Hospitali zaanza kutafuta wagonjwa mitandaoni, Wasanii wahusishwa!

Hospitali zaanza kutafuta wagonjwa mitandaoni, Wasanii wahusishwa!

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
yyy.jpeg


Shilole ameonekana akitangaza hospitali hiyo hapo kwenye picha na kusisitiza wagonjwa waende na kwamba ni hospitali Bora.

Kimaadili si sawa, ni kama hospitai hiyo inataka kupata watu waumwe ili wakatibiwe huko na ni muhimu sana kujua kwamba ni kama ndvyo basi bwana mochwari naye aombee ajali na vifo ili apate wateja.

Ummy Mwalimu, Jafari Liana na wahusika wengine tunaomba mshughulikie na mtupe watanzania msimamo kuhusu kutangaza hospitali kwenye media.
Katika nchi nyingi, hospitali na vituo vya afya vinaweza kukutana na vikwazo au marufuku kuhusu kujitangaza kwa sababu mbalimbali. Sababu hizi zinaweza kujumuisha zifuatazo:-

Maadili ya Matibabu: Katika tamaduni za Tanganyika na mifumo ya afya, matangazo ya hospitali yanaweza kuonekana kama yasiyo na maadili kwa sababu huduma za afya zinachukuliwa kuwa za kipekee na zinapaswa kulenga zaidi huduma bora kwa wagonjwa kuliko faida za kibiashara.

  1. Kuzuia Upotoshaji: Hospitali hupigwa marufuku kujitangaza ili kuepuka madai ya upotoshaji au matangazo yanayoweza kuwa na habari za kupotosha kuhusu uwezo wao wa matibabu au matokeo yanayotarajiwa. Hii ni muhimu kwa sababu afya ya wagonjwa iko hatarini, na matangazo yasiyo sahihi yanaweza kusababisha madhara makubwa.
  2. Usawa na Upatikanaji: Marufuku ya matangazo inaweza kusaidia kudumisha usawa katika upatikanaji wa huduma za afya. Hospitali kubwa zenye rasilimali nyingi zinaweza kuwa na uwezo wa kutangaza kwa wingi, na hivyo kuvutia wagonjwa wengi zaidi, huku hospitali ndogo zenye rasilimali chache zikibaki nyuma.
  3. Uangalizi wa Gharama: Matangazo yanaweza kuongeza gharama za uendeshaji wa hospitali, ambazo zinaweza kupitishwa kwa wagonjwa kupitia ada za juu za matibabu. Kuzuia matangazo kunasaidia kuhakikisha kuwa rasilimali za hospitali zinatumika moja kwa moja kwa huduma za wagonjwa badala ya matumizi ya masoko.
  4. Kanuni za Serikali na Sera za Afya: Serikali na vyombo vya udhibiti vya afya vinaweza kuweka sheria zinazodhibiti matangazo ya hospitali kama sehemu ya sera za afya za umma. Lengo ni kuhakikisha kuwa huduma za afya zinatolewa kwa usawa na kuzuia ushindani usiofaa kati ya watoa huduma za afya.
MWISHO:Watanganyika wenzangu, kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.Kwa wanawake wa DAr waliopitia uzazi ambao kidogo mifuko yao ni mirefu wanamjua dokta fulani gynocologist mzuri sana, ana asili ya kule nanii, hakuna asiye mjua, hana tangazo popote ila anatafutwa usiku na mchana, sababu kuu ni uwezo wake wa kazi.
Tukiruhusu wajitangaze ni mvurugano.

Da' Ummy Mwalimu, wewe ni Waziri mchapa Kazi , naomba uchukue hatua kali, lakini pia matangazo ya waganga wa kienyeji kwenye media wakijinasibu kutibu magonjwa fulani na kuwakataza wagonjwa wasiende hospitali.
 
Hii ni biashara kama zilivyo biashara zingine kama za majeneza au magari ya kusafirisha maiti.

Hivyo sioni ubaya kujitangaza maana mtu amefanya uwekezaji ili apate faida na si vinginevyo
Hapana proffessional business kama udaktari, uwakili kimaadili huruhusiwi kutangaza. Zinajitangaza zenyewe kwa huduma bora. Ukiacha mfumo wa matangazo utaua ubora wa huduma. Usije ukafikiri hiyo biashara kama kuuza machungwa au chu.pi kariakoo
 
Bora hata huyu anatangaza Hospitali ili wagonjwa wakatibiwe huko ambao tayari ni wagonjwa na wanahangaika kupata Hospitali iliyo bora na nafuu kwao ili kupata matibabu,

Vipi kuhusu wanaouza Misalaba na Majeneza? Nakumbuka kuna kiongozi fulani aliwahi kuwapa zawadi watu wa jimbo lake Gari la kubebea maiti.
 
Makanisani hospital zinatangazwa. Wewe bado kijana mdogo inaonekana. Banana zoro mwaka flani alikua akiitangaza CCBRT, Kairuki imetanngazwa sana Clouds Fm na TV, Vipi mloganzila hukuona wasanii wakiitangaza, peter msechu hukumuona, mpaka akasema kawekewa puto. Vipi agha khann na polycllinic zake mbona zimetangazwa sana ITV.
Wewe uko wapi.
Kutangaza sio kufanya watu waumwe. Nikuwaelekeza huduma fulani na safi zinapatikana mahala flani.
 
Back
Top Bottom