waruhusu Simba acheze na Yanga, na Zalaani wacheze na Big bullet atakaye shinda asonge mbele.
Hiki ndo mnachokiwaza, nyinyi subirini mtolewa na Al Hilal ili mrudi NBC (kama kawaida yenu) msubirie kucheza na Simba Sc.
 
Back
Top Bottom