Hospitali ya Taifa Muhimbili kutoisimamia tena Mloganzila, sasa Mloganzila kujiendesha yenyewe kuanzia Julai 2022

Hospitali ya Taifa Muhimbili kutoisimamia tena Mloganzila, sasa Mloganzila kujiendesha yenyewe kuanzia Julai 2022

Thread Starter

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2017
Posts
1,378
Reaction score
1,045
Hospitali ya MLOGANZILA itasimama yenyewe na kutoka chini ya usimamizi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuanzia Julai 2022. Hayo yamesemwa leo 18/3/2022 na Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu alipoitembelea Hospitali hiyo na kusema kuwa serikali imejiridhisha na jinsi hospitali hiyo inavyojiendesha na ni wakati umefika sasa hospitali hiyo ijitegemee.

Aidha katika hatua nyingine, waziri huyo wa Afya amezindua mtambo wa kuzalisha hewa ya oksijeni (Oxygen Plant) hospitalini hapo, mradi huo umefadhiliwa na Ubalozi wa Korea nchini kupitia taasisi ya ''Korea Foundation for International Healthcare (KOFIH)''

Soma pia: Hospitali ya MUHAS Mloganzila (MAMC) yawekwa chini ya uangalizi maalum wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)

My take: Kwa maana hiyo uongozi uliokuwepo utavunjwa na wafanyakazi walioazimwa kutoka Muhimbili watarejea Upanga na taasisi itakuwa separate chini ya wizara, je mabadiliko haya yataleta tija kwa changamoto zilizoikumba tangu ianzishwe mnamo 2016-2017? Anyways tunatarajia mema na kila la heri wana Mloganzila katika kuisimamisha taasisi yenu bila kutegemea usimamizi wa Muhimbili Taifa au MUHAS..

ummy.jpg
 
When it was conceived, it was meant to be an independent specialized hospital!! Jiwe akaja badalisha Mipango Akihisi kuwa watu wa Vasco Dagama walitarajia kufanya ufisadi hivyo kuwapiga pin kwa kuiweka chini ya Muhimbili!!
 
Hivi neno mloganzila lina maana gani?
Màana kwa kule dodoma
nzila-njia,mloga-kigagula(mlogaji/mshirikina)

Ukipangilia vizuri hapo unapata maana.
Ila ile hospital inatisha.
Nilikuwa naongea na mchawi mstaafu(alikamatwa kwny mkutano wa injiki wa walokole akaamua kuokoka)
Anasema ukipeleka mgonjwa wako kati ya hii hospital au mhimbili km ni mwepesimwepesi ataishia kuliwa supu mtakutana na msiba wa ndugu yenu.
Yaan ni vingunguti ya binadamu iwe,mimba,vichanga,wazee,vijana n.k ni kufagia tu hawakosi mboga.
 
Huku mtaani kwetu wanaamini mgonjwa wako akilazwa Mloganzila jiandae kisaikolojia kuna jambo litatokea... ngoja tuone ikijitegemea
Kwa mtu mwenye kufikiri sawa sawa bila mihemko hilo ni kawaida.
Ile sio zahanati kwamba unaenda ukiwa na mafua, yani umeshindikana koote huko maana yake chances za kupona sio kubwa wala sio uzembe wa wahudumu pamoja na kwamba uzembe upo sana mahospitalini kwa ngazi zote

Hatutegemei idadi ya vifo katika hospital ya rufaa ya kanda mfano KCMC ilingane na MNH au Mloganzila
 
Kwa mtu mwenye kufikiri sawa sawa bila mihemko hilo ni kawaida.
Ile sio zahanati kwamba unaenda ukiwa na mafua, yani umeshindikana koote huko maana yake chances za kupona sio kubwa wala sio uzembe wa wahudumu pamoja na kwamba uzembe upo sana mahospitalini kwa ngazi zote

Hatutegemei idadi ya vifo katika hospital ya rufaa ya kanda mfano KCMC ilingane na MNH au Mloganzila
Sijui,hebu tuone maoni ya wadau wengine wanasemaje... Mimi hayo ni maoni ya mtaani kwetu
 
Back
Top Bottom