#COVID19 Hospitali ya Bugando yakumbwa na upungufu wa mitungi ya Oksijeni kwa Wagonjwa wa Kupumua

#COVID19 Hospitali ya Bugando yakumbwa na upungufu wa mitungi ya Oksijeni kwa Wagonjwa wa Kupumua

Tapeli wewe, huna lolote..

Moshi ipi hiyo unayoizungumzia wewe?

Eti hali mbaya?? Mbaya gani?

Nyie matapeli ni wa kutandika bakora kabisa!
Sipo hapa kubishana,kuleta hofu ama kutangaza habari za chanjo ila katika kipindi hicho nilichokitaja nimehudhuria misiba sita, njia kuu ya kuingilia Arusha kutoka Moshi (Usa River) kuna pub inaitwa Rotterdam biashara ilikuwa imepwaya tuliokuwa tunakula pale ni watu wachache mno, zikisimama basi za wanaoenda ama kutoka kwenye misiba ndio angalau wanapata wateja. Ninacho kielezea ni hali halisi , hospitali za KCMC na Seliani hali ilikuwa ngumu mimi nimeuguza ndugu yangu wa damu kipindi hicho vitu vingine sio kukaza kichwa tu na kuleta kiburi uonekane mjuaji.

Arusha niliona taasisi za serikali kimya kimya waliweka hali ya tahadhari kubwa kujikinga na "matatizo ya upumuaji" barakoa zilikuwa zinavaliwa, sanitizer kila kona. Arusha imepoteza madaktari bingwa kiutani utani na matatizo ya upumuaji.

Moshi misiba ilikuwa mingi na ilikuwa haiishi wakienda baada ya wiki wanarudi lakini hakuna aliyeongelea mfano tu ni hii familia ambayo huenda iliongelewa kwa kuwa walikuwa ni familia ya profesa kutoka chuo kikubwa.👇


Sio kila kitu tushindane au tulete ujuaji, kama hayajakukuta mshukuru Mungu na endelea na maisha yako, kila mtu ana uhuru wa kuchagua namna ya kuishi katika mlipuko wa ugonjwa huu kwa hiyo tusilazimishane kukuza ama kupuuza hali halisi tuiseme hali kama ilivyokuwa, na ilivyo sasa. Kwa sasa Arusha tumetulia si kama ilivyokuwa mwanzoni mwa mwaka huu 2021.
 
Aisee..
Ukibishana na Wapumbavu, watakupeleka kwenye level yao, na kukushinda kwa uzoefu........
Corona corona corona Rwanda wametangaza lockdown nyingine na wanafunzi wameanza kurudishwa nyumbani.

Kumbuka Rwanda ni ya kwanza kabisa kuchanja watu wake.
 
Huo ugonjwa kuna wapumbavu wanauchukulia kirahisi rahisi mpaka mtu apoteze mtu wake wa karibu ndio atatia adabu..

By the way wote tumeona matokeo ya walioudharau huu ugonjwa tukianza iwa dikteta mwenyewe..
Corona corona corona Rwanda wametangaza lockdown nyingine na wanafunzi wameanza kurudishwa nyumbani.

Kumbuka Rwanda ni ya kwanza kabisa kuchanja watu wake.
 
Unakuta hospital yenyewe ina mitungi mitatu halafu unakuja na uzi kuwa imekumbwa na uungufu. Tuambie kwanza ina jumla ya mitungi mingapi iliyo active na mingapi inatumiwa na wagonjwa hadi muda huu.
Hoja nzuri
 
Ngoja tuone,kama tutatoboa bila lockdown this time around🙄🙄🙄🙄
Niko suala ambalo haliwezekani, lochdown itasababisha machafuko kwa maana watu huhitaji kutoka ili kupata riziki zao ukiwafungia inakuwaje?

Tungeweza kubenefit kama system za nida zipo active tangu 2015
 
Mama yuko under test. Lakini uhalisia wa corona utaujua mtaani. Ni ngumu sana kumshawushi MTU kuvaa hiyo mambo. Acha wanasiasa wateseke, ila mtaani raia tunadunda tu...

