Hospitali binafsi kutopokea kadi za NHIF kuanzia Januari 1 2024

Mbona ni taasisi isiyojitambua?
Hatujawahi kuwa na taasisi ya kijinga/kipuuzi kama hii toka tupate uhuru!

Yaani hii taasisi (kama kweli urais ni taasisi) inataka kutuaminisha kwamba gharama za maisha zimepanda kila sehemu isipokuwa tu upande wa sekta ya Afya?

Just imagine mfumko wa bei (inflation) toka 2016; petroli lita imepanda toka 1,600/= hadi zaidi ya 3,200/=
Nauli ya daladala toka 300/= hadi 600/=
Mche wa Sabuni (Jamaa) toka 1,500/= hadi 3,500/= n.k

Hata panadol nadhani (sina uhakika) ukienda Pharmacy kwa sasa huwezi kuipata kwa ile bei ya Tsh. 10/= kwa kidonge kama tulivyozoea bali ni kuanzia 50/= na kuendelea. Halafu wanatokea tu wapuuzi wachache kwa lengo la kuzua taharuki kwa watoa huduma wa private ili sisi ambao huwa tunakwenda kutibiwa huko kutokana na kukimbia ujinga ujinga wa hospitali za serikali tuanze kuteseka?!

Hii si sawa kabisa.

Acheni ujinga, kuweni serious na Afya za watu.
 
Nakubaliana na Wewe kwa 100%
 
Unapoandika haya, unajua hizi hospitali zinadai kiasi gani huko NHIF? Himiza serikali yako iwajibike! Au unafikiri hizo hospitali madawa wanaokota? Watumishi wanalipwaje? Anzisha wewe hospitali yako ukatoe huduma for free.
 
Unapoandika haya, unajua hizi hospitali zinadai kiasi gani huko NHIF? Himiza serikali yako iwajibike! Au unafikiri hizo hospitali madawa wanaokota? Watumishi wanalipwaje? Anzisha wewe hospitali yako ukatoe huduma for free.
Watu wanapenda kuongea tuu lkn ukiangalia kisomi zaidi hao wafanyabiashara wapo sahihi.

Wengi wanalalamika hawalipwi kwa wakati .
 
Nhif, haina pesa,pesa zinaliwa, na ma CCM, hosptari binafsi, zinafsnya biashara, hazina ruzuku, zisipopata pesa kwa wakati kwa huduma walizotoa(kupitia nhif), mustakabali wake na ajira za wafanyakazi, zinakuwa mashakani, haya, mamifuko hayalipi pesa, kabisa.
Yaani, umuhudumie, mgonjwa, dawa,consultation, harafu pesa, ije baada, ya, miezi Sita! Hiyo ofc si utwfunga?
 
Tuwekee jina la hiyo dawa ili tuwe na ushahidi wa kutosha, kinyume na hapo utakuwa unajenga hoja tu.
 
Ndugu zangu ngoja niwambie, kama unapesa zako Kwa sasa wekeza kwenye nywele za wadada tu, afya ni mzigo kuendesha.
 
Kumbe wametishia nikajua wameshatangaza. Serikali imejenga vituo vya afya vya kutosha wasitishe tu wenye shida ya biashara watatoa huduma.
 
Hawezi Kigoma. Hicho kitabakia kuwa kitisho tu. Atakayegoma kutii agizo la serikali tutamfutia leseni yake asitoe huduma hapa nchini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…