Hospitali inapomwambia Mwanachama wa NHIF Dawa fulani haipatikani kwenye Bima, Mgonjwa anathibitishaje kwamba ni kweli?

Wizara ya Afya ilishatoa orodha
 
Sasa hivi hii bima ya afya ni kama wamekosa mwelekeo. Ni mwendo wa kuchangia kika kitu. Sasa kuna haja gani ya kuwa na bima kama hii?
 
Sikatai mkuu Bima ya Afya wana mapungufu,lakini mtoa mada shida yake haipo kwa watu wa Bima,yeye kaelekeza kero yake kwa watu wa Hospital. Watu wa Hospital wanafuata maelekezo ya Bima,hiki mpe mgonjwa hiki usimpe,Huduma hii toa hii usitoe kama sio level yako...Sasa mgonjwa unapoanza kuhoji uhalali wa maelekezo unayopewa na mtoa huduma manake huna imani nae. Ikumbukwe kwamba ni Jukumu la Bima kuweka mifumo itakayofanya wagonjwa wake waonekane wafalme. Kuhusu ishu ya vipimo ni mambo ya Levels za Hospital,Pia kuna justification ya kipimo husika kana una ulazima kufanyiwa ama la kulingana na tatizo lako,Then kuna ishu ya mkataba,kituo kikiingia mkataba na bima wanaainisha vipimo vyote wanavyotoa,manake wakija kuongeza kipimo kingine hiko kinakuwa hakipo kwenye mkataba mpaka pale watu wa bima watakapokuja kukagua na kujiridhisha kuwa huduma husika ipo kweli. Ukienda kituo hiko lazima watakwambia ulipie kipimo husika kwa cash.
 
Daktari akikwambia una malaria huulizi utajuaje kama ni Malaria kweli?
kama wewe ni daktari bas usije omba uje nitibu.
Kuna mwenzako Pale hospitali around Kalolen Arusha baada ya kuona sielewi nikaanza kuhoji akajua mi ndio wale wale akaanza kuniletea pigo sizo ili tu kuni cut short niondoke niache kuuliza details za recomendations zake, akanitajia kipimo kinaitwa blood culture, nikasema sawa , mwisho wa siku nikaguza ofisi yake darasa kumpa shule kimueleza in details kuhus hizo culture mpaka akauliza bro we ni daktari?? Nikamwambia hapana, ni raia tu nilie serious na issue zangu za afya so kama hujui unachokisema ni busara kutoongopa.

Mpaka leo ni mshkaji wangu
 
Kwahiyo ulimuuliza ili kumpima wakati unajua?
 


Inasikitisha sana.
 


Swali la msingi sana hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…