Kwamba:

"Ushauli wangu:
1. Ushi kama vile hakuna covid
2. Usikubali kutishwa na barakoa
3. Treat hii kitu kama mafua tunazouguaga
4. Usikubali kupandishiwa pressure na huu msemo wa wimbi la 3."


Hata yule aliyekwenda alifuata.ushauri wako na anaendelea kuuzingatia kule chattle.
 
Usipotoa taarifa kama hizi za upungufu wa vifaa ama kuzika majeneza tupu hupati fedha za misaada za korona

Unaonaje ushauri huu?

IMG_20210707_031423_318.jpg



Pia tathmini huru hii?

IMG_20210706_211331_804.jpg
 
Upinzani ukija kichukua nchi tunalipiga chini,hatuwezi kuenzi MTU aliyeharibu demokrasia,mtekaji nk.

By the way hata litengenezwe kwa dhahabu tupu haizidi milioni mia moja,kuna upigaji hapo.
 
Ni kwa sababu wengi wenu kisomo mlichonacho ni duni, hamuelewi hata misingi ya uchumi na uzalishaji mali.
EeenHee Heee, angalia punguani kama huyu hapa!

Uchumi,...; ni bora kuliko maisha ya binaadamu. Huo uchumi utakuwa wa nini kama wanaotakiwa kuufaidi wanakufa!

Hao waliofungia, uchumi wa Tanzania unawazidi kitu gani?

Uchumi wa Tanzania unajitegemea wenyewe duniani?

Hamjaweka 'lockdown', lakini mbona uchumi umedoda?

Huu sio ujinga, ni upumbavu.
 
Huu ugonjwa ni vita ya kiuchumi Magu alikuwa amewashtukia. Lazima tujiulize kwa nini watu wamedunda tangu May 2020 hadi leo bila barakoa wala chanjo lakini sasa hivi tumeanza kutishana na kutiana hofu kuwa korona ipo tuvae barakoa tena kwa lazima?

Unajua ukiwa huna ushahidi wa madhara ya COVID-19 lazima utakua mropokaji wa style hii! Wengine tumeshapoteza mpaka ndugu kwasababu ya Corona! Huyo aliyewajaza hayo maneno yeye yuko wapi leo?
 
Ukiona unaota ndoto za mchana ujue karibu utakuwa chizi. Upinzani wa kuchukua utoke wapi ?
Upinzani ukija kichukua nchi tunalipiga chini,hatuwezi kuenzi MTU aliyeharibu demokrasia,mtekaji nk.

By the way hata litengenezwe kwa dhahabu tupu haizidi milioni mia moja,kuna upigaji hapo.
 
Wewe hiyo hela ni ndogo sana kwa serikali. Ni hela ya chai na mikate kwa siku moja tu.

Acha kuiaibisha serikali na kuitukana...
Sasa wewe! Kama mtu kaondoka na korona badala ya kumuenzi kwa kutumia pesa hiyo kununua mitungi ya gesi kuokoa maisha ya wengine mnatengeneza sanamu?

Hiyo ni akili au matope? Mtu mwenyewe mshagundua kuwa hata sanamu zikichongwa zinamkataa kabisa, si muache tuu aende zake?

20210706_100311.jpg
 
sasa unaonea wivu mpaka sanamu, MIL 420 hio sasa si ela ya ndan ya dakika kumi serikali imeingiza, whats special about hio sanamu isiwepo?
Je, kwasasa ndio kipaumbele?

Je, hili ni la muhimu kuliko huduma za msingi za jamii zinazochechema?

Je, hili ni la lazima sana kiasi kwamba lisipofanyika kuna watu wataathirika kiafya, kijamii na kiuchumi?

Kuingiza milion 400 kwa dakika kumi tu kwa serikali hakumaanishi kuwe na matumizi mabovu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom