DOKEZO Hospitali ya Kairuki wahuni wachunguzwe. Kila mgonjwa wa Bima anaumwa Helicobacter pylori (H. Pylori)

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hii ni hatari sana, tutakuwa taifa la ajabu sana
Maisha yamekuwa magumu siku hizi kila mtu anajiongeza pale alipo, kwenye maduka ya dawa wauzaji wanaongeza cha juu, huko hospitalini nako wanaangalia madawa ya bei mbaya ndio wanakusukumizia ugonjwa wake, ilimradi pesa itoke tu.
 
sawa sawa
 
Aisee pengine tunaweza tofautiana. Mimi mtoto wangu wa darasa la 4 alikuwa analalamika sana tumbo kwa wiki atalalamika hata mara 3. Nilienda na wife kairuki na kukutwa na hiyo Pyroli. Baada ya kutumia madawa yao ambayo ni mengi kwa kweli, sijasikia mtoto akilalamika tumbo, mwezi kariba wa 4 huu. Huu ni ushuhuda wangu.
 
Ndo nmetoka aga khan ya mwanza hapa nmepima hicho kipmo wamenambia nna mdudu anaesababisha vidonda vya tumbo...sasa kama ni utapel wanafanya kwa kwel wanatukosea
 
Kwenye hili suala la Bima ya Afya serikali ije na mfumo ambao mgonjwa akishapata matibabu hasa hawa wagonjwa wa OPD zile sms zinazotumwa kwenye simu zioneshe na mchanganuo/ gharama ya matibabu ya ugonjwa husika, hizi hospitali binafsi wamekuwa wagumu sana kujaza gharama kwenye zile sheet
 
Huyo jamaa Jana baada ya kumwambia nmetest h pylori + akanambia nitume 250000+10000 ya kutolea ..hapo nikajua huyo Mathew ni mchumia tumbo tu hakuna doctor hapo
 
Wezi, ndio maana Angela ananenepa, kumbe hiki ndio chanzo
 
Hii hali imewahi nitokea kwenye hospitali moja Ruvuma, bahati mbaya sikupata mawazo kama yako ya kwenda kuhakiki kwenye hospitali nyingine, mbaya zaidi sikuwa nimebeba kadi ya bima kwa hiyo ikawa ni mwendo wa cash.
Mfuko wa bima ndo maana unaelemewa maaana kuna ujanja mwingi sana kwenye mahospitali.
 
Sio Hospital hiyo pekee !
 
Pesa zetu zinapigwa ambazo ndio zinazoziendesha hizo Kampuni za Bima !
 
Hili ni jambo linalonifanya hata nikiumwa nisiende hospital, Ukienda hospital hata na mafua, Utarudi na Lundo la dawa. Madoctor wamekuwa wanafanya biashara si kuhudumia wagonjwa.
Iko vile bandugu na hasa hasa ukiwa na Bima 😳 !
 
Hii ni hatari sana, tutakuwa taifa la ajabu sana
Wale Wakubwa walioanzisha tabia ya kupiga pesa ili watajirike ndio wameleta hii balaa Nchini !
Hapo zamani Enzi za Nyerere watu hawakuwa hivi !
Wazee wenzangu nawauliza je ni kweli au nasema uongo ndugu zanguni ???!
 
Kuna wimbi la maabala nyingi zinazosimamiwa na vijana kugundua wadudu hao tu. Hasa private hospitals.

Binti yangu wa miaka 8 nilimpeleka hospital moja pamoja na mimi tukiwa na matatizo ya tumbo wote tulikutwa na huyo mdudu. Ikanitoka kama 200K. Lakini tulipoenda hospital ya Rufaa ya serikali ghalama zilikuwa chini sana. Baadae ikagundilika ana tatizo la hernia ya kitovu akafanyiwa Op na tatizo la maumivu ya tumbo likawa limeisha.

Hao watu wanamezesha watoto midawa ya ajabu sana.
 
Nikamchukua mtoto na mimi tukaenda kupima bochi na Kairuki kote tulikutwa hatuna hiyo H. pylori mtoto wangu amekutwa na matosi yanayompa homa basi.
Sijakuelewa vizuri hapa mkuu, hii "bochi na kairuki" ni nini hasa; hizi nazo ni hospitali nyingine au vipi.

Hayo unayo eleza hapo kuhusu kinacho fanyika kwenye hivyo vipimo, kama ni kweli, huo ndio utapeli wenyewe unao fanywa na kuivuruga hiyo Bima ya Afya. Hayo ni makosa ya jinai haswa wakigundulika kuyafanya.

Kama hiyo "bochi" ni hospitali nyingine uliko peleka vipimo ili kuhakikisha usahihi wa majibu uliyo pewa huko Kariuki, ni njia nzuri; ila bila shaka inakuongezea gharama.

Mimi ninge pendekeza uwaone viongozi wa hospitali hiyo uwaeleze kuwa kuna tatizo hilo. Wakipuuza, wajue wanajiweka kwenye matatizo na wanaweza kushitakiwa mahakamani kwa kufanya kazi 'unethically' namna hiyo, mbali na kuvunja sheria.
 
Huo ni uvunjifu mkubwa sana wa maadili ya kazi za hao watu, na ni uvunjifu wa sheria.
Wanajiweka kwenye hatari ya kushitakiwa hawa.
 
Nadhani kama tungeweza wote kwa umoja wetu kubadilisha neno ujanja kulitumia na badala yake tukasema kuna Uwizi mwingi sana !
Neno Ujanja ni sifa ya mtu kuwa mwerevu sana ! Ambayo ni sifa nzuri !
 
Dawa za H .pylori ni kali sana na unatumia kwa siku 30.
Sasa kama wanakupachika ugonjwa wa uongo ni hatari sana kwa figo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…