Hospitali ya Taifa Muhimbili yajibu hoja za Wana JamiiForums kuhusu vifo Hospitali ya Muhimbili-Mloganzila

Hospitali ya rufaa ni sehemu ya wagonjwa mahututi, sishangai wakifariki.

Sitegemei kusikia mtu kafiwa AAR, maana pale watu wanaenda na mafua, wakiwa na cancer wanaenda Muhimbili.
 
Muhimbili njooni jf hata kwa ID fake mpate madini
 
siata, Kwanini msiweke figures (instead mmeweka % tu) katika mortality rate nyie uongozi wa Mloganzila hospital!??.

Mbona MNH- upanga wameweka figures with %!??.

Kunakitu nahisi kinafichwa hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwe na utaratibu sasa wakufunguliana kesi za ‘medical negligence’ vifo ambavyo chanzo chake ni uzembe walipe fidia. Ndio njia pekee yakulazimishana ku maintain professionalism and quality standards kwenye kutoa huduma.

Watu wetu hufa hospitali kinamna isyokuwa na ufafanuzi wa kina,kisha sisi tunakubali na kubeba maiti,
Kumbe ilikuwa uzembe wa madaktari,au negligence.
Ingelikuwa Kenya mambo yangekuwa mengine .
 
Watu wanajisifu wagonjwa kuongezeka na vifo kupungua
Siasa bwana ![emoji16][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo hata mimi limeniduwaza, nimeshindwa kuelewa wagonjwa wanaongezeka sabab ya trust kwa hospitali husika ama wamejiimarisha na kujitanua kiasi cha kuweza kuhudumia wagonjwa wengi in a given time.

Kinyume chake ongezeko la wagonjwa ni dalili mbovu kwa nchi kwa sababu hizi
1. Kuna mazingira hatari kwenye jamii ambayo yana attract contraction ya magonjwa.
2. Level ya recurrency ya magonjwa baada ya magonjwa kutibiwa ni kubwa sn.

Zaidi ya hapo,kwa uzoefu wa kitanzania idadi ya ongezeko la wagonjwa ilitakiwa iendane na ongezeko la vifo.

Maelezo ya Prof. kwa kifupi nayachukulia km nyoka aliyekurupuka toka pangoni baada ya tuhuma.

Nashauri uchunguzi huru ufanyike,maisha sio kitu cha kuchezea...we only live once.
 
Exactly. This is what I wz talking about.

There's something fishy here.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Majibu ya profesa ni siasa tupu inayolenga kujilinda asitumbuliwe. Naendelea kushauri kama alivyopendekeza mtoa mada anayejibiwa kwa post hii na profesa, Mh Magufuli wakati akitokea chato mapumzikoni apitie hapo hospital ajionee ukweli.
 
Je, upasuaji aliofanyiwa Tundu Lisu ungefanyika hapo, angeendelea kuwa hai leo (Angepona) ?
Ndiyo maana tunasema Tundu Lisu ana makusudi na Mungu. We angalia, kitendo cha malaika gabriel kuwaongoza kuwa asitibiwe Muhimbili, ni Mngu tu! Huyu angelikufa kabla ya kupata chupa ya pili ya damu muhimbili! Lisu atakuja kuwa Mtume wa Kweli wa Mungu!
 
Hahahahah.. ebhana eeh!!

Yani kwa jinsi pepa lilivyo nyanya ukiamua kupiga section one tu unauhakika wa kutoka na 70% nzima,unausanya pepa unasepa hata sali moja upotezi katika chumba cha mtihani.

Kumbe ndii maana A's za kufa mtu mi nikajua madogo wapiga msuli nowdays kumbe wanapewa pepa za form two ACSE.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
data,
Mkuu wewe umeona tatizo lilipoanzia. Ni kweli kabisa na nadiriki kusema si kwenye afya tu bali sekta zote za nchi yetu wamejaa wahitimu vilaza. Kelele zilipigwa muda mrefu mamlaka zikapuuza na sasa tunavuna tulichopanda. Kuna wahitimu wa vyuo vikuu wengi sana hawana uelewa wa form four leaver aliyesoma shule nzuri.

Ni majanga. Hii issue ni kama ujengaji na mpangilio wa jiji la Dar. Tulifumbia macho siku za nyuma na sasa tumeshafikia stage ambayo kurekebisha itachukuwa ni gharama kubwa sana.
 
Tanzania ni taifa la Vilaza,
Watu wetu hufa hospitali kinamna isyokuwa na ufafanuzi wa kina,kisha sisi tunakubali na kubeba maiti,
Kumbe ilikuwa uzembe wa madaktari,au negligence.
Ingelikuwa Kenya mambo yangekuwa mengine .
Hapo hapo kabla uchungu aujaisha wa kumpoteza ndugu kwa uzembe wao tena unaambiwa uilipie kuitoa maiti.

Mtu anafika hospitali hawana blood bank (sijui dunia gani hospitali inayotoa huduma ya accident and emergency inakosa damu) ndugu ndio anaambiwa aende kutoa damu.

Halafu unafika ulipoelekezwa wahusika hawaoni sababu ya urgency, huyo mgonjwa atapona kweli.
 
Mbatia kaongea sanaa juu ya Elimu.. Kapiga kelele sana Bungeni Bunge la Sita.

Wacha tuendelee vuna tulichopanda.
 
Hawa madokta walio huko Mloganzila na sehemu nyingine nyiingi.

Bila shaka ndo wale wa Kikwete wa BRN... Division 5..
Wakaja wengine wa GPA....

Tumecheza na ELIMU sana.
Na bado. Huo ni mwanzo tu.
Ndio kwanza mawio.

Hali ni mbaya sanaa kuliko maelezo.

Naamini Ifikapo 2030 jua litakuwa utosini.


Na mimi na familia yangu tutakuwa tumesepa Tanzagiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…